1Ande kodia vriama po Sabat O Jesus nakhlia pa ek niva kai bariolas jiv, leske disipluria bokhaile, line anda jiv ai xale.
1Wakati huo, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano siku ya Sabato. Basi, wanafunzi wake wakaona njaa, wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakala punje zake.
2Kana le Farizeanuria dikhle kodia, phende leske, "Dikh, che disipluria keren so nai slobodo te keren po Sabat!"
2Mafarisayo walipoona hayo, wakamwambia Yesu, "Tazama, wanafunzi wako wanafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato."
3Wo phendia lenge, 'Chi jindian so kerdia o David kana bokhailo?
3Yesu akawajibu, "Je, hamjasoma alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4Wo ai le manush, kai sas lesa. Sar gelo ando kher le Devlesko, ai xalias andal desh u dui halome manrhe kai nas leske slobodo, te xal, vai kodolenge kai sas lesa, numa le rashange.
4Yeye aliingia katika Nyumba ya Mungu pamoja na wenzake, wakala ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu. Yeye wala hao wenzake hawakuruhusiwa kula mikate hiyo isipokuwa tu makuhani peke yao.
5Vai chi jindian andel zakonuria ke le rasha kai keren buchi ande tamplo po Sabat phagen o zakono, ai nai doshale?"
5Au je, hamjasoma katika Sheria kwamba kila siku ya Sabato makuhani huivunja Sheria Hekaluni, lakini hawafikiriwi kuwa na hatia?
6Phenav tumenge, "Si iek katse mai baro sar e tamplo.
6Basi, nawaambieni kwamba hapa pana kikuu kuliko Hekalu.
7Numa te haliardianas so si o divano, 'Mila me mangav te den, ai na sakrifis.' Antunchi chi doshardianas kodolen kai nai doshale.
7Kama tu mngejua maana ya maneno haya: Nataka huruma wala si dhabihu, hamngewahukumu watu wasio na hatia.
8Ke O Shav le Manushesko si gazda chi po Sabat."
8Maana Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato."
9Antunchi gelotar kotsar ai gelo ande lenge synagogue.
9Yesu alitoka hapo, akaenda katika sunagogi lao.
10Kotse sas iek manush kai sas les vas bango phushle katar O Jesus, "Slobodo te sastiarelpe po Sabat?"
10Kulikuwa na mtu mmoja mwenye mkono uliopooza. Basi, watu wakamwuliza Yesu, "Je, ni halali kumponya mtu siku ya Sabato?" Walimwuliza hivyo wapate kisa cha kumshtaki.
11Kashte te sai dosharen les. Wo phendia lenge, "Savo anda tumende te si les iek bakro, ai te perela ande hunia po Sabat, chi zhal te ankalavel les avri?
11Lakini Yesu akawaambia, "Tuseme mmoja wenu ana kondoo wake ambaye ametumbukia shimoni; je, hatamshika na kumtoa humo siku ya Sabato?
12Sode mai but mol manush sar bakro? Anda kodia slobodo te kerelpe mishtimos po Sabat.
12Mtu ana thamani kuliko kondoo! Basi, ni halali kutenda mema siku ya Sabato."
13Antunchi phendias le manusheske, "Lunzhar cho vas." Wo lunzhardia pesko vas ai sasto sas sar o kolaver.
13Kisha akamwambia yule mtu, "Nyosha mkono wako." Akaunyosha, nao ukawa mzima kabisa kama ule mwingine.
14Le Farizeanuria geletar ai dinepe duma sar te mudaren les.
14Basi, Mafarisayo wakatoka nje, wakashauriana jinsi watakavyomwangamiza Yesu.
15O Jesus zhanglias, ai gelotar kotsar, but manush linepe pala leste, ai sastiardia le sa.
15Lakini Yesu alipojua jambo hilo, akatoka mahali pale. Watu wengi walimfuata, akawaponya wagonjwa wote,
16Ai phendias lenge te na mothon kon si wo ai so kerdias.
16akawaamuru wasiwaambie watu habari zake,
17Te kerdiolpe sar phendiasas o profeto Isaiah.
17ili yale aliyosema nabii Isaya yatimie:
18"Eta, murhi sluga. kai halosardem, kado kai si mange drago, ande kado murho duxo raduilpe. Thava murho duxo pe leste, ai phenela ai sikavela chachi kris ka sa le manush.
18"Hapa ni mtumishi wangu niliyemteua, mpendwa wangu anipendezaye moyoni. Nitaiweka Roho yangu juu yake, naye atatangaza hukumu yangu kwa mataifa yote.
19Chi xalpe ai chi tsipila, chi ashundiola lesko glaso pel vulitsa.
19Hatakuwa na ubishi wala kupiga kelele, wala sauti yake haitasikika barabarani.
