1Pansh dies pala kodia avilo o baro rashai o Anianas ai avre manushensa mai phure, ai ieke ablakatosa ka busholas Tertullus, won avile karing o Felix ando Caesarea te thon dosh po Pavlo.
1Baada ya siku tano, Kuhani Mkuu Anania aliwasili Kaisarea pamoja na wazee kadhaa na wakili mmoja wa sheria aitwaye Tertulo. Walimwendea yule mkuu wa mkoa wakamweleza mashtaka yao juu ya Paulo.
2Akharde le Pavlos, ai o Tertullus liape te dosharel les, phenelas, "Tu kai san baro ando Caesarea, pala tute si ame iek bari pacha, ai but dieli kerdian te avel mishto amare themeske.
2Paulo aliitwa na Tertulo akafungua mashtaka hivi: "Mheshimiwa Felisi, uongozi wako bora umeleta amani kubwa na marekebisho ya lazima yanafanywa kwa manufaa ya taifa letu.
3Ai so godi si ame, ande swako vriama, ai katar godi, ame naisisaras tuke.
3Tunalipokea jambo hili kwa furaha daima na kutoa shukrani nyingi kwako kila mahali.
4Numa te na xasaras chi vriama, mangav ma tutar te ashunes ande cho lashimos so si ame te mothas tuke ande xantsi vorbi.
4Lakini, bila kupoteza wakati wako zaidi, tunakusihi kwa wema wako, usikilize taarifa yetu fupi.
5Ame arakhliam kadale manushes ek manush nai lasho, ai buntuil sa le Zhidovon ande lumia, ai o baro le Nazarengo.
5Tumegundua kwamba mtu huyu ni wa hatari mno. Yeye huanzisha ghasia kati ya Wayahudi kila mahali duniani na pia ni kiongozi wa kile chama cha Wanazareti.
6Ai vi zumadia te marel mui katar o tampla, ai ame aterdiardiam les. Ame mangliam te das les pe kris pala amaro zakono,
6Tena alijaribu kulikufuru Hekalu nasi tukamtia nguvuni. Kama ukimhoji wewe mwenyewe, utaweza kubainisha mambo haya yote tunayomshtaki kwayo." Tulitaka kumhukumu kufuatana na Sheria yetu.
7numa o baro le ketanengo o Lysias kana avilo, lia les anda amare vas ai xaliape amensa.
7Lakini Lusia, mkuu wa jeshi, aliingilia kati, akamchukua kwa nguvu kutoka mikononi mwetu.
8Ai dia ordina kodolen kai thon dosh pe kado manush te aven tute. Dikhesa tu kana phushesa lestar ai ashunesa lestar sa le dieli, kai ame dosharas les."
8Kisha akaamuru washtaki wake waje mbele yako.
9Le Zhiduvuria mai zuravenas e dosh pe leste, ai mothonas ke kadia si.
9Nao Wayahudi waliunga mkono mashtaka hayo wakisema kwamba hayo yote yalikuwa kweli.
10Pala kodia o governori kerdia semno le Pavloske te del duma, o Pavlo dia atweto, "Zhanav ke tu san o baro kadale themesko de dumult, ai bi darako phenav angla tute ke chi sim doshalo.
10Basi, mkuu wa mkoa alimwashiria Paulo aseme. Naye Paulo akasema, "Nafurahi kujitetea mbele yako nikijua kwamba umekuwa hakimu wa taifa hili kwa miaka mingi.
11Sai dikhes tu korkorho ke nai mai but de sar desh u dui dies kai simas ande Jerusalem te rhugiv ma ka Del.
11Unaweza kujihakikishia kwamba si zaidi ya siku kumi na mbili tu zimepita tangu nilipokwenda kuabudu Yerusalemu.
12Chi arakhle ma ande tampla, chi ande chi iek than, chi anda foro te dav duma varikasa, vai te chidav le narodos te buntuilpe.
12Wayahudi hawakunikuta nikijadiliana na mtu yeyote. Hawakunikuta nikichochea watu Hekaluni wala katika masunagogi yao, wala mahali pengine popote katika mji huo.
13Ai nai le so te sikaven te dosharen ma akana.
13Wala hawawezi kuthibitisha mashtaka waliyotoa juu yangu.
14Phenav tuke chachimasa, ke me kerav buchi le Devleski, O Del murhe dadengo, ai lav ma pala drom o nevo kai won mothon ke nai chacho, numa me pachav ma ande so godi si ramome ando zakono ai so mothon le profeturia.
14Ninachokubali mbele yako ni hiki: Mimi ninamwabudu Mungu na wazee wetu nikiishi kufuatana na Njia ile ambayo wao wanaiita chama cha uzushi. Ninaamini mambo yote yaliyoandikwa katika vitabu vya Sheria na manabii.
