1Num desses dias, quando Jesus ensinava o povo no templo, e anunciava o evangelho, sobrevieram os principais sacerdotes e os escribas, com os anciãos.
1Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2e falaram-lhe deste modo: Dize-nos, com que autoridade fazes tu estas coisas? Ou, quem é o que te deu esta autoridade?
2wakasema, "Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?"
3Respondeu-lhes ele: Eu também vos farei uma pergunta; dizei-me, pois:
3Yesu akawaambia, "Na mimi nitawaulizeni swali:
4O batismo de João era do céu ou dos homens?
4mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?"
5Ao que eles arrazoavam entre si: Se dissermos: do céu, ele dirá: Por que não crestes?
5Lakini wao wakajadiliana hivi: "Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6Mas, se dissermos: Dos homens, todo o povo nos apedrejará; pois está convencido de que João era profeta.
6Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii."
7Responderam, pois, que não sabiam donde era.
7Basi, wakamwambia, "Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi."
8Replicou-lhes Jesus: Nem eu vos digo com que autoridade faço estas coisas.
8Yesu akawaambia, "Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani."
9Começou então a dizer ao povo esta parábola: Um homem plantou uma vinha, arrendou-a a uns lavradores, e ausentou-se do país por muito tempo.
9Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: "Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10No tempo próprio mandou um servo aos lavradores, para que lhe dessem dos frutos da vinha; mas os lavradores, espancando-o, mandaram-no embora de mãos vazias.
10Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11Tornou a mandar outro servo; mas eles espancaram também a este e, afrontando-o, mandaram-no embora de mãos vazias.
11Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12E mandou ainda um terceiro; mas feriram também a este e lançaram-no fora.
12Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13Disse então o senhor da vinha: Que farei? Mandarei o meu filho amado; a ele talvez respeitarão.
13Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14Mas quando os lavradores o viram, arrazoaram entre si, dizendo: Este é o herdeiro; matemo-lo, para que a herança seja nossa.
14Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15E lançando-o fora da vinha, o mataram. Que lhes fará, pois, o senhor da vinha?
15Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua." Yesu akauliza, "Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16Virá e destruirá esses lavradores, e dará a vinha a outros. Ouvindo eles isso, disseram: Tal não aconteça!
16Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu." Watu waliposikia maneno hayo, walisema: "Hasha! Yasitukie hata kidogo!"
17Mas Jesus, olhando para eles, disse: Pois, que quer dizer isto que está escrito: A pedra que os edificadores rejeitaram, essa foi posta como pedra angular?
17Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, "Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18Todo o que cair sobre esta pedra será despedaçado; mas aquele sobre quem ela cair será reduzido a pó.
18Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa."
19Ainda na mesma hora os escribas e os principais sacerdotes, percebendo que contra eles proferira essa parábola, procuraram deitar-lhe as mãos, mas temeram o povo.
19Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20E, aguardando oportunidade, mandaram espias, os quais se fingiam justos, para o apanharem em alguma palavra, e o entregarem � jurisdição e � autoridade do governador.
20Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21Estes, pois, o interrogaram, dizendo: Mestre, sabemos que falas e ensinas retamente, e que não consideras a aparência da pessoa, mas ensinas segundo a verdade o caminho de Deus;
21Hao wapelelezi wakamwambia, "Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22é-nos lícito dar tributo a César, ou não?
22Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!"
23Mas Jesus, percebendo a astúcia deles, disse-lhes:
23Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24Mostrai-me um denário. De quem é a imagem e a inscrição que ele tem? Responderam: De César.
24"Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?"
25Disse-lhes então: Dai, pois, a César o que é de César, e a Deus o que é de Deus.
25Nao wakamjibu, "Ni vya Kaisari." Yesu akawaambia, "Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu."
26E não puderam apanhá-lo em palavra alguma diante do povo; e admirados da sua resposta, calaram-se.
26Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27Chegaram então alguns dos saduceus, que dizem não haver ressurreição, e perguntaram-lhe:
27Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28Mestre, Moisés nos deixou escrito que se morrer alguém, tendo mulher mas não tendo filhos, o irmão dele case com a viúva, e suscite descendência ao irmão.
28"Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29Havia, pois, sete irmãos. O primeiro casou-se e morreu sem filhos;
29Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30então o segundo, e depois o terceiro, casaram com a viúva;
30Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31e assim todos os sete, e morreram, sem deixar filhos.
31na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba--wote walikufa bila kuacha watoto.
32Depois morreu também a mulher.
32Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33Portanto, na ressurreição, de qual deles será ela esposa, pois os sete por esposa a tiveram?
33Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba."
34Respondeu-lhes Jesus: Os filhos deste mundo casaram-se e dão-se em casamento;
34Yesu akawaambia, "Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa;
35mas os que são julgados dignos de alcançar o mundo vindouro, e a ressurreição dentre os mortos, nem se casam nem se dão em casamento;
35lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa.
36porque já não podem mais morrer; pois são iguais aos anjos, e são filhos de Deus, sendo filhos da ressurreição.
36Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37Mas que os mortos hão de ressurgir, o próprio Moisés o mostrou, na passagem a respeito da sarça, quando chama ao Senhor; Deus de Abraão, e Deus de Isaque, e Deus de Jacó.
37Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38Ora, ele não é Deus de mortos, mas de vivos; porque para ele todos vivem.
38Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye."
39Responderam alguns dos escribas: Mestre, disseste bem.
39Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, "Mwalimu, umejibu vema kabisa."
40Não ousavam, pois, perguntar-lhe mais coisa alguma.
40Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41Jesus, porém, lhes perguntou: Como dizem que o Cristo é filho de Davi?
41Yesu akawauliza, "Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42Pois o próprio Davi diz no livro dos Salmos: Disse o Senhor ao meu Senhor: Assenta-te � minha direita,
42Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43até que eu ponha os teus inimigos por escabelo dos teus pés.
43mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44Logo Davi lhe chama Senhor como, pois, é ele seu filho?
44Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?"
45Enquanto todo o povo o ouvia, disse Jesus aos seus discípulos:
45Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46Guardai-vos dos escribas, que querem andar com vestes compridas, e gostam das saudações nas praças, dos primeiros assentos nas sinagogas, e dos primeiros lugares nos banquetes;
46"Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47que devoram as casas das viúvas, fazendo, por pretexto, longas orações; estes hão de receber maior condenação.
47Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!"