1A wiara jest gruntem tych rzeczy, których się spodziewamy i dowodem rzeczy niewidzialnych.
1Kuwa na imani ni kuwa na hakika ya mambo tunayotumainia; kusadiki kabisa mambo tusiyoyaona.
2Albowiem przez nią świadectwa doszli przodkowie.
2Maana wazee wa kale walipata kibali cha Mungu kwa sababu ya imani yao.
3Wiarą rozumiemy, iż świat jest sprawiony słowem Bożem, tak iż rzeczy, które widzimy, nie stały się z rzeczy widzialnych, ale z niczego.
3Kwa imani sisi tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu; vitu vinavyoonekana kutoka vitu visivyoonekana.
4Wiarą lepszą ofiarę ofiarował Abel Bogu, niżeli Kain, przez którą świadectwo otrzymał, że jest sprawiedliwy, jakoż sam Bóg świadectwo dał o darach jego, a przez te umarłszy jeszcze mówi.
4Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu iliyokuwa bora zaidi kuliko ile ya Kaini. Kwa imani yake alikubaliwa na Mungu kuwa mwadilifu; Mungu mwenyewe alizikubali sadaka zake. Kwa imani yake ingawa amekufa, bado ananena.
5Wiarą Enoch jest przeniesiony, aby nie oglądał śmierci i nie jest znaleziony, przeto że go Bóg przeniósł; albowiem pierwej niż jest przeniesiony, miał świadectwo, że się podobał Bogu.
5Kwa imani Henoki alichukuliwa na Mungu, asipate kufa. Hakuonekana tena kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Maandiko yasema kwamba kabla ya kuchukuliwa kwake, yeye alikuwa amempendeza Mungu.
6A bez wiary nie można podobać się Bogu; albowiem ten, co przystępuje do Boga, wierzyć musi, że jest Bóg, a że nagrodę daje tym, którzy go szukają.
6Basi, pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Kwa maana kila mtu anayemwendea Mungu ni lazima aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba huwatuza wale wanaomtafuta.
7Wiarą obwieszczony będąc od Boga Noe o tem, czego jeszcze nie było widzieć, uczciwości wyświadczając, przygotował korab ku zachowaniu domu swego, przez który potępił świat i stał się dziedzicem sprawiedliwości tej, która jest z wiary.
7Kwa imani Noa alionywa na Mungu juu ya mambo ya baadaye ambayo hakuweza kuyaona bado. Alimtii Mungu, akajenga ile safina ambamo aliokolewa yeye pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo ulimwengu ulihukumiwa, naye Noa akapokea uadilifu unaotokana na imani.
8Wiarą powołany będąc Abraham, usłuchał Boga, aby poszedł na ono miejsce, które miał wziąć za dziedzictwo i wyszedł, nie wiedząc, dokąd idzie.
8Kwa imani Abrahamu alimtii Mungu alipoitwa aende katika nchi ambayo Mungu angempa iwe yake. Ingawa hakujua alikokuwa anakwenda, Abrahamu alihama.
9Wiarą mieszkał w ziemi obiecanej jako w cudzej, mieszkając w namiotach z Izaakiem i z Jakóbem, spólnymi dziedzicami tejże obietnicy.
9Kwa imani aliishi kama mgeni katika nchi aliyoahidiwa na Mungu. Aliishi huko katika hema kama walivyoishi Isaka na Yakobo, ambao pia walishiriki ahadi ileile.
10Albowiem oczekiwał miasta mającego grunty, którego sprawcą i budownikiem jest Bóg.
10Maana Abrahamu alikuwa akingojea mji wenye misingi imara, mji ambao Mungu mwenyewe ndiye fundi aliyeubuni na kuujenga.
11Wiarą także Sara wzięła moc ku przyjęciu nasienia i mimo czasu wieku porodziła, gdyż miała za wiernego tego, który obiecał.
11Kwa imani hata Sara aliamini kwamba Mungu hutimiza ahadi zake, kwa hiyo akajaliwa kuchukua mimba ingawaje alikuwa amepita umri.
12A przetoż z jednego, i to obumarłego, rozpłodziło się potomstwo jako mnóstwo gwiazd niebieskich i jako piasek niezliczony, który jest na brzegu morskim.
