1Potemem widział drugi cud na niebie wielki i dziwny, to jest siedm Aniołów mających siedm plag ostatecznych, iż przez nie skoóczony jest gniew Boży.
1Kisha nikaona ishara nyingine mbinguni, kubwa na ya kushangaza. Palikuwa hapo malaika saba wenye mabaa makubwa saba ya mwisho. Kwa mabaa hayo makubwa saba, ghadhabu ya Mungu imekamilishwa.
2I widziałem, jakoby morze szklane zmieszane z ogniem; a tych, co zwycięstwo otrzymali nad oną bestyją i nad obrazem jej, i nad piętnem jej, i nad liczbą imienia jej, stojących nad morzem szklanem, mających cytry Boże.
2Kisha nikaona kitu kama bahari ya kioo, imechanganywa na moto. Nikawaona pia wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake na ambaye jina lake lilitajwa kwa ile tarakimu. Watu hao walikuwa wamesimama kando ya hiyo bahari ya kioo, wakiwa na vinubi walivyopewa na Mungu.
3A śpiewali pieśó Mojżesza, sługi Bożego, i pieśó Barankową, mówiąc: Wielkie i dziwne są sprawy twoje, Panie Boże wszechmogący! sprawiedliwe i prawdziwe są drogi twoje, o królu świętych!
3Walikuwa wakiimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwanakondoo: "Bwana Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makuu mno! Ewe Mfalme wa mataifa, njia zako ni za haki na za kweli!
4Któż by się ciebie nie bał, Panie! i nie wielbił imienia twego? gdyżeś sam święty, gdyż wszystkie narody przyjdą i kłaniać się będą przed obliczem twojem, że się okazały sprawiedliwe sądy twoje.
4Bwana, ni nani asiyekucha wewe? Nani asiyelitukuza jina lako? Wewe peke yako ni Mtakatifu. Mataifa yote yatakujia na kukuabudu maana matendo yako ya haki yameonekana na wote."
5A potemem widział, a oto otworzony był kościół przybytku świadectwa na niebie.
5Baada ya hayo nikaona Hekalu limefunguliwa mbinguni, na ndani yake hema ionyeshayo kuwapo kwa Mungu.
6I wyszło z kościoła siedm onych Aniołów, mających siedm plag, obleczonych płótnem czystem i świetnem, i przepasanych na piersiach złotemi pasami.
6Basi, wale malaika saba wenye mabaa saba wakatoka humo Hekaluni, wakiwa wamevaa nguo za kitani safi zenye kung'aa, na kanda za dhahabu vifuani mwao.
7A jedno ze czworga zwierząt dało siedmiu Aniołom siedm czasz złotych, pełnych gniewu Boga żyjącego na wieki wieków.
7Kisha, mmojawapo wa vile viumbe vinne akawapa hao malaika saba mabakuli ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, aishiye milele na milele.
8I napełniony jest kościół dymem od chwały Bożej i od mocy jego, a nie mógł nikt wnijść do kościoła, aż się skoóczyło siedm plag onych siedmiu Aniołów.
8Hekalu likajaa moshi uliosababishwa na utukufu na nguvu ya Mungu, na hakuna mtu aliyeweza kuingia Hekaluni mpaka mwisho wa mabaa makubwa saba ya wale malaika saba.