Spanish: Reina Valera (1909)

Swahili: New Testament

Matthew

22

1Y RESPONDIENDO Jesús, les volvió á hablar en parábolas, diciendo:
1Yesu alisema nao tena kwa kutumia mifano:
2El reino de los cielos es semejante á un hombre rey, que hizo bodas á su hijo;
2"Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme aliyemwandalia mwanawe karamu ya arusi.
3Y envió sus siervos para que llamasen los llamados á las bodas; mas no quisieron venir.
3Basi, akawatuma watumishi kuwaita walioalikwa waje arusini, lakini walioalikwa hawakutaka kufika.
4Volvió á enviar otros siervos, diciendo: Decid á los llamados: He aquí, mi comida he aparejado; mis toros y animales engordados son muertos, y todo está prevenido: venid á las bodas.
4Akawatuma tena watumishi wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa: karamu yangu iko tayari sasa; fahali wangu na ng'ombe wanono wamekwisha chinjwa; kila kitu ni tayari, njoni arusini.
5Mas ellos no se cuidaron, y se fueron, uno á su labranza, y otro á sus negocios;
5Lakini wao hawakujali, wakaenda zao; mmoja shambani kwake, mwingine kwenye shughuli zake,
6Y otros, tomando á sus siervos, los afrentaron y los mataron.
6na wengine wakawakamata wale watumishi wakawatukana, wakawaua.
7Y el rey, oyendo esto, se enojó; y enviando sus ejércitos, destruyó á aquellos homicidas, y puso fuego á su ciudad.
7Yule mfalme akakasirika, akawatuma askari wake wakawaangamize wauaji hao na kuuteketeza mji wao.
8Entonces dice á sus siervos: Las bodas á la verdad están aparejadas; mas los que eran llamados no eran dignos.
8Kisha akawaambia watumishi wake: Karamu ya arusi iko tayari kweli, lakini walioalikwa hawakustahili.
9Id pues á las salidas de los caminos, y llamad á las bodas á cuantos hallareis.
9Basi, nendeni kwenye barabara na wowote wale mtakaowakuta waiteni waje arusini.
10Y saliendo los siervos por los caminos, juntaron á todos los que hallaron, juntamente malos y buenos: y las bodas fueron llenas de convidados.
10Wale watumishi wakatoka, wakaenda njiani, wakawaleta watu wote, wabaya na wema. Nyumba ya arusi ikajaa wageni.
11Y entró el rey para ver los convidados, y vió allí un hombre no vestido de boda.
11"Mfalme alipoingia kuwaona wageni, akamwona mtu mmoja ambaye hakuvaa mavazi ya arusi.
12Y le dijo: Amigo, ¿cómo entraste aquí no teniendo vestido de boda? Mas él cerró la boca.
12Mfalme akamwuliza, Rafiki, umeingiaje hapa bila vazi la arusi? Lakini yeye akakaa kimya.
13Entonces el rey dijo á los que servían: Atado de pies y de manos tomadle, y echadle en las tinieblas de afuera: allí será el lloro y el crujir de dientes.
13Hapo mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni miguu na mikono mkamtupe nje gizani; huko atalia na kusaga meno."
14Porque muchos son llamados, y pocos escogidos.
14Yesu akamaliza kwa kusema, "Wengi wamealikwa, lakini wachache wameteuliwa."
15Entonces, idos los Fariseos, consultaron cómo le tomarían en alguna palabra.
15Kisha, Mafarisayo wakaenda zao, wakashauriana jinsi ya kumnasa Yesu kwa maneno yake.
16Y envían á él los discípulos de ellos, con los Herodianos, diciendo: Maestro, sabemos que eres amador de la verdad, y que enseñas con verdad el camino de Dios, y que no te curas de nadie, porque no tienes acepción de persona de hombres.
16Basi, wakawatuma wafuasi wao pamoja na wafuasi wa kikundi cha Herode. Wakamwuliza, "Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwaminifu, na kwamba wafundisha njia ya Mungu kwa uaminifu; humwogopi mtu yeyote, maana cheo cha mtu si kitu kwako.
17Dinos pues, ¿qué te parece? ¿es lícito dar tributo á César, ó no?
17Haya, twambie maoni yako. Je, ni halali au la, kulipa Kaisari?"
18Mas Jesús, entendida la malicia de ellos, les dice: ¿Por qué me tentáis, hipócritas?
18Lakini Yesu alitambua uovu wao, akawaambia, "Enyi
19Mostradme la moneda del tributo. Y ellos le presentaron un denario.
19Nionyesheni fedha ya kulipia kodi." Nao wakamtolea sarafu ya fedha. sarafu ya fedha.
20Entonces les dice: ¿Cúya es esta figura, y lo que está encima escrito?
20Basi, Yesu akawauliza, "Sura na chapa hii ni ya nani?"
21Dícenle: De César. Y díceles: Pagad pues á César lo que es de César, y á Dios lo que es de Dios.
21Wakamjibu, "Ni vya Kaisari." Hapo Yesu akawaambia, "Basi, mpeni Kaisari yaliyo yake Kaisari, na Mungu yaliyo yake Mungu."