12Kwa hiyo, kutoka katika mtu huyo mmoja, Abrahamu, ambaye alikuwa kama amekufa, walitokea watu wengi wasiohesabika kama vile nyota za mbinguni na mchanga wa pwani.
13Według wiary umarli ci wszyscy, nie wziąwszy obietnic, ale z daleka je upatrując i cieszyli się niemi, i witali je i wyznawali, iż są gośćmi i przychodniami na ziemi.
13Watu hawa wote walikufa wakiwa na imani. Walikufa kabla ya kupokea mambo ambayo Mungu alikuwa ameahidi, lakini kwa mbali waliyaona, wakashangilia, na kukiri wazi kwamba wao walikuwa wageni na wakimbizi duniani.
14Bo ci, którzy tak mówią, jawnie okazują, iż ojczyzny szukają.
14Watu wanaosema mambo kama hayo, huonyesha wazi kwamba wanaitafuta nchi yao wenyewe.
15A wprawdzie, gdyby byli na onę pamiętali, z której byli wyszli, mieli dosyć czasu wrócić się zaś.
15Kama wangalikuwa wanaifikiria nchi walikotoka zamani, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
16Ale oni lepszej żądają, to jest niebieskiej; przetoż i sam Bóg nie wstydzi się nazywać Bogiem ich, bo im miasto zgotował.
16Lakini sasa wanataka nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Ndiyo maana Mungu haoni haya wakimwita yeye Mungu wao, kwa sababu yeye mwenyewe amekwisha watayarishia mji.
17Wiarą ofiarował Abraham Izaaka, będąc kuszony, a ofiarował jednorodzonego ten, który był wziął obietnicę.
17Kwa imani, Abrahamu alimtoa mwanae Isaka sadaka wakati Mungu alipomjaribu. Huyo Abrahamu ndiye aliyekuwa amepokea ahadi ya Mungu, lakini, hata hivyo, alikubali kumtoa dhabihu mwanae wa pekee,
18Do którego rzeczono: W Izaaku tobie będzie nazwane nasienie;
18ingawa Mungu alikuwa amemwambia: "Wazawa wako watatokana na Isaka."
19Uważając to, iż Bóg może i od umarłych wzbudzić; skąd go też w podobieóstwie zmartwychwstania przyjął.
19Abrahamu aliamini kwamba Mungu anaweza kuwafufua wafu: na kwa namna fulani kweli Abrahamu alimpata tena mwanae kutoka wafu.
20Wiarą około przyszłych rzeczy błogosławił Izaak Jakóba i Ezawa.
20Kwa imani Isaka aliwabariki Yakobo na Esau, wapate baraka zitakazokuja baadaye.
21Wiarą Jakób umierając, każdemu z synów Józefowych błogosławił i pokłonił się podparłszy się na wierzch laski swojej.
21Kwa imani Yakobo alipokuwa karibu kufa, aliwabariki kila mmoja wa wana wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiegemea ile fimbo yake.
22Wiarą Józef umierając, o wyjściu synów Izraelskich wzmiankę uczynił i z strony kości swoich rozkazał.
22Kwa imani Yosefu alipokuwa karibu kufa, alinena juu ya kutoka kwa Waisraeli katika nchi ya Misri, na pia akawaachia maagizo kuhusu mifupa yake.
23Wiarą narodziwszy się Mojżesz, był ukryty przez trzy miesiące od rodziców swoich, przeto że widzieli nadobne dzieciątko i nie bali się wyroku królewskiego.
23Kwa imani wazazi wa Mose walimficha huyo mtoto kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuzaliwa kwake. Walimwona kuwa ni mtoto mzuri, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
24Wiarą Mojżesz, będąc już dorosłym, zbraniał się być zwany synem córki Faraonowej,
24Kwa imani Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
25Raczej sobie obrawszy złe rzeczy cierpieć z ludem Bożym, niżeli doczesną mieć z grzechu rozkosz,
25Aliona ni afadhali kuteseka pamoja na watu wa Mungu kuliko kufurahia raha ya dhambi kwa kitambo kidogo.
26Za większe pokładając bogactwo nad skarby Egipskie urąganie Chrystusowe; bo się oglądał na odpłatę.
26Alitambua kwamba kuteseka kwa ajili ya Masiha kuna faida kubwa zaidi kuliko utajiri wote wa nchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia tuzo la baadaye.
27Wiarą opuścił Egipt, nie bojąc się gniewu królewskiego; bo jakoby widział niewidzialnego, mężnie sobie poczynał.
