Zarma

Swahili: New Testament

Hebrews

7

1 Malcizadaka wo, Salim kwaara bonkoono no, alfaga no Irikoy Beeray-Beeri-Koyo se. A koy ka Ibrahim kubay waato kaŋ a ye ka kaa ka fun bonkooney boŋ zaamayaŋo do. A na Ibrahim albarkandi mo.
1Melkisedeki alikuwa mfalme wa Salemu, na kuhani wa Mungu Mkuu. Abrahamu alipokuwa anarudi kutoka vitani ambako aliwaua wafalme, Melkisedeki alikutana naye akambariki,
2 A se no Ibrahim na hay kulu zakka no. (Sintina day, Malcizadaka maa feerijo ga ti adilitaraykoy. Woodin banda nga no ga ti Salim bonkoono, laakal kanay bonkoono nooya.
2naye Abrahamu akampa sehemu ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo. (Maana ya kwanza ya jina hili Melkisedeki ni "Mfalme wa Uadilifu"; na, kwa vile yeye alikuwa mfalme wa Salemu, jina lake pia lina maana ya "Mfalme wa Amani.")
3 A sinda baaba, a sinda nya, a sinda asuli* lasaabuyaŋ, a jirbey sinda sintinay, a fundo mo si ban. Amma a hima Irikoy Izo cine.) Malcizadaka din alfaga no duumi.
3Baba yake na mama yake hawatajwi, wala ukoo wake hautajwi; haisemwi alizaliwa lini au alikufa lini. Anafanana na Mwana wa Mungu, na anaendelea kuwa kuhani daima.
4 Guna ka di boro wo beera, kaŋ se Ibrahim iri kaay-kaayo na wongu arzaka zakka no.
4Basi, mwaona jinsi mtu huyu alivyokuwa maarufu. Baba Abrahamu alimpa sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyoteka vitani.
5 Lawi izey ra, wo kaŋ yaŋ gonda alfagataray du lordi asariya* boŋ kaŋ ne i ma zakka ta jama gaa kaŋ ga ti i nya-izey, baa kaŋ nya-izey din mo fun Ibrahim banda gaa.
5Tunajua vilevile kwamba kufuatana na Sheria, wana wa Lawi ambao ni makuhani, wanayo haki ya kuchukua sehemu ya kumi kutoka kwa watu, yaani ndugu zao, ingawaje nao ni watoto wa Abrahamu.
6 Amma bora din kaŋ i s'a asulo lasaabu i do na zakka ta Ibrahim gaa. A na albarka daŋ bora kaŋ se Irikoy na alkawley no gaa mo.
6Lakini huyo Melkisedeki hakuwa wa ukoo wa Lawi, hata hivyo alipokea sehemu ya kumi kutoka kwa Abrahamu; tena akambariki yeye ambaye alikuwa amepewa ahadi ya Mungu.
7 Kakaw si, boro kaŋ ga kayna ga du albarka boro kaŋ ga beeri nd'a kambe ra.
7Hakuna mashaka hata kidogo kwamba anayebariki ni mkuu zaidi kuliko yule anayebarikiwa.
8 Neewo mo, borey kaŋ yaŋ ga bu ga zakka ta. Amma yongo, boro go no _g'i ta|_ kaŋ i seeda kaŋ a go ga funa.
8Tena, hao makuhani wanaopokea sehemu ya kumi, ni watu ambao hufa; lakini hapa anayepokea sehemu ya kumi, yaani Melkisedeki, anasemekana kwamba hafi.
9 Boro ga hin ka ne mo kaŋ Lawi kaŋ ga zakka ta, nga bumbo na zakka no waato kaŋ Ibrahim n'a no,
9Twaweza, basi, kusema kwamba Abrahamu alipotoa sehemu moja ya kumi, Lawi (ambaye watoto wake hupokea sehemu moja ya kumi) alitoa sehemu moja ya kumi pia.
10 zama waato kaŋ Malcizadaka kubay da Ibrahim, Lawi go nga kaayo gaahamo ra jina.
10Maana Lawi hakuwa amezaliwa bado, bali ni kama alikuwa katika mwili wa baba yake, Abrahamu, wakati Melkisedeki alipokutana naye.
11 Yaadin gaa, da toonandiyaŋ go Lawi alfagatara ra (zama alfagatara din boŋ no asariya* kaŋ i no jama se bara) a si hima i ma alfaga waani fo daŋ, Malcizadaka wano cine, kaŋ manti Haruna* wano cine.
11Kutokana na ukuhani wa Walawi, watu wa Israeli walipewa Sheria. Sasa, kama huduma ya Walawi ingalikuwa kamilifu hapangekuwa tena na haja ya kutokea ukuhani mwingine tofauti, ukuhani ambao umefuata utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki, na si ule wa Aroni.
12 Zama, za kaŋ alfagatara barmay, tilas kal asariya mo ma barmay.
12Maana ukuhani ukibadilika ni lazima Sheria nayo ibadilike.
13 Zama bora kaŋ ciine i te hayey din ra, a kunda go waani. Kunda din ra boro kulu mana saajaw te sargay* feema se.
13Naye Bwana wetu ambaye mambo hayo yote yanasemwa juu yake, alikuwa wa kabila lingine, na wala hakuna hata mmoja wa kabila lake aliyepata kutumikia madhabahuni akiwa kuhani.
