1Paweł, sługa Boży i Apostoł Jezusa Chrystusa według wiary wybranych Bożych i znajomości prawdy, która jest według pobożności,
1Mimi Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo naandika. Mimi nimechaguliwa kuijenga imani ya wateule wa Mungu na kuwaongoza waufahamu ukweli wa dini yetu,
2Ku nadziei żywota wiecznego, który obiecał przed czasy wiekuistemi ten, który nie kłamie, Bóg, a objawił czasów swoich,
2ambayo msingi wake ni tumaini la kupata uzima wa milele. Mungu ambaye hasemi uongo, alituahidia uzima huo kabla ya mwanzo wa nyakati,
3To słowo swoje przez kazanie, które mi jest zwierzone według rozrządzenia zbawiciela naszego Boga:
3na wakati ufaao ulipowadia, akaudhihirisha katika ujumbe wake. Mimi nilikabidhiwa ujumbe huo nuutangaze kufuatana na amri ya Mungu, Mwokozi wetu.
4Tytusowi, własnemu synowi według spólnej wiary, łaska, miłosierdzie i pokój niech będzie od Boga Ojca, i Pana Jezusa Chrystusa, zbawiciela naszego.
4Ninakuandikia wewe Tito, mwanangu wa kweli katika imani tunayoshiriki. Nakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba, na kutoka kwa Kristo Yesu, Mkombozi wetu.
5Dlategom cię zostawił w Krecie, abyś to, co tam jeszcze zostaje, w rząd dobry wprawił i postanowił po miastach starszych, jakom ci ja był rozkazał;
5Nilikuacha Krete ili urekebishe yale mambo ambayo hayakuwa yamekamilika bado, na kuwateua wazee wa kanisa katika kila mji. Kumbuka maagizo yangu:
6Jeźli kto jest bez nagany, mąż jednej żony, dzieci wierne mający, które by nie mogły być obwinione w zbytku, albo niepoddane rządowi.
6mzee wa kanisa anapaswa kuwa mtu asiye na hatia; aliye na mke mmoja tu, na watoto wake wanapaswa kuwa waumini, wasiojulikana kuwa wakorofi au wakaidi.
7Albowiem biskup ma być bez nagany, jako szafarz Boży, nie sam sobie się podobający, nie gniewliwy, nie pijanica wina, nie bitny, nie szukający zysku sprośnego;
7Maana kwa vile kiongozi wa kanisa ni mkurugenzi wa kazi ya Mungu, anapaswa kuwa mtu asiye na hatia. Asiwe mwenye majivuno, mwepesi wa hasira, mlevi, mkorofi au mchoyo.
8Ale gościnny, dobre miłujący, roztropny, sprawiedliwy, świętobliwy, powściągliwy,
8Anapaswa kuwa mkarimu na anayependa mambo mema. Anapaswa kuwa mtu mtaratibu, mwadilifu, mtakatifu na mwenye nidhamu.
9Trzymający się onej wiernej mowy, która jest według nauki, iżby też mógł napominać nauką zdrową i tych, którzy się sprzeciwiają, przekonywać;
9Ni lazima ashike kikamilifu ujumbe ule wa kuaminika kama unavyofundishwa. Ndivyo atakavyoweza kuwatia wengine moyo kwa mafundisho ya kweli na kuyafichua makosa ya wale wanaoyapinga mafundisho hayo.
10Albowiem jest wiele rządowi niepoddanych, próżnomównych i zwodzicieli myśli, a najwięcej tych, którzy są z obrzezki,
10Maana, wako watu wengi, hasa wale walioongoka kutoka dini ya Kiyahudi, ambao ni wakaidi, wanaowapotosha wengine kwa upumbavu wao.
11Którym trzeba usta zatkać; którzy całe domy podwracają, ucząc rzeczy niesłusznych dla zysku sprośnego.
11Lazima kukomesha maneno yao, kwani wanavuruga jumuiya nzima kwa kufundisha mambo ambayo hawapaswi kufundisha; wanafanya hivyo kwa nia mbaya ya kupata faida ya fedha.
12Powiedział niektóry z nich własny ich prorok: Kreteóczycy zawsze są kłamcami, złemi bestyjami, brzuchami leniwemi.
12Hata mmoja wa manabii wao, ambaye naye pia ni Mkrete, alisema: "Wakrete, husema uongo daima; ni kama wanyama wabaya, walafi na wavivu!"
13To świadectwo jest prawdziwe; dla której przyczyny ostro ich karz, aby zdrowi byli w wierze.
13Naye alitoboa ukweli kwa sababu hiyo, unapaswa kuwakaripia vikali, ili wawe na imani kamilifu.
14Nie pilnując żydowskich baśni i przykazaó ludzi tych, którzy się odwracają od prawdy.
14Wasiendelee kushikilia hadithi tupu za Kiyahudi na maagizo ya kibinadamu yanayozuka kwa watu walioukataa ukweli.
15Wszystkoć czyste czystym, lecz pokalanym i niewiernym nie masz nic czystego, ale pokalany jest i umysł, i sumienie ich.
15Kila kitu ni safi kwa watu walio safi; lakini hakuna chochote kilicho safi kwa wale waliochafuliwa na wasioamini, maana dhamiri na akili zao zimechafuliwa.
16Udawają, że Boga znają; ale uczynkami swemi tego się zapierają, będąc obrzydłymi i nieposłusznymi, a do wszelkiego dobrego uczynku niesposobnymi.
16Watu kama hao hujidai kwamba wanamjua Mungu, lakini kwa matendo yao humkana. Ni watu wa kuchukiza mno na wakaidi, hawafai kwa jambo lolote jema.