1ESTAD, pues, firmes en la libertad con que Cristo nos hizo libres, y no volváis otra vez á ser presos en el yugo de servidumbre.
1Kristo alitupa uhuru akataka tubaki huru. Basi, simameni imara wala msikubali tena kuwa chini ya nira ya utumwa.
2He aquí yo Pablo os digo, que si os circuncidareis, Cristo no os aprovechará nada.
2Sikilizeni! Ni mimi Paulo ninayesema nanyi! Kama mkikubali kutahiriwa, Kristo hatawafaidia chochote.
3Y otra vez vuelvo á protestar á todo hombre que se circuncidare, que está obligado á hacer toda la ley.
3Nasema tena wazi: kila anayekubali kutahiriwa itambidi kuishika Sheria yote.
4Vacíos sois de Cristo los que por la ley os justificáis; de la gracia habéis caído.
4Kama mnatazamia kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Sheria, basi, mmejitenga mbali na Kristo; mko nje ya neema ya Mungu.
5Porque nosotros por el Espíritu esperamos la esperanza de la justicia por la fe.
5Kwa upande wetu, lakini, sisi tunatumaini kwamba kwa nguvu ya Roho tunakubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani.
6Porque en Cristo Jesús ni la circuncisión vale algo, ni la incircuncisión; sino la fe que obra por la caridad.
6Maana ikiwa tumeungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutotahiriwa hakuna maana; cha maana ni imani ifanyayo kazi kwa mapendo.
7Vosotros corríais bien: ¿quién os embarazó para no obedecer á la verdad?
7Mwenendo wenu ulikuwa mzuri! Nani, basi aliyewazuia kuuzingatia ukweli?
8Esta persuasión no es de aquel que os llama.
8Aliyesababisha hali hiyo si Mungu ambaye amewaiteni.
9Un poco de levadura leuda toda la masa.
9"chachu kidogo tu huchachusha donge lote la unga!"
10Yo confío de vosotros en el Señor, que ninguna otra cosa sentiréis: mas el que os inquieta, llevará el juicio, quienquiera que él sea.
10Kutokana na kuungana kwetu na Bwana, nina tumaini kubwa kwamba ninyi hamtakuwa na msimamo tofauti nami. Tena yeyote huyo anayewavurugeni--awe nani au nani--hakika ataadhibiwa.
11Y yo, hermanos, si aun predico la circuncisión, ¿por qué padezco pesecución todavía? pues que quitado es el escándalo de la cruz.
11Na kwa upande wangu, ndugu zangu, kama bado ninahubiri kwamba kutahiriwa ni lazima, kwa nini basi, bado ninadhulumiwa? Kama ingalikuwa hivyo, mahubiri yangu juu ya msalaba wa Kristo yasingalileta aibu yoyote.
12Ojalá fuesen también cortados los que os inquietan.
12Laiti hao wanaowavurugeni wangejikatakata wenyewe!
13Porque vosotros, hermanos, á libertad habéis sido llamados; solamente que no uséis la libertad como ocasión á la carne, sino servíos por amor los unos á los otros.
13Ninyi, ndugu, mliitwa muwe watu huru. Lakini uhuru huo usiwe kisingizio cha kutawaliwa na tamaa za kidunia; ila mnapaswa kutumikiana kwa upendo.
14Porque toda la ley en aquesta sola palabra se cumple: Amarás á tu prójimo como á ti mismo.
14Maana Sheria yote hutimizwa katika kushika amri hii moja: "Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe."
15Y si os mordéis y os coméis los unos á los otros, mirad que también no os consumáis los unos á los otros.
15Lakini ikiwa mtaumana na kutafunana kama wanyama, jihadharini msije mkaangamizana wenyewe kwa wenyewe!
16Digo pues: Andad en el Espíritu, y no satisfagáis la concupiscencia de la carne.
16Basi, nasema hivi: mwenendo wenu na uongozwe na Roho, nanyi hamtafuata tena tamaa za kidunia.
17Porque la carne codicia contra el Espíritu, y el Espíritu contra la carne: y estas cosas se oponen la una á la otra, para que no hagáis lo que quisieres.
17Maana, tamaa za kidunia hupingana na matakwa ya Roho; na matakwa ya Roho hupingana na tamaa za kidunia. Mambo hayo mawili hayaafikiani; kwa sababu hiyo hamwezi kufanya yale mnayotaka ninyi wenyewe.
18Mas si sois guiados del Espíritu, no estáis bajo la ley.
18Kama mkiongozwa na Roho, basi, hamko tena chini ya Sheria.
19Y manifiestas son las obras de la carne, que son: adulterio, fornicación, inmundicia, disolución,
19Basi, matendo ya kidunia yanajulikana: uzinzi, uasherati, ufisadi;
20Idolatría, hechicerías, enemistades, pleitos, celos, iras, contiendas, disensiones, herejías,
20kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, choyo, mabishano, mafarakano;
21Envidias, homicidios, borracheras, banqueteos, y cosas semejantes á éstas: de las cuales os denuncio, como ya os he anunciado, que los que hacen tales cosas no heredarán el reino de Dios.
21husuda, ulevi, ulafi na mambo mengine kama hayo. Nawaambieni tena kama nilivyokwisha sema: watu wanaotenda mambo hayo hawatakuwa na nafasi yao katika ufalme wa Mungu.
22Mas el fruto del Espíritu es: caridad, gozo, paz, tolerancia, benignidad, bondad, fe,
22Lakini matokeo ya kuongozwa na Roho ni mapendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fadhili, uaminifu,
23Mansedumbre, templanza: contra tales cosas no hay ley.
23upole na kuwa na kiasi. Hakuna Sheria inayoweza kupinga mambo hayo.
24Porque los que son de Cristo, han crucificado la carne con los afectos y concupiscencias.
24Wale walio wa Kristo wameisulubisha hali yao ya kidunia pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
25Si vivimos en el Espíritu, andemos también en el Espíritu.
25Tukiishi kwa msaada wa Roho, na tuufuate mwongozo wake.
26No seamos codiciosos de vana gloria, irritando los unos á los otros, envidiándose los unos á los otros.
26Basi, tusijivune, tusichokozane wala kuoneana wivu.