Polish

Swahili: New Testament

Revelation

17

1I przyszedł jeden z siedmiu Aniołów, którzy mieli siedm czasz, i rzekł do mnie, mówiąc mi: Chodź, okażę ci osądzenie onej wielkiej wszetecznicy, która siedzi nad wodami wielkiemi,
1Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na bakuli akaja, akaniambia, "Njoo, mimi nitakuonyesha adhabu aliyopewa yule mzinzi mkuu, mji ule uliojengwa juu ya maji mengi.
2Z którą wszeteczeóstwo płodzili królowie ziemi i upili się winem wszeteczeóstwa jej obywatele ziemi.
2Wafalme wa dunia wamefanya uzinzi pamoja naye; na wakazi wa dunia wamelewa divai ya uzinzi wake."
3I odniósł mię na puszczę w duchu. I widziałem niewiastę siedzącą na szarłatnoczerwonej bestyi, pełnej imion bluźnierstwa, która miała siedm głów i dziesięć rogów.
3Kisha, Roho akanikumba, akaniongoza mpaka jangwani. Huko nikamwona mwanamke ameketi juu ya mnyama mwekundu. Mnyama huyo alikuwa ameandikwa kila mahali majina ya makufuru; alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.
4A ona niewiasta przyobleczona była w purpurę i w szarłat, i uzłocona złotem i drogim kamieniem, i perłami, mając kubek złoty w ręce swej, pełen obrzydliwości i nieczystości wszeteczeóstwa swego.
4Mwanamke huyo alikuwa amevaa vazi la rangi ya zambarau na nyekundu; alikuwa amejipamba kwa dhahabu, mawe ya thamani na lulu. Mkononi mwake alishika kikombe cha dhahabu ambacho kilikuwa kimejaa machukizo na mambo machafu yanayoonyesha uzinzi wake.
5A na czole jej było imię napisane: Tajemnica, Babilon wielki, matka wszeteczeóstw i obrzydliwości ziemi.
5Alikuwa ameandikwa juu ya paji la uso wake jina la fumbo "Babuloni mkuu, mama wa wazinzi na wa mambo yote ya kuchukiza sana duniani."
6I widziałem niewiastę onę pijaną krwią świętych i krwią męczenników Jezusowych; a widząc ją, dziwowałem się wielkim podziwieniem.
6Nikamwona huyo mwanamke amelewa damu ya watu wa Mungu, na damu ya watu waliouawa kwa sababu ya kumtangaza Yesu. Nilipomwona nilishangaa mno.
7I rzekł mi Anioł: Czemuż się dziwujesz? Ja tobie powiem tajemnicę tej niewiasty i bestyi, która ją nosi, która ma siedm głów i dziesięć rogów.
7Lakini malaika akaniambia, "Kwa nini unashangaa? Mimi nitakuambia maana iliyofichika ya mwanamke huyu na mnyama huyo amchukuaye ambaye ana vichwa saba na pembe kumi.
8Bestyja, którąś widział, była, a nie jest, a ma wystąpić z przepaści, a iść na zginienie; i zadziwią się mieszkający na ziemi, (których imiona nie są napisane w księgach żywota od założenia świata), widząc bestyję, która była, a nie jest, a przecię jest.
8Huyo mnyama uliyemwona alikuwa hai hapo awali, lakini sasa amekufa. Hata hivyo, karibu sana atapanda kutoka shimoni kuzimu, lakini ataangamizwa. Wanaoishi duniani watashangaa; naam, watu wote ambao majina yao hayakupata kuandikwa katika kitabu cha uzima tangu mwanzo wa ulimwengu, watashangaa kumwona huyo mnyama ambaye hapo awali, aliishi, kisha akafa na sasa anatokea tena!
9Tuć jest rozum mający mądrość: Te siedm głów są siedm gór, na których ta niewiasta siedzi.
9"Hapa panahitaji akili na hekima! Hivyo vichwa saba ni vilima saba, na huyo mwanamke anaketi juu yake. Vichwa hivyo pia ni wafalme saba.
10A królów jest siedm, pięć ich upadło, a jeden jest, inszy jeszcze nie przyszedł, a gdy przyjdzie, na mały czas musi trwać.
10Kati ya hao wafalme saba, watano wamekwisha angamia, mmoja anatawala bado, na yule mwingine bado hajafika; na atakapofika atabaki kwa muda mfupi.
11A bestyja, która była a nie jest, toć jest ten ósmy, a jest z onych siedmiu, a idzie na zginienie.
11Huyo mnyama ambaye alikuwa anaishi hapo awali lakini sasa haishi tena ni mfalme wa nane, naye pia ni miongoni mwa hao saba, na anakwenda zake kuharibiwa.
12A dziesięć rogów, któreś widział, jest dziesięć królów, którzy królestwa jeszcze nie wzięli; ale wezmą moc jako królowie, na jednę godzinę z bestyją.
12"Zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme ambao bado hawajaanza kutawala. Lakini watapewa mamlaka ya kutawala kwa muda wa saa moja pamoja na yule mnyama.
13Ci jedną radę mają i moc, i zwierzchność swoję bestyi podadzą.
13Shabaha ya hawa kumi ni moja, na watampa yule mnyama nguvu na mamlaka yao yote.
14Ci z Barankiem walczyć będą, i Baranek ich zwycięży, bo jest Panem panów i królem królów, i którzy są z nim powołani i wybrani, i wierni.
14Watapigana na Mwanakondoo, lakini Mwanakondoo pamoja na wale aliowaita na kuwachagua, ambao ni waaminifu, atawashinda kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme."
15I rzekł mi: Wody, któreś widział, gdzie wszetecznica siedzi, są ludzie i zastępy, i narody, i języki.
15Malaika akaniambia pia, "Yale maji uliyoyaona pale alipokaa yule mzinzi, ni mataifa, watu wa kila rangi na lugha.
16A dziesięć rogów, któreś widział na bestyi, cić w nienawiści mieć będą wszetecznicę i uczynią ją spustoszoną i nagą, i ciało jej będą jeść, a samą ogniem spalą.
16Pembe zile kumi ulizoziona na yule mnyama watamchukia huyo mzinzi. Watachukua kila kitu alicho nacho na kumwacha uchi; watakula nyama yake na kumteketeza kwa moto.
17Albowiem Bóg podał do serc ich, aby czynili wolę jego, a czynili jednomyślnie, i dali królestwo swoje bestyi, ażby się wypełniły słowa Boże.
17Maana Mungu ametia mioyoni mwao nia ya kutekeleza shabaha yake, yaani kwa kukubaliana wao kwa wao na kumpa huyo mnyama mamlaka yao ya kutawala, mpaka hapo neno la Mungu litakapotimia.
18A niewiasta, którąś widział, jest miasto ono wielkie, które ma królestwo nad królami ziemi.
18"Na yule mwanamke uliyemwona ndio ule mji mkuu unaowatawala wafalme wa dunia."