Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Colossians

2

1Mangav te zhanen sode de trutno o marimos kai marav ma anda tumende, ai kodolenge kai si ande Laodicea, ai mai sa kodolenge kai chi zhanen ma ai shoxar chi dikhle ma.
1Napenda mjue jinsi ninavyofanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa ajili ya watu wa Laodikea na kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona kwa macho.
2Marav ma me, saxke lengo ilo te avel pherdo zor ai pechime te aven chidine ande dragostia, ai barvale andek bari goji te zhanen e buchi e garadi le Devleske, ai le Dadesko ai le Kristosko.
2Nafanya hivi kusudi mioyo yao ifarijiwe na kuvutwa pamoja katika upendo, ili wajazwe uthabiti mwingi uletwao na elimu ya kweli. Hapo wataijua siri ya Mungu ambayo ni Kristo mwenyewe.
3Ande leste si garadi sa le barvalimata le pachivalimaske ai le zhanglimaske kai aven katar O Del.
3Ndani yake zimefichika hazina zote za hekima na elimu.
4Me dav duma tumensa kadia, saxke te na meken khonik te dziliarel tumen la xitreniasa.
4Basi, nawaambieni, msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa maneno ya uongo hata kama ni ya kuvutia sana.
5Vi te sim dur tumendar murhe statosa, pasha tumende sim murhe gindonsa, ai raduime sim ke dikhav sar inkeren mishto savorhe andek than ande tumaro pachamos ando Kristo.
5Maana, ingawa mimi niko mbali nanyi kwa mwili, lakini niko pamoja nanyi kwa roho, na ninafurahi kuona uthabiti kamili mnaosimama nao pamoja katika imani yenu kwa Kristo.
6Tume premisardian le Jesus Kristos sar tumaro Devles O Skepitori, traiin andek than lesa.
6Maadamu ninyi mmemkubali Kristo Yesu kuwa Bwana, basi, ishini katika muungano naye.
7Aven zurales astarde ande leste, keren sa tumaro traio pe leste, barion ando pachamos pala so sichilian, ai naisin sagda.
7Mnapaswa kuwa na mizizi ndani yake, kujijenga juu yake na kuwa imara katika imani yenu kama mlivyofundishwa. Muwe na shukrani tele.
8Na meken le kolavren te rimon tumaro pachamos ai tumaro raduimos penge xoxamle sicharimasa, lenge divanuria nai lashe, won len pe palal ginduria le manushenge, ai na pala so phendia O Kristo.
8Angalieni basi, mtu asiwapotoshe kwa udanganyifu mtupu wa hekima ya kibinadamu, ambayo chanzo chake ni mafundisho ya mapokeo ya watu na ya pepo watawala, na wala si Kristo mwenyewe!
9Ke so godi si O Del thodiape sar stato ando Kristo, saxke te avel sa ande leste.
9Maana, ndani yake Kristo katika ubinadamu wake, umo ukamilifu wote wa Mungu,
10Ai tume lian swako fielo lesa. Ke wo poronchil pe sa le zora ai pe sa le putiera kai chi dichon.
10nanyi mmepewa uzima kamili katika kuungana naye. Yeye yuko juu ya pepo watawala wote na wakuu wote.
11Lesa andek than sanas semnome, na o semno kai si kerdo katar le manush, numa o semno kai avel katar O Kristo, ai kodo semno si te na mai aves phuterdo katar e putiera le statoski kai si bezexalo.
11Katika kuungana na Kristo ninyi mlitahiriwa, lakini si kwa tohara ifanywayo na watu, bali inayofanywa na Kristo mwenyewe, na ambayo inahusikana na kukombolewa kutoka katika utu wa dhambi.
12Kana sanas bolde, tume sanas angropome le Kristosa, ai porme zhuvindisailian lesa, ke tume pachaian tume ande putiera le Devleski kai andia les katar e martia ka traio.
12Maana, mlipobatizwa mlizikwa pamoja na Kristo, na katika ubatizo, mlifufuliwa pia pamoja naye kwa imani yenu katika nguvu ya Mungu ambaye alimfufua Kristo kutoka wafu.
