1Naquele tempo Herodes, o tetrarca, ouviu a fama de Jesus,
1Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu.
2e disse aos seus cortesãos: Este é João, o Batista; ele ressuscitou dentre os mortos, e por isso estes poderes milagrosos operam nele.
2Basi, akawaambia watumishi wake, "Mtu huyu ni Yohane mbatizaji, amefufuka kutoka wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake."
3Pois Herodes havia prendido a João, e, maniatando-o, o guardara no cárcere, por causa de Herodias, mulher de seu irmão Felipe;
3Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Sababu hasa ni
4porque João lhe dizia: Não te é lícito possuí-la.
4kwamba alikuwa amemwambia Herode, "Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!"
5E queria matá-lo, mas temia o povo; porque o tinham como profeta.
5Herode alitaka kumwua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.
6Festejando-se, porém, o dia natalício de Herodes, a filha de Herodias dançou no meio dos convivas, e agradou a Herodes,
6Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa,
7pelo que este prometeu com juramento dar-lhe tudo o que pedisse.
7hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba.
8E instigada por sua mãe, disse ela: Dá-me aqui num prato a cabeça de João, o Batista.
8Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, "Nipe papahapa katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji."
9Entristeceu-se, então, o rei; mas, por causa do juramento, e dos que estavam � mesa com ele, ordenou que se lhe desse,
9Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe.
10e mandou degolar a João no cárcere;
10Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane.
11e a cabeça foi trazida num prato, e dada � jovem, e ela a levou para a sua mãe.
11Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake.
12Então vieram os seus discípulos, levaram o corpo e o sepultaram; e foram anunciá-lo a Jesus.
12Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.
13Jesus, ouvindo isto, retirou-se dali num barco, para um, lugar deserto, � parte; e quando as multidões o souberam, seguiram-no a pé desde as cidades.
13Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini.
14E ele, ao desembarcar, viu uma grande multidão; e, compadecendo-se dela, curou os seus enfermos.
14Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.
15Chegada a tarde, aproximaram-se dele os discípulos, dizendo: O lugar é deserto, e a hora é já passada; despede as multidões, para que vão �s aldeias, e comprem o que comer.
15Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, "Mahali hapa ni nyikani, na saa zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula."
16Jesus, porém, lhes disse: Não precisam ir embora; dai-lhes vós de comer.
16Yesu akawaambia, "Si lazima waende, wapeni ninyi chakula."
17Então eles lhe disseram: Não temos aqui senão cinco pães e dois peixes.
17Lakini wao wakamwambia, "Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili."
18E ele disse: trazei-mos aqui.
18Yesu akawaambia, "Nileteeni hapa."
19Tendo mandado �s multidões que se reclinassem sobre a relva, tomou os cinco pães e os dois peixes e, erguendo os olhos ao céu, os abençoou; e partindo os pães, deu-os aos discípulos, e os discípulos �s multidões.
19Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.
20Todos comeram e se fartaram; e dos pedaços que sobejaram levantaram doze cestos cheios.
20Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.
21Ora, os que comeram foram cerca de cinco mil homens, além de mulheres e crianças.
21Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.
22Logo em seguida obrigou os seus discípulos a entrar no barco, e passar adiante dele para o outro lado, enquanto ele despedia as multidões.
22Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ng'ambo ya ziwa wakati yeye anawaaga watu.
23Tendo-as despedido, subiu ao monte para orar � parte. Ao anoitecer, estava ali sozinho.
23Baada ya kuwaaga, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake,
24Entrementes, o barco já estava a muitos estádios da terra, açoitado pelas ondas; porque o vento era contrário.
24na wakati huo ile mashua ilikwishafika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikuwa inakwenda mrama kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga.
25Â quarta vigília da noite, foi Jesus ter com eles, andando sobre o mar.
25Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji.
26Os discípulos, porém, ao vê-lo andando sobre o mar, assustaram-se e disseram: É um fantasma. E gritaram de medo.
26Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliingiwa na hofu, wakasema, "Ni mzimu!" Wakapiga kelele kwa hofu.
27Jesus, porém, imediatamente lhes falou, dizendo: Tende ânimo; sou eu; não temais.
27Mara, Yesu akasema nao, "Tulieni, ni mimi. Msiogope!"
28Respondeu-lhe Pedro: Senhor! se és tu, manda-me ir ter contigo sobre as águas.
28Petro akamwambia, "Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako."
29Disse-lhe ele: Vem. Pedro, descendo do barco, e andando sobre as águas, foi ao encontro de Jesus.
29Yesu akasema, "Haya, njoo." Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu.
30Mas, sentindo o vento, teve medo; e, começando a submergir, clamou: Senhor, salva-me.
30Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, "Bwana, niokoe!"
31Imediatamente estendeu Jesus a mão, segurou-o, e disse-lhe: Homem de pouca fé, por que duvidaste?
31Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, "Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?"
32E logo que subiram para o barco, o vento cessou.
32Basi, wakapanda mashuani, na upepo ukatulia.
33Então os que estavam no barco adoraram-no, dizendo: Verdadeiramente tu és Filho de Deus.
33Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, "Hakika wewe ni Mwana wa Mungu."
34Ora, terminada a travessia, chegaram � terra em Genezaré.
34Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti.
35Quando os homens daquele lugar o reconheceram, mandaram por toda aquela circunvizinhança, e trouxeram-lhe todos os enfermos;
35Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote,
36e rogaram-lhe que apenas os deixasse tocar a orla do seu manto; e todos os que a tocaram ficaram curados.
36wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake; wote waliomgusa walipona.