1PABLO, prisionero de Jesucristo, y el hermano Timoteo, á Filemón amado, y coadjutor nuestro;
1Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu
2Y á la amada Apphia, y á Archîpo, compañero de nuestra milicia, y á la iglesia que está en tu casa:
2na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkupo.
3Gracia á vosotros y paz de Dios nuestro Padre, y del Señor Jesucristo.
3Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yesu Kristo.
4Doy gracias á mi Dios, haciendo siempre memoria de ti en mis oraciones.
4Kila wakati ninaposali nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu
5Oyendo tu caridad, y la fe que tienes en el Señor Jesús, y para con todos los santos;
5maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana wetu Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
6Para que la comunicación de tu fe sea eficaz, en el conocimiento de todo el bien que está en vosotros, por Cristo Jesús.
6Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo.
7Porque tenemos gran gozo y consolación de tu caridad, de que por ti, oh hermano, han sido recreadas las entrañas de los santos.
7Ndugu, upendo wako yameniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
8Por lo cual, aunque tengo mucha resolución en Cristo para mandarte lo que conviene,
8Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya.
9Ruégo te más bien por amor, siendo tal cual soy, Pablo viejo, y aun ahora prisionero de Jesucristo:
9Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
10Ruégote por mi hijo Onésimo, que he engendrado en mis prisiones,
10Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni.
11El cual en otro tiempo te fué inútil, mas ahora á ti y á mí es útil;
11Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
12El cual te vuelvo á enviar; tu pues, recíbele como á mis entrañas.
12Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.
13Yo quisiera detenerle conmigo, para que en lugar de ti me sirviese en las prisiones del evangelio;
13Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Habari Njema.
14Mas nada quise hacer sin tu consejo, porque tu beneficio no fuese como de necesidad, sino voluntario.
14Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
15Porque acaso por esto se ha apartado de ti por algún tiempo, para que le recibieses para siempre;
15Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima.
16No ya como siervo, antes más que siervo, como hermano amado, mayormente de mí, pero cuánto más de ti, en la carne y en el Señor.
16Na sasa yeye si mtumwa tu, ila ni bora zaidi ya mtumwa: yeye ni ndugu yetu mpenzi. Na wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.
17Así que, si me tienes por compañero, recíbele como á mi.
17Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.
18Y si en algo te dañó, ó te debe, ponlo á mi cuenta.
18Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi.
19Yo Pablo lo escribí de mi mano, yo lo pagaré: por no decirte que aun á ti mismo te me debes demás.
19Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako.)
20Sí, hermano, góceme yo de ti en el Señor; recrea mis entrañas en el Señor.
20Haya, basi, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.
21Te he escrito confiando en tu obediencia, sabiendo que aun harás más de lo que digo.
21Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba.
22Y asimismo prepárame también alojamiento; porque espero que por vuestras oraciones os tengo de ser concedido.
22Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.
23Te saludan Epafras, mi compañero en la prisión por Cristo Jesús,
23Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu.
24Marcos, Aristarco, Demas y Lucas, mis cooperadores.
24Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu.
25La gracia de nuestro Señor Jesucristo sea con vuestro espíritu. Amén.
25Nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.