22Y oyendo esto, se maravillaron, y dejándole se fueron.
22Waliposikia hivyo wakashangaa; wakamwacha, wakaenda zao.
23Aquel día llegaron á él los Saduceos, que dicen no haber resurrección, y le preguntaron,
23Siku hiyo, baadhi ya Masadukayo walimwendea Yesu. Hao ndio wale wasemao kwamba wafu hawafufuki.
24Diciendo: Maestro, Moisés dijo: Si alguno muriere sin hijos, su hermano se casará con su mujer, y despertará simiente á su hermano.
24Basi, wakamwambia, "Mwalimu, Mose alisema mtu aliyeoa akifa bila kuacha watoto, lazima ndugu yake amwoe huyo mama mjane, amzalie ndugu yake watoto.
25Fueron pues, entre nosotros siete hermanos: y el primero tomó mujer, y murió; y no teniendo generación, dejó su mujer á su hermano.
25Sasa, hapa petu palikuwa na ndugu saba. Wa kwanza alioa kisha akafa bila kujaliwa watoto, akamwachia ndugu yake huyo mke wake mjane.
26De la misma manera también el segundo, y el tercero, hasta los siete.
26Ikawa vivyo hivyo kwa ndugu wa pili, na wa tatu, mpaka wa saba.
27Y después de todos murió también la mujer.
27Baada ya ndugu hao wote kufa, akafa pia yule mama.
28En la resurrección pues, ¿de cuál de los siete será ella mujer? porque todos la tuvieron.
28Je, siku wafu watakapofufuka mama huyo atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba? Maana Wote saba walimwoa."
29Entonces respondiendo Jesús, les dijo: Erráis ignorando las Escrituras, y el poder de Dios.
29Yesu akawajibu, "Kweli mmekosea kwa sababu hamjui Maandiko Matakatifu wala nguvu ya Mungu!
30Porque en la resurrección, ni los hombres tomarán mujeres, ni las mujeres marido; mas son como los ángeles de Dios en el cielo.
30Maana wafu watakapofufuliwa hawataoa wala kuolewa, watakuwa kama malaika mbinguni.
31Y de la resurrección de los muertos, ¿no habéis leído lo que os es dicho por Dios, que dice:
31Lakini kuhusu suala la wafu kufufuka, hamjasoma yale aliyowaambieni Mungu?
32Yo soy el Dios de Abraham, y el Dios de Isaac, y el Dios de Jacob? Dios no es Dios de muertos, sino de vivos.
32Aliwaambia, Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo! Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai."
33Y oyendo esto las gentes, estaban atónitas de su doctrina.
33Ule umati wa watu uliposikia hivyo ukayastaajabia mafundisho yake.
34Entonces los Fariseos, oyendo que había cerrado la boca á los Saduceos, se juntaron á una.
34Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, wakakutana pamoja.
35Y preguntó uno de ellos, intérprete de la ley, tentándole y diciendo:
35Mmoja wao, mwanasheria, akamwuliza Yesu kwa kumjaribu,
36Maestro, ¿cuál es el mandamiento grande en la ley?
36"Mwalimu, ni amri ipi iliyo kuu katika Sheria ya Mose?"
37Y Jesús le dijo: Amarás al Señor tu Dios de todo tu corazón, y de toda tu alma, y de toda tu mente.
37Yesu akamjibu, "Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote na kwa akili yako yote.
38Este es el primero y el grande mandamiento.
38Hii ndiyo amri kuu ya kwanza.
39Y el segundo es semejante á éste: Amarás á tu prójimo como á ti mismo.
39Ya pili inafanana na hiyo: Mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe.
40De estos dos mandamientos depende toda la ley y los profetas.
40Sheria yote ya Mose na mafundisho ya manabii vinategemea amri hizi mbili."
41Y estando juntos los Fariseos, Jesús les preguntó,
41Mafarisayo walipokusanyika pamoja, Yesu aliwauliza,
42Diciendo: ¿Qué os parece del Cristo? ¿de quién es Hijo? Dícenle: De David.
42"Ninyi mwaonaje juu ya Kristo? Je, ni mwana wa nani?" Wakamjibu, "Wa Daudi."
43El les dice: ¿Pues cómo David en Espíritu le llama Señor, diciendo:
43Yesu akawaambia, "Basi, inawezekanaje kwamba kwa nguvu ya Roho Mtakatifu Daudi anamwita yeye Bwana? Maana alisema:
44Dijo el Señor á mi Señor: Siéntate á mi diestra, Entre tanto que pongo tus enemigos por estrado de tus pies?
44Bwana alimwambia Bwana wangu: keti upande wangu wa kulia, mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako.
45Pues si David le llama Señor, ¿cómo es su Hijo?
45Basi, ikiwa Daudi anamwita Kristo Bwana, anawezaje kuwa mwanawe?"
46Y nadie le podía responder palabra; ni osó alguno desde aquel día preguntarle más.
46Hakuna mtu yeyote aliyeweza kumjibu neno. Na tangu siku hiyo hakuna aliyethubutu tena kumwuliza swali.