Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Acts

19

1Zhi kai o Apollos sas ande Corinth, o Pavlo kana nakhlo anda sa le gava kai si ande Asia, areslo ando Ephesus, ai kotse arakhlia uni disiplon.
1Wakati Apolo alipokuwa Korintho, Paulo alisafiri sehemu za bara, akafika Efeso ambako aliwakuta wanafunzi kadhaa.
2Ai phendia lenge, "Lian anda tumende O Swunto Duxo kana pachan tume?" Won phende leske, "Ame chi ashundiam ke si ek Swunto Duxo."
2Akauliza, "Je, mlipopata kuwa waumini mlipokea Roho Mtakatifu?" Nao wakamjibu, "La! Hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatujasikia."
3Ai phendia lenge, "Anda savo bolimos tume sanas bolde?" Ai won phende leske, "Ando bolimos le Iovanosko."
3Naye akasema, "Sasa mlipata ubatizo wa namna gani?" Wakamjibu, "Ubatizo wa Yohane."
4Antunchi o Pavlo phendia, "O Iovano boldia kodolen kai mangenas te parhuven pengo traio, ai motholas le Zhidovonge te pachanpe ande kodo kai avela pala leste, kodo si O Kristo.
4Naye Paulo akasema, "Ubatizo wa Yohane ulikuwa wa kuonyesha kwamba watu wametubu. Yohane aliwaambia watu wamwamini yule ambaye alikuwa anakuja baada yake, yaani Yesu."
5Pe kodola vorbi, bolde sas ando anav le Devlesko O Jesus.
5Baada ya kusikia hayo, walibatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
6Kana o Pavlo thodia le vas pe lende, O Swunto Duxo avilo pe lende, ai denas duma andal kolaver shiba, ai mothonas so si te avel.
6Basi, Paulo akawawekea mikono, na Roho Mtakatifu akawashukia, wakaanza kusema lugha mbalimbali na kutangaza ujumbe wa Mungu.
7Won sas sa andek than desh u dui manush.
7Wote jumla, walikuwa watu wapatao kumi na wawili.
8Porme o Pavlo gelo ande synagogue, ai kotse dia duma bi darako trin shon, ai delas duma pal dieli le rhaioske kai si le Devlesko.
8Kwa muda wa miezi mitatu Paulo alikuwa akienda katika sunagogi, akawa na majadiliano ya kuvutia sana juu ya Ufalme wa Mungu.
9Numa uni lengo ilo zuralo sas, ai chi pachanaspe, ai mothonas chorhe dieli pa drom le Devlesko angla narodo. Antunchi o Pavlo gelotar lendar, ai lia le manushen kai pachanaspe ando Del pesa; ai sicharelas len pa Del swako dies andek shkola ieke manusheske kai busholas Tirannas.
9Lakini wengine walikuwa wakaidi, wakakataa kuamini, wakaanza kuongea vibaya hadharani juu ya Njia ya Bwana. Hapo Paulo alivunja uhusiano nao, akawachukua pembeni wale wanafunzi wake, akawa anazungumza nao kila siku katika jumba la masomo la Turano.
10Kodia buchi gelia dui bersh, ai sa kodola kai beshenas ande Asia, Zhiduvuria ai Grekuria ashunde E Vorba le Devleski.
10Aliendelea kufanya hivyo kwa muda wa miaka miwili hata wakazi wote wa Asia, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, wakaweza kusikia neno la Bwana.
11Ai O Del kerelas bare mirakluria le Pavlosa.
11Mungu alifanya miujiza ya ajabu kwa mikono ya Paulo.
12Kadia kai thonas pe naswale gada vai dikhlorhe kai azbade sas le Pavlos, ai le naswale sastionas, ai le manush kai sas o beng lende zhalastar.
12Watu walikuwa wakichukua leso na nguo nyingine za kazi ambazo Paulo alikuwa amezitumia, wakazipeleka kwa wagonjwa, nao wakaponywa magonjwa yao; na wale waliokuwa na pepo wabaya wakatokwa na pepo hao.
13Sas uni Zhiduvuria kai zhanas andek than ando foro forestar te gonin le bengen andal naswale, zumavenas ando anav le Devlesko Jesus te keren le te anklen avri, phende le bengenge, "Dav tume ordina ando anav le Jesusosko, anklen avri, kado Jesus kai o Pavlo mothol pe leste."
13Wayahudi kadhaa wenye kupunga pepo wabaya, walisafiri huko na huko, wakijaribu kulitumia jina la Bwana Yesu kwa wale waliokuwa wamepagawa na pepo wabaya. Walikuwa wakisema: "Ninawaamuru kwa jina la Yesu ambaye Paulo anamhubiri."
14Ieke bare rasha kai sas Zhidovo, busholas Sceva, sas les efta shave, kodola shave kerenas kadia.
14Watoto saba wa Skewa, Kuhani Mkuu wa Kiyahudi, walikuwa miongoni mwa hao waliokuwa wanafanya hivyo.
