Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Matthew

4

1Antunchi o Jesus angerdosas katar o Swunto Duxo ande pusta te avel zumado katar o beng.
1Kisha Roho alimwongoza Yesu mpaka jangwani ili ajaribiwe na Ibilisi.
2O Jesus zhunilas ai kana chi xalias shtarvardesh dies ai shtarvardesh racha, bokhailo.
2Akafunga siku arubaini mchana na usiku, na mwishowe akaona njaa.
3O beng avilo ai phendias leske, "Te san O Shav le Devleske, phen te kerdiol anda kadala bax manrho."
3Basi, mshawishi akamjia, akamwambia, "Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate."
4Numa o Jesus phendia, "Ramome ke o manush chi traiila ferdi katar o manrho, numa katar swako vorba kai avel anda mui le Devlesko."
4Yesu akamjibu, "Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: Binadamu hataishi kwa mikate tu, ila kwa kila neno asemalo Mungu."
5Porme o beng ingerdia les ando Swunto foro, ai thodia les ta opre pe tamplo.
5Kisha Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, mji mtakatifu, akamweka juu ya mnara wa hekalu,
6Ai phenel leske, "Te san O Shav le Devlesko, shude tu tele, ke ramome 'O Del phenela peske angelonge te len tut pel vas, kaste te na dukhaves chi cho punrho pek bax.'"
6akamwambia, "Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini; maana imeandikwa: Mungu atawaamuru malaika wake kwa ajili yako; watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa kwenye jiwe."
7O Jesus phenel leske, 'Ai vi ramome, te na zumaves che Devles.'
7Yesu akamwambia, "Imeandikwa pia: Usimjaribu Bwana, Mungu wako."
8Antunchi o beng ingerdia les pe ek bari plai, ai sikadia leske sa le thema la lumiake, ai lengo barimos.
8Kisha Ibilisi akamchukua mpaka juu ya mlima mrefu, akamwonyesha falme zote za ulimwengu na fahari zake,
9Ai phendia leske, "Dava tu sa kadala te thosa tu ande changende te preznais ai te luvudis man."
9akamwambia, "Hivi vyote nitakupa kama tu ukipiga magoti na kuniabudu."
10Antunchi o Jesus phendias leske, " Zhatar Satano ke si ramome, Preznaisar ai luvudisar ferdi che Devles ai servisar ferdi les!"
10Hapo, Yesu akamwambia, "Nenda zako Shetani! Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako na kumtumikia yeye peke yake."
11Antunchi o beng meklia les, ai le angeluria avile ka Jesus ai zhutisarde les.
11Basi, Ibilisi akamwacha, na malaika wakaja, wakamhudumia.
12Kana o Jesus ashundia ke o Iovano sas thodino ande temnitsa, gelo palpale ande Galilee.
12Yesu aliposikia kwamba Yohane ametiwa gerezani alikwenda Galilaya.
13Gelotar andai Nazareth, avilo ai beshlo ande Capernaum, foro kai si pasha e maria karing o Zabulon ai Nephthalim.
13Aliondoka Nazareti, akaenda Kafarnaumu, mji ulio kando ya bahari ya Genesareti, mpakani mwa wilaya za Zabuloni na Naftali, akakaa huko.
14Te pherdiol so o profet o Isaiah phendias,
14Ndivyo lilivyotimia lile neno lililosemwa kwa njia ya nabii Isaya:
15"O them Zabulon, ai o them Nephtalim, karing e maria, inchal o Jordan, e Galilee kai beshen le manush kai Nai Zhiduvuria!
15"Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kuelekea baharini ng'ambo ya mto Yordani, Galilaya nchi ya watu wa Mataifa!
16O narodo kai traiinas ando tuniariko dikhle ek bari vediara. Kodola kai traiinas ande vushalin la martiaki, avili vediara pe lende."
16Watu waliokaa gizani wameona mwanga mkubwa. Nao walioishi katika nchi ya giza na kivuli cha kifo, mwanga umewaangazia!"
17De kotar o Jesus dias duma te phenel, ambolden tume katar tumare bezexa ke e amperetsia le rhaioski pashol!"
17Tangu wakati huo Yesu alianza kuhubiri akisema, "Tubuni, maana ufalme wa mbinguni umekaribia!"
18Sar phirelas o Jesus pasha maria Galilee, dikhlia do phralen, O Simon (akharenas les Petri) ai lesko phral, o Andres, shudenas sita ande maria ke won sas masharia.
18Yesu alipokuwa anatembea kando ya ziwa Galilaya, aliwaona ndugu wawili wavuvi; Simoni (aitwae Petro) na Andrea, ndugu yake; walikuwa wakivua samaki kwa nyavu ziwani.
19O Jesus phendia lenge, "Aven mansa, ai kerava anda tumende masharia kai astaren manushen".
19Basi, akawaambia, "Nifuateni, nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu."
20Strazo mekle penge siti, ai linepe pala leste.
20Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
21Gelo mai angle ai mai dikhlia do phralen, O James ai O Iovano, le shave le Zebedeske ando chuno sas peske dadesa, lasharenas penge siti kana o Jesus akhardia le.
21Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona ndugu wengine wawili: Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Hao walikuwa ndani ya mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakitengeneza nyavu zao. Basi Yesu akawaita,
22Ai strazo mekle o chuno ai peske dades, ai linepe pala leste.
22nao mara wakaiacha mashua pamoja na baba yao, wakamfuata.
23O Jesus gelo ande sa e Galilee, ai sicharelas ande lenge synagoguria, motholas e lashi viasta pa e amperetsia le rhaioski, ai sastiarelas le manushen anda sa lengo naswalimos ai nasulimos.
23Yesu alikuwa anakwenda kila mahali wilayani Galilaya, akifundisha katika masunagogi na kuhubiri Habari Njema juu ya ufalme wa Mungu. Aliponya kila namna ya maradhi na magonjwa waliyokuwa nayo watu.
24Leski viasta geli pe sa e Syria; anda kodia andine leste sa kodolen kai sas le but fialuria naswalimos ai but fialuria dukha, kodola kai sas beng ande lende, kodolen kai zalin ai peren, ai le bangen, ai wo sastisardia le.
24Habari zake zikaenea katika mkoa wote wa Siria. Wagonjwa wote wenye maradhi ya kila namna na wale waliosumbuliwa na kila namna ya taabu: waliopagawa na pepo, wenye kifafa na watu waliokuwa wamelemaa, walipelekwa kwake; naye akawaponya wote.
25Bare naroduria andai Galilee, andai Decapolis, andai Jerusalem, andai Judea, ai inchal o Jordan lenaspe pala leste.
25Makundi mengi ya watu kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Yudea na ng'ambo ya mto Yordani, walimfuata.