Spanish: Reina Valera (1909)

Swahili: New Testament

1 Corinthians

16

1CUANTO á la colecta para los santos, haced vosotros también de la manera que ordené en las iglesias de Galacia.
1Sasa, yahusu ule mchango kwa ajili ya watu wa Mungu: fanyeni kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia.
2Cada primer día de la semana cada uno de vosotros aparte en su casa, guardando lo que por la bondad de Dios pudiere; para que cuando yo llegare, no se hagan entonces colectas.
2Kila Jumapili kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake, ili kusiwe na haja ya kufanya mchango wakati nitakapokuja.
3Y cuando habré llegado, los que aprobareis por cartas, á éstos enviaré que lleven vuestro beneficio á Jerusalem.
3Wakati nitakapokuja kwenu, nitawatuma wale mtakaowachagua miongoni mwenu wapeleke barua na zawadi zenu Yerusalemu.
4Y si fuere digno el negocio de que yo también vaya, irán conmigo.
4Kama itafaa nami niende, basi, watakwenda pamoja nami.
5Y á vosotros iré, cuando hubiere pasado por Macedonia, porque por Macedonia tengo de pasar.
5Nitakuja kwenu, baada ya kupitia Makedonia--maana nataraji kupitia Makedonia.
6Y podrá ser que me quede con vosotros, ó invernaré también, para que vosotros me llevéis á donde hubiere de ir.
6Labda nitakaa kwenu kwa muda fulani, au huenda nitakaa pamoja nanyi wakati wote wa baridi, ili mpate kunisaidia niendelee na safari yangu kokote nitakakokwenda.
7Porque no os quiero ahora ver de paso; porque espero estar con vosotros algún tiempo, si el Señor lo permitiere.
7Sipendi kupita kwenu harakaharaka na kuendelea na safari. Natumaini kukaa kwenu kwa kitambo fulani, Bwana akiniruhusu.
8Empero estaré en Efeso hasta Pentecostés;
8Lakini nitabaki hapa Efeso mpaka siku ya Pentekoste.
9Porque se me ha abierto puerta grande y eficaz, y muchos son los adversarios.
9Mlango uko wazi kabisa kwa ajili ya kazi yangu muhimu hapa, ingawa wapinzani nao ni wengi.
10Y si llegare Timoteo, mirad que esté con vosotros seguramente; porque la obra del Señor hace también como yo.
10Timotheo akija, angalieni asiwe na hofu yoyote wakati yupo kati yenu, kwani anafanya kazi ya Bwana kama mimi.
11Por tanto, nadie le tenga en poco; antes, llevadlo en paz, para que venga á mí: porque lo espero con los hermanos.
11Kwa hiyo mtu yeyote asimdharau, ila msaidieni aendelee na safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu, maana mimi namngojea pamoja na ndugu zetu.
12Acerca del hermano Apolos, mucho le he rogado que fuese á vosotros con los hermanos; mas en ninguna manera tuvo voluntad de ir por ahora; pero irá cuando tuviere oportunidad.
12Kuhusu ndugu Apolo, nimemsihi sana aje kwenu pamoja na ndugu wengine, lakini hapendelei kabisa kuja sasa ila atakuja mara itakapowezekana.
13Velad, estad firmes en la fe; portaos varonilmente, y esforzaos.
13Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.
14Todas vuestras cosas sean hechas con caridad.
14Kila mfanyacho kifanyike kwa upendo.
15Y os ruego, hermanos, (ya sabéis que la casa de Estéfanas es las primicias de Acaya, y que se han dedicado al ministerio de los santos,)
15Ndugu, mnaifahamu jamaa ya Stefana; wao ni watu wa kwanza kabisa kuipokea imani ya Kikristo katika Akaya, na wamejitolea kuwatumikia watu wa Mungu. Ninawasihi ninyi ndugu zangu,
16Que vosotros os sujetéis á los tales, y á todos los que ayudan y trabajan.
16muufuate uongozi wa watu kama hao, na uongozi wa kila mtu afanyaye kazi na kutumikia pamoja nao.
17Huélgome de la venida de Estéfanas y de Fortunato y de Achâico: porque éstos suplieron lo que á vosotros faltaba.
17Nafurahi sana kwamba Stefana, Fortunato na Akaiko wamefika; wamelijaza pengo lililokuwako kwa kutokuwako kwenu.
18Porque recrearon mi espíritu y el vuestro: reconoced pues á los tales.
18Wameiburudisha roho yangu na yenu pia. Kwa hiyo inafaa kuwakumbuka watu wa namna hii.
19Las iglesias de Asia os saludan. Os saludan mucho en el Señor Aquila y Priscila, con la iglesia que está en su casa.
19Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priskila pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika Bwana.
20Os saludan todos los hermanos. Saludaos los unos á los otros con ósculo santo.
20Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
21La salutación de mí, Pablo, de mi mano.
21Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
22El que no amare al Señor Jesucristo, sea anatema. Maranatha.
22Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANA THA--BWANA, njoo!
23La gracia del Señor Jesucristo sea con vosotros.
23Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
24Mi amor en Cristo Jesús sea con todos vosotros. Amén.
24Mapendo yangu yawe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.