1EMPERO acerca de los tiempos y de los momentos, no tenéis, hermanos, necesidad de que yo os escriba:
1Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
2Porque vosotros sabéis bien, que el día del Señor vendrá así como ladrón de noche,
2Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
3Que cuando dirán, Paz y seguridad, entonces vendrá sobre ellos destrucción de repente, como los dolores á la mujer preñada; y no escaparán.
3Watu watakapokuwa wanasema: "Kila kitu ni shwari na salama" ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
4Mas vosotros, hermanos, no estáis en tinieblas, para que aquel día os sobrecoja como ladrón;
4Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
5Porque todos vosotros sois hijos de luz, é hijos del día; no somos de la noche, ni de las tinieblas.
5Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
6Por tanto, no durmamos como los demás; antes velemos y seamos sobrios.
6Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
7Porque los que duermen, de noche duermen; y los que están borrachos, de noche están borrachos.
7Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
8Mas nosotros, que somos del día, estemos sobrios, vestidos de cota de fe y de caridad, y la esperanza de salud por yelmo.
8Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
9Porque no nos ha puesto Dios para ira, sino para alcanzar salud por nuestro Señor Jesucristo;
9Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
10El cual murió por nosotros, para que ó que velemos, ó que durmamos, vivamos juntamente con él.
10ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
11Por lo cual, consolaos los unos á los otros, y edificaos los unos á los otros, así como lo hacéis.
11Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
12Y os rogamos, hermanos, que reconozcáis á los que trabajan entre vosotros, y os presiden en el Señor, y os amonestan:
12Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
13Y que los tengáis en mucha estima por amor de su obra. Tened paz los unos con los otros.
13Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
14También os rogamos, hermanos, que amonestéis á los que andan desordenadamente, que consoléis á los de poco ánimo, que soportéis á los flacos, que seáis sufridos para con todos.
14Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
15Mirad que ninguno dé á otro mal por mal; antes seguid lo bueno siempre los unos para con los otros, y para con todos.
15Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
16Estad siempre gozosos.
16Furahini daima,
17Orad sin cesar.
17salini kila wakati
18Dad gracias en todo; porque esta es la voluntad de Dios para con vosotros en Cristo Jesús.
18na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
19No apaguéis el Espíritu.
19Msimpinge Roho Mtakatifu;
20No menospreciéis las profecías.
20msidharau unabii.
21Examinadlo todo; retened lo bueno.
21Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
22Apartaos de toda especie de mal.
22na epukeni kila aina ya uovu.
23Y el Dios de paz os santifique en todo; para que vuestro espíritu y alma y cuerpo sea guardado entero sin reprensión para la venida de nuestro Señor Jesucristo.
23Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu--roho, mioyo na miili yenu--mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24Fiel es el que os ha llamado; el cual también lo hará.
24Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
25Hermanos, orad por nosotros.
25Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
26Saludad á todos los hermanos en ósculo santo.
26Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
27Conjúroos por el Señor, que esta carta sea leída á todos los santos hermanos.
27Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
28La gracia de nuestro Señor Jesucristo sea con vosotros. Amén. {espístola á los Tesalonicenses fué escrita de Atenas.}
28Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.