15Numa o beng mothol lenge, "Zhanav kon si O Jesus, ai zhanav kon si o Pavlo, numa tume kon san?"
15Lakini pepo mbaya aliwajibu, "Ninamfahamu Yesu, ninamjua pia Paulo, lakini ninyi ni nani?"
16Ai kado manush kai sas o beng ande leste xoko pe lende, ai sas les putiera pe lende, ai mardia le. Kadia de zurales kai nashle anda kodo kher sa nange ai dukhade.
16Kisha yule mtu aliyepagawa aliwarukia wote kwa kishindo, akawashinda nguvu. Na hao watoto wa Skewa wakakimbia kutoka ile nyumba wakiwa uchi na wamejaa majeraha.
17Kodola diela zhanenas sa le Zhiduvuria sa le Grekuria kai beshenas ando Ephesus, ai daraile savorhe, ai o anav le Devlesko Jesus sas bariardia.
17Kila mtu huko Efeso, Myahudi na asiye Myahudi, alisikia juu ya tukio hilo. Wote waliingiwa na hofu, wakalitukuza jina la Bwana Yesu.
18But shave le Devleske avenas te mothonas angla narodo so kerde.
18Waumini wengi walijitokeza wakakiri hadharani mambo waliyokuwa wametenda.
19But anda kodola kai kerenas drabarimos, andine penge klishki, ai phabarenas le angla sa o narodo. Ai line sama le love kai monas kadala klishki, ai arakhle ke sas pe panvardesh mi teliara rupune.
19Wengine waliokuwa wameshughulikia mambo ya uchawi hapo awali, walikusanya vitabu vyao, wakavichoma mbele ya wote. Walikisia gharama ya vitabu hivyo, wakaona yafikia vipande vya fedha elfu hamsini.
20Ai E Vorba le Devleski zhalas katar godi ande putiera ai ande zor.
20Kwa namna hiyo, neno la Bwana lilizidi kuenea na kuwa na nguvu zaidi.
21Akana kai kodola dieli nakhle, o Pavlo manglia te zhal ande Jerusalem. Ai manglia te nakhel pai Macedonia ai pai Greece, "Ai kana avava kotse," phendia, "Trobul te dikhav Rome."
21Baada ya mambo hayo, Paulo aliamua kwenda Yerusalemu kwa kupitia Makedonia na Akaya. Alisema, "Baada ya kufika huko, itanilazimu kuona Roma pia."
22Tradia antunchi ande Macedonia dui anda peske zhutitoria, o Timote ai o Erastus; ai wo mai beshlo xantsi vriama ande Asia.
22Hivyo, aliwatuma wawili wa wasaidizi wake, Timotheo na Erasto, wamtangulie kwenda Makedonia, naye akabaki kwa muda huko Asia.
23Ande kodia vriama kerdilia but bunto pala zakono le Devlesko.
23Wakati huo ndipo kulipotokea ghasia kubwa huko Efeso kwa sababu ya hiyo Njia ya Bwana.
24Iek manush kai sas zhintari, wo busholas Demetrius, wo kerelas ikoni rupeske pala Diana, ai le manush kai kerenas leski buchi nirinas but love.
24Kulikuwa na mfua fedha mmoja aitwaye Demetrio, ambaye alikuwa na kazi ya kutengeneza sanamu za nyumba ya mungu wa kike aitwaye Artemi. Shughuli hiyo iliwapatia mafundi faida kubwa.
25Ai chidia sa kodolen kai kerenas kodalatar buchi, ai phendia lenge, "Manushale, te sam barvale, barvale sam pala e buchi kai si ame.
25Demetrio aliwakusanya hao wafanyakazi pamoja na wengine waliokuwa na kazi kama hiyo, akawaambia, "Wananchi, mnafahamu kwamba kipato chetu kinatokana na biashara hii.
26Ai dikhen ai ashunen, ke na ferdi ando Ephesus, numa pashte ande sa Asia, kado kai bushol Pavlo phendia le manushenge ai sikadia lenge ke le dela kai si kerde andal vas le manushenge nai dela.
26Sasa, mnaweza kusikia na kujionea wenyewe mambo Paulo anayofanya, si tu hapa Efeso, ila pia kote katika Asia. Yeye amewashawishi na kuwageuza watu wakakubali kwamba miungu ile iliyotengenezwa na watu si miungu hata kidogo.
27Kadia diela chi rimol ferdi amari buchi, numa vi e bari del Diana te xasarel sa pesko barimos ande tampla, ai antunchi chi mai avela la lako barimos, ai kadia ikona kai rhuginpe late o narodo kai si ande Asia ai sa le lumia!"
27Hivyo iko hatari kwamba biashara yetu itakuwa na jina baya. Si hivyo tu, bali pia jambo hilo linaweza kuifanya nyumba ya mungu Artemi kuwa si kitu cha maana. Hatimaye sifa zake huyo ambaye Asia na dunia yote inamwabudu, zitakwisha."