27Kwa imani Mose alihama kutoka nchi ya Misri bila kuogopa hasira ya mfalme; na wala hakurudi nyuma, kwani alikuwa kama mtu aliyemwona yule Mungu asiyeonekana.
28Wiarą obchodził wielkanoc i wylanie krwi, aby ten, który tracił pierworodnych, nie dotknął się ich.
28Kwa imani aliadhimisha siku ya Pasaka, akaamuru damu inyunyizwe juu ya milango, ili yule Malaika Mwangamizi asiwaue wazaliwa wa kwanza wa Israeli.
29Wiarą przeszli przez morze Czerwone, jako po suszy, o co kusiwszy się Egipczanie, potonęli.
29Kwa imani watu wa Israeli walivuka bahari ya Shamu, kana kwamba ilikuwa nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo walikufa maji.
30Wiarą mury Jerycha upadły, gdy je obchodzono przez siedm dni.
30Kwa imani kuta za mji wa Yeriko zilianguka watu wa Israeli walipokwisha zunguka kwa muda wa siku saba.
31Wiarą Rachab wszetecznica nie zginęła wespół z nieposłusznymi, przyjąwszy z pokojem szpiegów do gospody.
31Kwa imani Rahabu aliyekuwa malaya hakuangamia pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa sababu aliwakaribisha wale wapelelezi.
32A cóż więcej mam mówić? Bo by mi czasu nie stało, gdybym miał powiadać o Giedeonie i o Baraku, i o Samsonie, i o Jefcie, i o Dawidzie, i o Samuelu, i o prorokach.
32Basi, niseme nini zaidi? Wakati hauniruhusu kueleza juu ya Gedeoni, Baraki, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii.
33Którzy przez wiarę zwalczyli królestwa, czynili sprawiedliwość, dostępowali obietnic, lwom paszczęki zawierali;
33Kwa imani hawa wote walipigana vita na wafalme, wakashinda. Walitenda mambo adili, wakapokea yale aliyoahidi Mungu. Walifunga vinywa vya simba,
34Zagaszali moc ognia, uchodzili ostrza mieczów, mocnymi się stawali z niemocnych, mężnymi bywali na wojnie, wojska cudzoziemców do uciekania przywodzili.
34Walizima mioto mikali, waliepuka kuuawa kwa upanga. Walikuwa dhaifu lakini walipata nguvu. Walikuwa hodari katika vita wakashinda majeshi ya kigeni.
35Niewiasty odbierały umarłych swoich wzbudzonych; a drudzy są na próbach rozciągnieni, nie przyjąwszy wybawienia, aby lepszego dostąpili zmartwychwstania.
35Na, wanawake walioamini walirudishiwa wafu wao wakiwa wamefufuliwa. Baadhi yao walikataa kufunguliwa, wakateswa mpaka kufa ili wapate kufufuliwa na kuingia katika maisha bora zaidi.
36Drudzy zasię pośmiewisk i biczowania doświadczyli, nadto i związek i więzienia.
36Wengine walidhihakiwa na kupigwa mijeledi, na wengine walifungwa minyororo na kutupwa gerezani.
37Byli kamionowani, piłą przecierani, kuszeni, mieczem zabijani, chodzili w owczych i kozich skórach; byli w niedostatku, w ucisku, w niewczasach;
37Walipigwa mawe, walipasuliwa vipandevipande, waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi, walikuwa watu maskini, walioteswa na kudhulumiwa.
38(Których nie był świat godzien;) tułali się po pustyniach i po górach, i jaskiniach, i jamach ziemi.
38Ulimwengu haukustahili kuwa na watu hao. Walitangatanga jangwani na mlimani, wakaishi katika mashimo na mapango ya ardhi.
39A ci wszyscy świadectwo otrzymawszy przez wiarę, nie dostąpili obietnicy.
39Watu hawa wote walionekana kuwa mashujaa kwa sababu ya imani yao. Hata hivyo, hawakupokea yale ambayo Mungu aliwaahidia,
40Przeto, że Bóg o nas coś lepszego przejrzał, aby oni bez nas nie stali się doskonałymi.
40maana Mungu alikuwa ameazimia mpango ulio bora zaidi kwa ajili yetu; yaani wao wangeufikia ukamilifu wakiwa pamoja nasi.