13Tume mai anglal mule sanas le Devleske pala tumare bezexa ai ke chi sanas semnome, tume chi zhanenas le Devles. Numa akana O Del dia tume te traiin le Kristosa; O Del iertisardia ame anda sa amare bezexa.
13Wakati mmoja nanyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kwa sababu ninyi mlikuwa watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amewapa ninyi uzima pamoja na Kristo. Mungu ametusamehe dhambi zetu zote;
14Wo xaladia e buchi kai o zakono dosharelas ame, ai kai ashelas pe amende, ai lia sa kana karfosardia le Kristos po trushul.
14alifutilia mbali ile hati ya deni iliyokuwa inatukabili na masharti yake, na kuifuta kabisa kwa kuipigilia msalabani.
15Kadia O Del lia le bengeski putiera kai tholas dosh pe tumende ke bezexale san, ai O Del sikadia sa la lumiake, ke O Kristo nirisardia po trushul kana lia sa tumare bezexa.
15Juu ya msalaba Kristo aliwapokonya nguvu zao hao pepo watawala na wakuu; aliwafanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuwaburuta kama mateka katika msafara wa ushindi wake.
16Na meken khonik te thol tumenge dosh anda so xan, ai anda so pen, vai ke chi keren le praznikuria le Zhidovonge, ai chi rhugin tume ka nevo shunuto, vai kal Sabat.
16Kwa hiyo, basi, msikubali kupewa masharti na mtu yeyote kuhusu vyakula au vinywaji, siku za sherehe, sikukuu ya Mwezi mpya au Sabato.
17Kodia si ek patreto le dielenge kai avena, numa o stato si ando Kristo.
17Mambo ya aina hiyo ni kivuli tu cha yale yatakayokuja; ukweli wenyewe ndiye Kristo.
18Na meken kanikas te mothol ke chi san skepime ke chi rhugin tume kal angeluria, ke won mothon ke trobul. Won mothon ke dikhle iek vizion, ai mothon ke vi tume trobulas te dikhen, ke kasavendar manush si le defial xitro, bezex ginduria ai won mothon ke nai barimatange.
18Msikubali kuhukumiwa na mtu yeyote anayejitakia kuwa wa maana kwa sababu ya maono ya pekee na ambaye anasisitiza juu ya unyenyekevu wa uongo na ibada kwa malaika. Mtu wa namna hiyo amepumbazika kwa fikira danganifu za kidunia
19Kodola manush chi beshen astarde le Kristosa kai si o shero, nais le Kristoske ke ame sam o stato antrego le Kristosko. Amari zor te barios ando Del avel katar O Kristo.
19na amejitenga na Kristo aliye kichwa cha huo mwili. Chini ya uongozi wa Kristo, mwili wote unalishwa na kuunganishwa pamoja kwa viungo na mishipa yake, nao hukua kama atakavyo Mungu.
20Tume mulian ke Kristosa ai sanas line avri anda phanglimos anda gindo kadala lumiako. Sostar, traiin sar te avilianas kadala lumiake? Sostar premin te len tume pala kasavendar ginduria?
20Ninyi mmekufa pamoja na Kristo na kukombolewa kutoka nguvu za pepo watawala wa ulimwengu. Kwa nini, basi, kuishi tena kama vile mngekuwa wa ulimwengu huu? Ya nini kuwekewa masharti:
21"Na azba, na zumav kako, na le kako." Kadala dieli kai si nai mai aven kana ma nai lashe.
21"Msishike hiki," "Msionje kile," "Msiguse kile!"
22Kado si o zakono ai o sicharimos le manushengo.
22Mambo hayo yote yanahusika na vitu vyenye kuharibika mara tu vinapotumiwa; hayo ni maagizo na mafundisho ya kibinadamu tu.
23Miazol kai kadala dieli si mishto te keren, ke kodola dieli si trutno po stato, miazon te na aven barimatange. Won chi aterdiaren o manush te mangen te keren bezex.
23Kweli, masharti hayo yaonekana kuwa ya hekima katika namna ya ibada ya kujitakia wenyewe, unyenyekevu wa uongo na kuutendea mwili kwa ukali; lakini kwa kweli, haifai chochote kuzuia tamaa za mwili.