14 Zama boro kulu ga bay kaŋ iri Rabbi mana fun kala Yahuda kunda gaa, kunda no kaŋ Musa man'a ciine te alfagataray sanno ra.
14Inafahamika wazi kwamba yeye alizaliwa katika kabila la Yuda ambalo Mose hakulitaja alipokuwa anasema juu ya makuhani.
15 Haya kaŋ iri goono ga ne bangay mo taray kwaaray ka tonton, za kaŋ alfaga waani fo tun, Malcizadaka wano cine,
15Tena jambo hili ni dhahiri zaidi: kuhani mwingine anayefanana na Melkisedeki amekwisha tokea.
16 kaŋ mana ciya alfaga asariya lordey kaŋ ga ti gaaham waney boŋ, amma fundi kaŋ si ban dabaro boŋ.
16Yeye hakufanywa kuwa kuhani kwa sheria na maagizo ya kibinadamu, bali kwa nguvu ya uhai ambao hauna mwisho.
17 Zama Irikoy seeda a se ka ne: «Ni ya alfaga no hal abada, Malcizadaka wano cine.»
17Maana Maandiko yasema: "Wewe ni kuhani milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki."
18 Yaadin gaa, i na doŋ lordo kaa, za kaŋ a sinda gaabi, a sinda albarka mo.
18Basi, ile amri ya zamani ilifutwa kwa sababu ilikuwa hafifu na isiyofaa kitu.
19 Zama _Musa|_ asariya mana hay kulu toonandi. Amma beeje kaŋ ga boori ka bisa furo, kaŋ a do no iri go ga maan Irikoy gaa.
19Maana Sheria ya Mose haikuweza kukamilisha jambo lolote. Lakini sasa, mahali pake pamewekwa tumaini lililo bora zaidi ambalo kwalo tunaweza kumkaribia Mungu.
20 Irikoy n'a daŋ mo zeyaŋ boŋ.
20Zaidi ya hayo hapa pana kiapo cha Mungu. Wakati wale wengine walipofanywa makuhani hapakuwako kiapo.
21 Zama Lawitey* mana ciya alfagayaŋ zeyaŋ boŋ, amma nga wo _ciya alfaga|_ zeyaŋ boŋ, bora do kaŋ ne a se: «Rabbi ze, zeyaŋo si tun mo. A ne: ‹Ni ya alfaga no hal abada.› »
21Lakini Yesu alifanywa kuhani kwa kiapo wakati Mungu alipomwambia: "Bwana ameapa, wala hataigeuza nia yake: Wewe ni kuhani milele."
22 Zeyaŋo din boŋ mo no Yesu ciya tabbatandiko alkawlo se kaŋ bisa afa din booriyaŋ.
22Basi, kutokana na tofauti hii, Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.
23 Koyne Lawitey alfagey ciya iboobo, zama buuyaŋ g'i ganji i ma goro duumi.
23Kuna tofauti nyingine pia: hao makuhani wengine walikuwa wengi kwa sababu walikufa na hawakuweza kuendelea na kazi yao.
24 Amma Almasihu wo, zama a go no hal abada, a gonda alfagataray kaŋ i si ye boro fo do.
24Lakini Yesu si kama wao, yeye anaishi milele; ukuhani wake hauondoki kwake.
25 Woodin sabbay se no a gonda dabari ka borey no faaba toonante, ngey kaŋ yaŋ go ga maan Irikoy gaa a do, zama alwaati kulu a go ga funa hal a ma ŋwaarayyaŋ te i se.
25Hivyo, yeye anaweza daima kuwaokoa kabisa wote wanaomwendea Mungu kwa njia yake, maana yeye anaishi milele kuwaombea kwa Mungu.
26 Alfaga beero wo dumi no iri hima nd'a: ihanno, baanikom, kaŋ sinda ziibi, kaŋ go fayante da zunubikooney, kaŋ beera beeri ka bisa beena.
26Basi, Yesu ndiye Kuhani Mkuu ambaye anatufaa sana katika mahitaji yetu. Yeye ni mtakatifu, hana hatia wala dhambi ndani yake; hayumo katika kundi la wenye dhambi na ameinuliwa mpaka juu mbinguni.
27 A manti sanda alfaga beeri fey din cine. Manti tilas no a ma sargayyaŋ salle zaari kulu, sintina nga bumbo zunubey se, waato din gaa jama waney se. Zama a na sargay salle sorro folloŋ lok! waato kaŋ a na nga boŋ salle sargay.
27Yeye si kama wale makuhani wakuu wengine; hana haja ya kutoa dhabihu kila siku, kwanza kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kisha kwa ajili ya dhambi za watu. Yeye alifanya hivyo mara moja tu wakati alipojitoa yeye mwenyewe, na hiyo yatosha kwa nyakati zote.
28 Asariya ga alfaga beeri yaŋ daŋ kaŋ gazanteyaŋ no. Amma Irikoy zeyaŋo kaŋ kaa asariya* banda na Ize daŋ, kaŋ nga wo toonante no hal abada.
28Sheria ya Mose huwateua watu waliokuwa dhaifu kuwa makuhani wakuu; lakini ahadi ya Mungu aliyoifanya kwa kiapo na ambayo imefika baada ya sheria imemteua Mwana ambaye amefanywa mkamilifu milele.