20Ci phagela e treshtia kai si bangi, ai chi mudarela e fishtila le lamposki kai si makar thuv, zhi kai chi nirila o chachimos le Devlesko.
20Mwanzi uliopondeka hatauvunja, wala utambi ufukao moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya hukumu ya haki itawale.
21Ai ande lesko anav sa le manush wuzdinape."
21Katika jina lake mataifa yatakuwa na tumaini."
22Antunchi andine ka Jesus iek manush kai sas korho ai muto ke sas beng ande leste. O Jesus sastiardia kodole manushes, ta dias duma ai vi dikhlias.
22Hapo watu wakamletea Yesu kipofu mmoja ambaye alikuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo. Yesu akamponya hata, akaweza kusema na kuona.
23Sa o narodo chudisaile, ai phenenas, "Sai avela kado o Shav le Davidosko?"
23Umati wote wa watu ulishangaa ukasema, "Je, huenda ikawa huyu ndiye Mwana wa Daudi?"
24Numa kana le Farizeanuria ashunde so kerdias phende, "Kado manush gonil le bengen ke o baro le bengengo, o Beelzebub del les e putiera."
24Lakini Mafarisayo waliposikia hayo, wakasema, "Mtu huyu anawafukuza pepo kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo."
25O Jesus zhanelas lenge ginduria, ai phendias lenge, "Swako amperetsia kai si xulade pe peste si te xaiil, swako foro vai familia kai si xulade pe peste chi ashena.
25Yesu, akiwa anayajua mawazo yao, akawaambia, "Ufalme wowote uliogawanyika makundimakundi yanayopingana, hauwezi kudumu, na mji wowote au jamaa yoyote iliyogawanyika makundimakundi yanayopingana, itaanguka.
26Teala o beng gonil le bengen, won si xulade pe peste. Sar rhivdila ai ashela leski amperetisa?
26Ikiwa Shetani anamfukuza Shetani, anajipinga mwenyewe. Basi, ufalme wake utasimamaje?
27Te goniva me le bengen katar e putiera kai o Beelzebub del tumare shave. Katar len won e putiera te gonin le bengen? Anda kodia won si te shinen tumari kris!
27Ninyi mnasema ati nawafukuza pepo kwa uwezo wa Beelzebuli; je, watoto wenu huwafukuza kwa uwezo wa nani? Kwa sababu hiyo wao ndio watakaowahukumu ninyi.
28Numa te goniva me le bengen katar O Swunto Duxo e putiera le Devleski, antunchi e amperetsia le Devleski avili pe tumende.
28Lakini ikiwa ninawafukuza pepo kwa nguvu ya Roho wa Mungu, basi jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekwisha fika kwenu.
29Vai sar sai del vari kon ando kher zurale manushesko ai te lel so si lesko, bi te phandel le zurale manushes ai antunchi te lel so si lesko.
29"Au, anawezaje mtu kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, bila kwanza kumfunga huyo mtu mwenye nguvu? Hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
30Kodo kai nai pe murhi rig chi zhutil ma, numa kerel nasul karing mande; ai kodo kai chi chidel mansa xulavel."
30"Yeyote asiyejiunga nami, anapingana nami; na yeyote asiyekusanya pamoja nami, hutawanya.
31Anda kodia phenav tumenge: "Vari savo bezex vai kai den duma nasul le manush sai iertilpe; numa kon dela duma nasul pe Swunto Duxo shoxar chi avela iertime.
31Kwa sababu hiyo, nawaambieni, watu watasamehewa dhambi na kufuru zao zote, lakini hawatasamehewa dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu.
32Ai kon godi dela duma nasul karing O Shav le Manushesko sai iertilape; numa kon godi dela duma nasul karing O Swunto Duxo chi avela iertime. Chi ande kadia lumia vai e lumia kai si te avel."
32Tena, asemaye neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa, lakini yule asemaye neno la kumpinga Roho Mtakatifu, hatasamehewa, wala katika ulimwengu huu, wala katika ulimwengu ujao.
33Halon te keren e pruing lashi ai e fruta lashi; vai halon te keren e pruing chorhi ai e fruta chorhi ke e pruing prinzhardiol katar peski fruta.
33"Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake yatakuwa mema; ufanyeni kuwa mbaya na matunda yake yatakuwa mabaya. Mti hujulikana kwa matunda yake.
34Tume vitsa sapenge, sar sai den duma lashimos, kana san nasul? Ke so ilo si pherdo, kodia del duma o mui.
34Enyi kizazi cha nyoka! Mnawezaje kusema mambo mema hali ninyi ni waovu? Maana mtu husema kutokana na yale yaliyojaa moyoni.
35Lasho manushesko divano sikavel o barvalimos kai si ande leste, ai manush kai si les nasul ilo pherdo nasulimos lo, ai lesko divano sikavel kodia.
