1Kana mekliam le, geliamtar po paraxodo ai geliam strazo ando Cos; ai pe terharin aresliam kai izula Rhodes, ai kotsar geliamtar ando Patara.
1Tulipokwisha agana nao, tulipanda meli tukaenda moja kwa moja mpaka Kosi. Kesho yake tulifika Rodo, na kutoka huko tulikwenda Patara.
2Ai arakhliam iek paraxodo kai nakhelas pai Phoenicia, liam les, ai geliamtar.
2Huko, tulikuta meli iliyokuwa inakwenda Foinike, hivyo tulipanda, tukasafiri.
3Kana dikhliam e izula Cyprus, chi aterdiliam, mekliam la pe stingo, ai geliam mai angle karing e Syria, ai aterdiliam ande Tyre: Ke o paraxodo trobulas te huliarel tele o tovorho kai sas les.
3Baada ya kufika mahali ambapo tuliweza kuona Kupro, tulipitia upande wake wa kusini tukaelekea Siria. Tulitia nanga katika mji wa Tiro ambapo ile meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
4Ai kotse arakhliam manush kai pachanaspe ando Del, beshliam lensa iek kurko. Ai O Swunto Duxo phendia kodola phral te mothon le Pavloske te na zhal ando Jerusalem.
4Tulikuta waumini huko, tukakaa pamoja nao kwa muda wa juma moja. Waumini hao wakawa waongea kwa nguvu ya Roho, wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu.
5Ai kana nakhlo kurko, mangliamas te zhastar mai angle. Ai savorhe avile amensa, zhi avri anda foro penge rhomniansa penge shavensa. Thodiam ame anda changende pe chishai pasha pai te rhugisavas.
5Lakini muda wetu ulipokwisha tuliondoka. Wote pamoja na wanawake na watoto wao walitusindikiza mpaka nje ya mji. Tulipofika pwani, sote tulipiga magoti tukasali.
6Porme kana liam amenge dies lasho iek kavrestar, anklistiam po paraxodo, ai won geletar khere.
6Kisha tuliagana; sisi tukapanda meli nao wakarudi makwao.
7Kana getosardiam te zhas po paraxodo, geliam anda Tyre ando Ptolemais,ai kotse geliam te dikhas le shave le Devleske, amare phral, ai beshliam lensa iek dies.
7Sisi tuliendelea na safari yetu kutoka Tiro tukafika Tolemai ambapo tuliwasalimu ndugu zetu, tukakaa nao siku moja.
8Pe terharin geliamtar, ai aresliam ando Caesarea. Kana aviliam ando kher le Filiposko, wo sas manush kai divinilas pa Del, iek andal efta manush kai alosardiamas ando Jerusalem, beshliam leste.
8Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisarea. Huko Kaisarea tulikwenda nyumbani kwa mhubiri Filipo. Yeye alikuwa mmoja wa wale saba waliochaguliwa kule Yerusalemu.
9Sas les shtar sheia, kai nas ansurime. Won denas duma pa E Vorba le Devleski.
9Alikuwa na binti watatu ambao walikuwa na kipaji cha unabii.
10Beshliam kotse neskolki dies, iek profeto kai busholas Agabus avilo andai Judea.
10Baada ya kukaa huko siku kadhaa, nabii mmoja aitwaye Agabo alifika kutoka Yudea.
11Ai avilo te dikhel ame, ai lia e prashtia le Pavloski, ai phanglia peske punrhe ai peske vas, ai phendia, "Eta, so phendia O Swunto Duxo, kodo manush kai si leski kadia prashtia le Zhiduvuria phandenas les sakadia ando Jerusalem, ai dena les ka le Nai Zhiduvuria."
11Alitujia, akachukua mkanda wa Paulo, akajifunga mikono na miguu, akasema "Roho Mtakatifu asema hivi: Wayahudi kule Yerusalemu watamfunga namna hii mtu mwenye ukanda na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa."
12Kana ashundiam kodia, ame ai kodola kai samas lende ando kher, mangliam ame katar o Pavlo te na zhal ande Jerusalem.
12Tuliposikia hayo, sisi na wale watu wengine waliokuwa hapo tulimsihi Paulo asiende Yerusalemu.
13O Pavlo phendia, "So keren, kai roven ai dukhaven murho ilo? Vi mekava te phanden ma, ai vi te mudaren ma ando Jerusalem pala o anav le Devlesko, Jesus Kristo."
13Lakini yeye alijibu, "Mnataka kufanya nini? Mnataka kuvunja moyo wangu kwa machozi? Niko tayari siyo tu kutiwa ndani kule Yerusalemu, ila hata kufa kwa ajili ya Bwana Yesu."
14O Pavlo chi mekelaspe pala lende, ai won chi mai phende leske kanch, phenenas, "E voia le Devleski te kerdiol."
14Tuliposhindwa kumshawishi tulinyamaza, tukasema tu: "Mapenzi ya Bwana yafanyike"
15Xantsi dies pala kodia lashardiliam, ai geliamtar ando Jerusalem.
15Baada ya kukaa pale kwa muda, tulifunga mizigo yetu, tukaendelea na safari kwenda Yerusalemu.
16Uni andal shave le Devleske anda Caesarea avile amensa, ai angerdia lensa iek manush kai busholas Mnason andai Cyprus, wo diasas pe ka Del de dumult ai leste trobulas te beshas.
16Wengine kati ya wale wafuasi wa Kaisarea walienda pamoja nasi, wakatupeleka nyumbani kwa Mnasoni ambaye tulikuwa tunakwenda kukaa naye kwa muda. Mnasoni alikuwa mwenyeji wa Kupro na alikuwa amekuwa muumini kwa siku nyingi.
17Kana aresliam ande Jerusalem, le shave le Devleske kai sas kotse raduime sas kana dikhle ame.
17Tulipofika Yerusalemu, ndugu waumini walitupokea vizuri sana.
18Pe terharin o Pavlo gelo amensa ka iek phral kai busholas Iakov, ai sa le mai phure chidepe kotse.
18Kesho yake Paulo alikwenda pamoja nasi kumwamkia Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwako pia.
19Kana dia o vas savorhensa, o Pavlo phendia lenge so godi O Del kerdia mashkar le Nai Zhiduvuria, la buchasa kai dia les O Del.
19Baada ya kuwasalimu, Paulo aliwapa taarifa kamili kuhusu yote Mungu aliyokuwa ametenda kati ya mataifa kwa njia ya utumishi wake.
20Kana ashunde leste, bariarenas o anav le Devlesko, phende leske, "Dikhes, amaro phral, sode mi Zhiduvuria pachaiepe ai si le o zakono ande lengo ilo."
20Waliposikia hayo, walimtukuza Mungu. Kisha wakamwambia Paulo, "Ndugu, unaweza kuona kwamba kuna maelfu ya Wayahudi ambao sasa wamekuwa waumini na wote hao wanashika kwa makini Sheria ya Mose.
21Ai won ashunde pa tute, ke tu sichares sa le Zhidovon kai traiin mashkar le Nai Zhiduvuria, te na lenpe pala zakono le Mosesosko, ai ke mothos lenge te na shinen penge glaten ai te na lenpe pala zakono o Zhidovisko.
21Wamepata habari zako kwamba umekuwa ukiwafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa mengine kuwa wasiijali Sheria ya Mose, wasiwatahiri watoto wao na kwamba wasizifuate mila za Wayahudi.
22So te keras? Kodola manush si te chidenpe andek than, ke si te zhangliolpe ke avilian.
22Sasa, mambo yatakuwaje? Ni dhahiri kuwa watapata habari kwamba umekwisha wasili hapa.
23Anda kodia ker so si te mothas tuke. Si mashkar amende shtar manush kai shinade te rhuginpe ai te lenpe pala zakono le Devlesko.
23Basi, fanya kama tunavyokushauri. Tunao hapa watu wanne ambao wameweka nadhiri.
24Anger le tusa, ai zha lensa kai khangeri kai vuzharen, ai pochin anda lende, te rhanden penge bal: ai kadia savorhe zhanena ke nas kanchi chacho pa so phendesas pa tute, numa ke vi tu les tu pala zakono le Mosesosko.
24Jiunge nao katika ibada ya kujitakasa, ukalipe na gharama zinazohusika, kisha wanyolewe nywele zao. Hivyo watu wote watatambua kwamba habari zile walizoambiwa juu yako hazina msingi wowote, na kwamba wewe binafsi bado unaishi kufuatana na maagizo ya Sheria za Mose.
25Numa kodola kai Nai Zhiduvuria kai pachanpe, tradiam lenge ek lil, ai phendiam lenge, te na xan anda mas kai sas dino anglal ikoni, ai chi rat, chi zhigeniengo kai sas tasade, ai te arakhenpe katar e biznibraznia."
25Kuhusu wale watu wa mataifa mengine ambao wamekuwa waumini, tumekwisha wapelekea barua tukiwaambia mambo tuliyoamua: wasile chochote kilichotambikiwa miungu ya uongo, wasinywe damu, wasile nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati."
26O Pavlo lia kodole manushen, vuzhardiape, ai pe terharin gelo ande tamplo lensa, te mothol savo dies o vuzhimos kerdiolape, ai te den iek zhigania sako anda peste.
26Basi, kesho yake Paulo aliwachukua wale watu akafanya ibada ya kujitakasa pamoja nao. Kisha akaingia Hekaluni kutoa taarifa kuhusu mwisho wa siku za kujitakasa na kuhusu dhabihu itakayotolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
27Ai kana o kurko pashte getolaspe, le Zhiduvuria andai Asia avile, ai dikhle le Pavlos ande tampla, buntuisarde sa le narodos, ai line les, tsipinas,
27Wakati siku hizo saba zilipokaribia kuisha, Wayahudi waliokuwa wametoka katika mkoa wa Asia walimwona Paulo Hekaluni. Wakachochea hasira kati ya kundi lote la watu, wakamtia nguvuni
28"Tume kai san anda Isarel, zhutin! Kodo si o manush kai del duma bi malades pal Zhiduvuria ai amaro zakono le Mosesosko, ai pa kadia tampla, ai akana angerdias le Grekuria ande Swunto than, Ai kadia tampla mai nai vuzhi."
