Spanish: Reina Valera (1909)

Swahili: New Testament

1 Timothy

2

1AMONESTO pues, ante todas cosas, que se hagan rogativas, oraciones, peticiones, hacimientos de gracias, por todos los hombres;
1Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,
2Por los reyes y por todos los que están en eminencia, para que vivamos quieta y reposadamente en toda piedad y honestidad.
2kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.
3Porque esto es bueno y agradable delante de Dios nuestro Salvador;
3Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,
4El cual quiere que todos los hombres sean salvos, y que vengan al conocimiento de la verdad.
4ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
5Porque hay un Dios, asimismo un mediador entre Dios y los hombres, Jesucristo hombre;
5Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,
6El cual se dió á sí mismo en precio del rescate por todos, para testimonio en sus tiempos:
6ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.
7De lo que yo soy puesto por predicador y apóstol, (digo verdad en Cristo, no miento) doctor de los Gentiles en fidelidad y verdad.
7Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
8Quiero, pues, que los hombres oren en todo lugar, levantando manos limpias, sin ira ni contienda.
8Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.
9Asimismo también las mujeres, ataviándose en hábito honesto, con vergüenza y modestia; no con cabellos encrespados, u oro, ó perlas, ó vestidos costosos.
9Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10Sino de buenas obras, como conviene á mujeres que profesan piedad.
10bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.
11La mujer aprenda en silencio, con toda sujeción.
11Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
12Porque no permito á la mujer enseñar, ni tomar autoridad sobre el hombre, sino estar en silencio.
12Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
13Porque Adam fué formado el primero, después Eva;
13Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
14Y Adam no fué engañado, sino la mujer, siendo seducida, vino á ser envuelta en transgresión:
14Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
15Empero se salvará engendrando hijos, si permaneciere en la fe y caridad y santidad, con modestia.
15Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.