35Mtu mwema hutoa mambo mema katika hazina yake njema; na mtu mbaya hutoa mambo mabaya katika hazina yake mbaya.
36Phenav tumenge, "Le manush trobuna te den atweto po dies kai shindiolpe e kris anda swako vorba kai phende intaino.
36"Basi, nawaambieni, Siku ya hukumu watu watapaswa kujibu juu ya kila neno lisilofaa wanalosema.
37Ke pala chire vorbi avesa jindo chacho, vai pala chire vorbi avesa jindo doshalo."
37Maana kwa maneno yako, utakubaliwa kuwa mwadilifu, na kwa maneno yako, utahukumiwa kuwa na hatia."
38Antunchi uni andal Gramnoturia ai Farizeanuria dine les atweto ai phende leske, "Gazda, mangas te dikhas semno tutar."
38Kisha baadhi ya walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamwambia Yesu, "Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako."
39O Jesus phendias lenge, ferdi ek vitsa kai si nasul ai kai nai chachimasa le Devlesa mangen semno, numa chi iek chi avela dino, ferdi so kerdiliape ka profeto o Jonah.
39Naye akawajibu, "Kizazi kiovu kisicho na uaminifu! Mnataka ishara; hamtapewa ishara nyingine, ila tu ile ishara ya nabii Yona.
40Ke sar o Jonah sas ando ji le bare mashesko trin jes ai trin racha, kadia o Shav le manushesko si te avel ando mashkar la phuviako trin jes ai trin racha.
40Jinsi Yona alivyokaa siku tatu kutwa kucha tumboni mwa nyangumi, ndivyo naye Mwana wa Mtu atakavyokaa ndani ya ardhi siku tatu kutwa kucha.
41Le manush andai Ninevah si te wushten kadala vitsasa kai kris te dosharen len. Ke kana o Jonah dias duma pa Del lenge, won keisaile, ai akana iek mai baro katar o Jonah si katse!
41Watu wa Ninewi watatokea siku ya hukumu, nao watakihukumu kizazi hiki kwamba kina hatia. Maana Waninewi walitubu kwa sababu ya mahubiri ya Yona, na kumbe hapa kuna kikuu kuliko Yona!
42E amperetsasa andai Sheba si te wushtel kadala vitsasa kai kris te dosharel len. Woi avili dural te ashunel ka Soloman ke de sa gojaver sas ai akana si iek mai baro katar o Solomon katse!
42Malkia wa kusini atatokea wakati kizazi hiki kitakapohukumiwa, naye atakihukumu kwamba kina hatia. Maana yeye alisafiri kutoka mbali akaja kusikiliza maneno ya hekima ya Solomoni, na kumbe hapa kuna kikuu kuliko Solomoni.
43Kana o bi vuzho duxo zhaltar anda o manush zhal ando pusta te rodel than te hodinil ai chi arakhel.
43"Pepo mchafu akifukuzwa kwa mtu, huzururazurura jangwani akitafuta mahali pa kupumzika asipate.
44Antunchi mothol, "Amboldav palpale katar avilem" Antunchi amboldel palpale ai arakhel le manushesko ilo vuzho numa nango.
44Hapo hujisemea: Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka. Lakini anaporudi na kuikuta tupu, imefagiwa na kupambwa,
45Antunchi o bi vuzho duxo arakhel efta aver duxuria mai nasul lestar, ai sa zhan te traiin ande kudo manush. Antunchi mai nasul leske de sar mai anglal. Sa kadia si te avel kadala nasul vitsaka.
45huenda kuwachukua pepo wengine saba, wabaya kuliko yeye; na wote huja wakamwingia huyo mtu. Na hali ya mtu huyo sasa huwa mbaya kuliko hapo mwanzo. Ndivyo itakavyokuwa kwa watu hawa waovu."
46Sar O Jesus delas duma le narodosa leske dei ai leske phral avri sas, ai mangenas te den duma lesa.
46Yesu alikuwa bado anasema na umati wa watu wakati mama yake na ndugu zake walipofika na kusimama nje, wakitaka kusema naye.
47Vari kon phendia leske, Chi dei ai che phral avri, ai mangen te den duma tusa."
47Basi, mtu mmoja akamwambia, "Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kusema nawe."
48O Jesus phendias leske, "Kon si murhi dei? Ai kon si murhe phral?"
48Lakini Yesu akamjibu mtu huyo, "Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni kina nani?"
49Anzhardias pesko vas karing peske disipluria ai phendias, 'Eta! Murhi dei ai murhe phral!
49Kisha akaunyosha mkono wake kuelekea wanafunzi wake, akasema, "Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu!
50Ke kon godi kerel e voia murho Dadeske kai si ando rhaio, si murho phral, murhi phei, ai murhi dei."
50Maana yeyote anayefanya anavyotaka Baba yangu aliye mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu."