1Rogo-vos pois, irmãos, pela compaixão de Deus, que apresenteis os vossos corpos como um sacrifício vivo, santo e agradável a Deus, que é o vosso culto racional.
1Kwa hiyo, ndugu zangu, maadam Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: jitoleeni nafsi zenu kwa Mungu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.
2E não vos conformeis a este mundo, mas transformai-vos pela renovação da vossa mente, para que experimenteis qual seja a boa, agradável, e perfeita vontade de Deus.
2Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu.
3Porque pela graça que me foi dada, digo a cada um dentre vós que não tenha de si mesmo mais alto conceito do que convém; mas que pense de si sobriamente, conforme a medida da fé que Deus, repartiu a cada um.
3Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni ninyi nyote: msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kufuatana na kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.
4Pois assim como em um corpo temos muitos membros, e nem todos os membros têm a mesma função,
4Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake.
5assim nós, embora muitos, somos um só corpo em Cristo, e individualmente uns dos outros.
5Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
6De modo que, tendo diferentes dons segundo a graça que nos foi dada, se é profecia, seja ela segundo a medida da fé;
6Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake.
7se é ministério, seja em ministrar; se é ensinar, haja dedicação ao ensino;
7Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe.
8ou que exorta, use esse dom em exortar; o que reparte, faça-o com liberalidade; o que preside, com zelo; o que usa de misericórdia, com alegria.
8Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.
9O amor seja não fingido. Aborrecei o mal e apegai-vos ao bem.
9Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
10Amai-vos cordialmente uns aos outros com amor fraternal, preferindo-vos em honra uns aos outros;
10Pendaneni kidugu; kila mmoja amfikirie mwenzake kwanza kwa heshima.
11não sejais vagarosos no cuidado; sede fervorosos no espírito, servindo ao Senhor;
11Msilegee katika bidii, muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.
12alegrai-vos na esperança, sede pacientes na tribulação, perseverai na oração;
12Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida na kusali daima.
13acudi aos santos nas suas necessidades, exercei a hospitalidade;
13Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.
14abençoai aos que vos perseguem; abençoai, e não amaldiçoeis;
14Watakieni baraka wote wanaowadhulumu ninyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani.
15alegrai-vos com os que se alegram; chorai com os que choram;
15Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
16sede unânimes entre vós; não ambicioneis coisas altivas mas acomodai-vos �s humildes; não sejais sábios aos vossos olhos;
16Muwe na wema uleule kwa kila mtu. Msijitakie makuu, bali jishugulisheni na watu wadogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.
17a ninguém torneis mal por mal; procurai as coisas dignas, perante todos os homens.
17Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.
18Se for possível, quanto depender de vós, tende paz com todos os homens.
18Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.
19Não vos vingueis a vós mesmos, amados, mas dai lugar � ira de Deus, porque está escrito: Minha é a vingança, eu retribuirei, diz o Senhor.
19Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza asema Bwana."
20Antes, se o teu inimigo tiver fome, dá-lhe de comer; se tiver sede, dá-lhe de beber; porque, fazendo isto amontoarás brasas de fogo sobre a sua cabeça.
20Tena, Maandiko yasema: "Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake."
21Não te deixes vencer do mal, mas vence o mal com o bem.
21Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.