28wakipiga kelele: "Wananchi wa Israeli, msaada, msaada! Huyu ndiye yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo yanayopinga watu wa Israeli, yanayopinga Sheria ya Mose na mahali hapa patakatifu. Hata sasa amewaingiza watu wa mataifa mengine Hekaluni na kupatia najisi mahali hapa patakatifu."
29Won mothonas kadia, ke mai anglal o Trophimus andai Ephesus sas lesa ando foro. Ai won gindinas ke o Pavlo angerdiasas les ande tampla.
29Sababu ya kusema hivyo ni kwamba walikuwa wamemwona Trofimo mwenyeji, wa Efeso, akiwa pamoja na Paulo mjini, wakadhani kwamba Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.
30Sa o foro buntuisailo, ai o narodo pa sako rik avelas, line o Pavlos, ai line les avri andai tampla, ai phandade strazo le wudara.
30Mji wote ulienea ghasia; watu wakaja kutoka pande zote, wakamkamata Paulo, wakamburuta, wakamtoa nje ya Hekalu na papo hapo milango ya Hekalu ikafungwa.
31Mangenas te mudaren le Pavlos, numa e viasta avili zhi ka baro le ketanengo kai sas andal Romanuria, ke sa e Jerusalem buntuilaspe.
31Walikuwa tayari kumuua, lakini habari zilimfikia mkuu wa jeshi la Kiroma kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
32Strazo lia pesa ketanen ai mai baren, ai gele lende, kana dikhle le bares le ketanengo ai le ketanen, chi mai marenas le Pavlos.
32Mara, mkuu wa jeshi akawachukua askari na jemadari, akalikabili lile kundi la watu. Nao walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
33Antunchi o baro le ketanengo pashilo pasha Pavlo, lia les, ai phendia te phanden les duie lantsonsa. Ai porme phushlia kon si wo ai so kerdia?
33Mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamtia nguvuni na kuamuru afungwe minyororo miwili. Kisha akauliza, "Ni mtu gani huyu, na amefanya nini?"
34Numa anda narodo uni tsipinas iek diela, uni mothonas aver diela, ai nashtilas te lel o gor kanikastar ke pra but bunto sas, ai phendia leske ketana te angeren o Pavlos ando baro kher le ketanengo.
34Wengine katika lile kundi la watu walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kitu kingine. Kwa sababu ya ghasia hiyo, mkuu wa jeshi hakufaulu kujua kisa kamili. Hivyo, aliamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome.
35Kana aresle kal skeri, le ketani line le Pavlos andel vas ke de but narodo kai sas.
35Paulo alipofika kwenye ngazi, askari walilazimika kumbeba kwa sababu ya fujo za watu.
36Ke savorhe lenaspe pala leste ai tsipinas te mudaren les.
36Kwa maana kundi kubwa la watu walimfuata wakipiga kelele, "Muulie mbali!"
37Strazo kana zhanas ando baro kher le ketanengo o Pavlo phendia le bareske, "Sai mothav vari so tuke?" ai o baro phushel les, "Zhanes te des duma Grechisko?"
37Walipokuwa wanamwingiza ndani ya ngome, Paulo alimwomba mkuu wa jeshi akisema, "Naweza kukwambia kitu?" Yule mkuu wa jeshi akamjibu, "Je unajua Kigiriki?
38"Apo tu chi san o Egypsiano, kai mai buntisailo sas, ai kai angerdia pesa ande pusta shtare mien choren?"
38Kwani wewe si yule Mmisri ambaye hivi majuzi alianzisha uasi na kuwaongoza majahili elfu nne hadi jangwani?"
39O Pavlo phendia, "Zhidovo sim, me sim o Pavlo anda e Tarsus, kai si ande e Cilicia, me kerdilem andek baro foro. Mek ma, mangav ma tutar te dav duma le narodosa."
39Paulo akajibu, "Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia; mimi ni raia wa mji maarufu. Tafadhali, niruhusu niongee na watu.
40O baro le ketanengo meklia les te del duma, o Pavlo ande punrhende sas pel skeri, ai kerelas anda vas le narodoske. Ai kerdilia iek baro chixo (ma nai bunto), ai o Pavlo dia duma lenge ande shib le Zhidovisko ai phenelas,
40Yule mkuu wa jeshi akamruhusu. Hivyo Paulo alisimama juu ya ngazi, akawapungia mkono wale watu na walipokaa kimya, akaanza kuongea nao kwa Kiebrania.