15Ai si ma o pachamos ando Del, sar sas murhe daden ke zhuvindina, vi le manush kai si vorta ai vi le manush kai nai vorta.
15Mimi namtumainia Mungu, na wao wanalo tumaini hilo, kwamba watu, wema na wabaya, watafufuka.
16Anda kodia thav murhi zor te avel sagda murho gindo bi doshako angla Del, ai angla manush.
16Kwa hiyo ninajitahidi daima kuwa na dhamiri njema mbele ya Mungu na mbele ya watu.
17But bersh gelemtar anda Jerusalem, numa akana avilem te anav zhutimos le lovensa ka murhe narodos.
17"Baada ya kukaa mbali kwa miaka kadhaa, nilirudi Yerusalemu ili kuwapelekea wananchi wenzangu msaada na kutoa dhabihu.
18Uni Zhiduvuria andai Asia arakhle ma ande tampla vuzhardo. Nas narodo mansa, ai nas chi iek bunto.
18Wakati nilipokuwa nikifanya hayo ndipo waliponikuta Hekaluni, nilipokuwa nimekwisha fanya ile ibada ya kujitakasa. Hakukuwako kundi la watu wala ghasia.
19Won trobunas te aven tute, ai te mothon le dosha, kai won sas le pe mande.
19Lakini kulikuwa na Wayahudi wengine kutoka mkoa wa Asia; hao ndio wangepaswa kuwa hapa mbele yako na kutoa mashtaka yao kama wana chochote cha kusema dhidi yangu.
20Vai kakala te mothon, savestar baio won arakhle ke me sim doshalo, kana simas anglal bare kai keren la krisa.
20Au, waache hawa walio hapa waseme kosa waliloliona kwangu wakati niliposimama mbele ya Baraza lao kuu,
21Vai amborim kai tsipisardem kana simas mashkar lende, ai kai phendem ke pachav ma ke le mule wushten, anda kodia dino sim pe kris adies angla tute."
21isipokuwa tu maneno haya niliyosema niliposimama mbele yao: Mnanihukumu leo hii kwa sababu ya kushikilia kwamba wafu watafufuliwa!"
22Ai o Felix zhanelas mishto kodo zakono, ai phendia, "Dikhasa mai angle pa kadia diela, kana o baro le ketanengo o Lysias avela, dikhava so kerava anda chi diela."
22Hapo, Felisi, ambaye mwenyewe alikuwa anaifahamu hiyo Njia vizuri, aliahirisha kesi hiyo. Akawaambia, "Nitatoa hukumu juu ya kesi hiyo wakati Luisa, mkuu wa jeshi, atakapokuja hapa."
23Ai dia ordina ka ek ketana te lel sama katar o Pavlo, te na nashel, numa te meken leske vortachen te dikhen les vai te den les vari so.
23Kisha akamwamuru yule jemadari amweke Paulo kizuizini, lakini awe na uhuru kiasi, na rafiki zake wasizuiwe kumpatia mahitaji yake.
24Xantsi dies pala kodia o Felix avilo peska rhomniasa, woi bushol Drusilla, woi si Zhidovaika. Ai akhardia le Paulos te ashunen sar del duma pa pachamos ando Kristo.
24Baada ya siku chache, Felisi alifika pamoja na mkewe Drusila ambaye alikuwa Myahudi. Aliamuru Paulo aletwe, akamsikiliza akiongea juu ya kumwamini Yesu Kristo.
25Numa o Pavlo delas duma sar te traiis ek traio vorta, ai te les tutar sama, ai e kris kai si te avel pe lumia, o Felix darailo, ai phendia, "Zhatar ai mai ashunava tute aver data kana avela ma vriama."
25Lakini wakati Paulo alipoanza kuongea juu ya uadilifu, juu ya kuwa na kiasi na juu ya siku ya hukumu inayokuja, Felisi aliogopa, akasema, "Kwa sasa unaweza kwenda; nitakuita tena nitakapopata nafasi."
26Ai vi gindilas ke o Pavlo del les love, anda kodia akharela les butivar te del duma lesa.
26Wakati huohuo alikuwa anatumaini kwamba Paulo angempa fedha. Kwa sababu hii alimwita Paulo mara kwa mara na kuzungumza naye.
27Dui bersh nakhle kadia, porme o Porcius Festus lia o than le governorosko o Felix, ai o Felix te avel drago le Zhidovonge, meklia le Pavlos ande temnitsa.
27Baada ya miaka miwili, Porkio Festo alichukua nafasi ya Felisi, akawa mkuu wa Mkoa. Kwa kuwa alitaka kujipendekeza kwa Wayahudi, Felisi alimwacha Paulo kizuizini.