1Proszę was tedy, bracia! przez litości Boże, abyście stawiali ciała wasze ofiarą żywą, świętą, przyjemną Bogu, to jest rozumną służbę waszę.
1Kwa hiyo, ndugu zangu, maadam Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: jitoleeni nafsi zenu kwa Mungu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.
2A nie przypodobywajcie się temu światu, ale się przemieócie przez odnowienie umysłu waszego na to, abyście doświadczyli, która jest wola Boża dobra, przyjemna i doskonała.
2Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu.
3Albowiem powiadam przez łaskę, która mi jest dana, każdemu, co jest między wami, aby więcej o sobie nie rozumiał, niżeli potrzeba rozumieć; ale żeby o sobie rozumiał skromnie, tak jako komu Bóg udzielił miarę wiary.
3Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni ninyi nyote: msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kufuatana na kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.
4Albowiem jako w jednem ciele wiele członków mamy, ale wszystkie członki nie jednoż dzieło mają:
4Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake.
5Tak wiele nas jest jednem ciałem w Chrystusie, aleśmy z osobna jedni drugich członkami.
5Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
6Mając tedy różne dary według łaski, która nam jest dana; jeźli proroctwo, niech będzie według sznuru wiary;
6Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake.
7Jeźli posługowanie, niech będzie w posługowaniu; jeźli kto naucza, niech trwa w nauczaniu;
7Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe.
8Jeźli kto napomina, w napominaniu; kto rozdaje, w szczerości; kto przełożony jest, w pilności; kto czyni miłosierdzie, niech czyni z ochotą.
8Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.
9Miłość niech będzie nieobłudna; miejcie w obrzydliwości złe; imając się dobrego.
9Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
10Miłością braterską jedni ku drugim skłonni bądźcie, uczciwością jedni drugich uprzedzając.
10Pendaneni kidugu; kila mmoja amfikirie mwenzake kwanza kwa heshima.
11W pracy nie leniwi, duchem pałający, Panu służący;
11Msilegee katika bidii, muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.
12W nadziei się weselący, w ucisku cierpliwi, w modlitwie ustawiczni;
12Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida na kusali daima.
13Potrzebom świętych udzielający, gościnności naśladujący.
13Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.
14Dobrorzeczcie tym, którzy was prześladują; dobrorzeczcie, a nie przeklinajcie.
14Watakieni baraka wote wanaowadhulumu ninyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani.
15Weselcie się z weselącymi, a płaczcie z płaczącymi.
15Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
16Bądźcie między sobą jednomyślni, wysoko o sobie nie rozumiejąc, ale się do niskich nakłaniając.
16Muwe na wema uleule kwa kila mtu. Msijitakie makuu, bali jishugulisheni na watu wadogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.
17(Bracia!) nie bądźcie mądrymi sami u siebie; żadnemu złem za złe nie oddawajcie, obmyśliwając to, co jest uczciwego przed wszystkimi ludźmi.
17Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.
18Jeźli można, ile z was jest, ze wszystkimi ludźmi pokój miejcie.
18Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.
19Nie mścijcie się sami, najmilsi: ale dajcie miejsce gniewowi; albowiem napisano: Mnie pomsta, a Ja oddam, mówi Pan.
19Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza asema Bwana."
20Jeźli tedy łaknie nieprzyjaciel twój, nakarm go; jeźli pragnie, napój go: bo to czyniąc, węgle rozpalone zgarniesz na głowę jego.
20Tena, Maandiko yasema: "Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake."
21Nie daj się zwyciężyć złemu, ale złe dobrem zwyciężaj.
21Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.