28Kana ashunde kodola vorbi, savorhe xolaile, ai tsipinas. Phenenas, "Bari si e ikona Diana le Ephesusonge."
28Waliposikia hayo, waliwaka hasira, wakaanza kupiga kelele: "Mkuu ni Artemi, wa Efeso!"
29Sa o foro buntisailosas, ai line pesa o Gaius ai o Aristarchus, dui andal Macedonia, kai sas le vortacha le Pauloske kai zhanas lesa, ai gele savorhe andek bari soba.
29Mji wote ukajaa ghasia. Wakawavamia Gayo na Aristarko, wenyeji wa Makedonia, ambao walikuwa wasafiri wenzake Paulo, wakakimbia nao mpaka kwenye ukumbi wa michezo.
30O Pavlo mangelas vi wo te zhal angla narodo, numa le shave le Devleske chi mekenas les.
30Paulo mwenyewe alitaka kuukabili huo umati wa watu, lakini wale waumini walimzuia.
31Uni andel bare kai poronchinas pe uni gava ande Asia, kai sas leske vortacha, trade leske lil te mangenpe lestar te na zhal ande kodo kher.
31Maofisa wengine wa huo mkoa wa Asia, waliokuwa rafiki zake, walimtumia Paulo ujumbe wakimsihi asijihatarishe kwa kwenda kwenye ukumbi wa michezo.
32Uni mothonas kadia, uni aver fialo ke buntuimos kerdiliasas; ai but anda narodo chi zhanenas sostar chidinisaile sas andek than.
32Wakati huo, kila mtu alikuwa anapayuka; wengine hili na wengine lile, mpaka hata ule mkutano ukavurugika. Wengi hawakujua hata sababu ya kukutana kwao.
33Uni manush anda narodo line o Alexander ai thode les angla narodo. O Alexander antunchi kerdia iek semno anda vas ai manglia te del duma te chacharel le angla narodo.
33Kwa vile Wayahudi walimfanya Aleksanda ajitokeze mbele, baadhi ya watu katika ule umati walidhani kuwa ndiye. Basi, Aleksanda aliwaashiria watu kwa mkono akitaka kujitetea mbele ya ule umati wa watu.
34Numa kana haliarde ke Zhidovo sas, tsipisarde savorhe andek than sa kodola vorbi pashte dui chasuria, "Bari si e ikona Diana le Ephesusonge".
34Lakini walipotambua kuwa yeye ni Myahudi, wote kwa sauti moja walipiga kelele: "Mkuu ni Artemi wa Efeso!" Wakaendelea kupayukapayuka hivyo kwa muda wa saa mbili.
35Ai kana o baro manush le forosko ashadia le narodos te na mai buntuilpe, phendia, "Ephesusanuria, sa e lumia zhanel ke o foro kai si ando Ephesus, lel sama katar o tampla kai si e ikona Diana ai lako patreto kai hulisto anda cheri (Jupiter).
35Hatimaye karani wa mji alifaulu kuwanyamazisha, akawaambia, "Wananchi wa Efeso, kila mtu anajua kwamba mji huu wa Efeso ni mlinzi wa nyumba ya mungu Artemi na mlinzi wa ile sanamu iliyoanguka kutoka mbinguni.
36Khonik nashti mothol ke chi zhanel, anda kodia trobul te na mai buntuin tume, ai te na keren kanch mai anglal sar te gindin tume.
36Hakuna anayeweza kukana mambo haya. Hivyo basi, tulieni; msifanye chochote bila hadhari.
37Tume andian kadale manushen katse, won chi chorde andal tampluria, ai chi marde mui katar amari ikona.
37Mmewaita watu hawa hapa ingawaje hawakuikufuru nyumba ya mungu wala kumtukana mungu wetu wa kike.
38Te si o Demetrius, ai leske manush te thonpe vari kashte dosh, si diesa krisake, ai si zhandari, ai kotse trobul te zhan te mothon pe kaste thon dosh.
38Kama, basi Demetrio na wafanyakazi wake wana mashtaka yao kuhusu watu hawa, yapo mahakama na wakuu wa mikoa; wanaweza kushtakiana huko.
39Ai te mai si tumen vari so kai miazol tumenge ke nai mishto, lasharasa kodia diela ande kris.
39Kama mna matatizo mengine, yapelekeni katika kikao halali.
40Ke sai dosharen ame ke buntuisailiam anda so kerdilia adies. Ke kanchi nai ame te sikavas ke vorta keras kai chidinisailiam.
40Kwa maana tungaliweza kushtakiwa kwa kusababisha ghasia kutokana na vituko vya leo. Ghasia hii haina msingi halali na hatungeweza kutoa sababu za kuridhisha za ghasia hiyo."
41Kana getosardia pesko divano, phendia le narodoske te zhantar khere.
41Baada ya kusema hayo aliuvunja mkutano.