Zarma

Swahili: New Testament

Matthew

1

1 Yesu Almasihu kaajo tira neeya, Dawda izo, Ibrahim ize.
1Yesu Kristo alikuwa mzawa wa Daudi, mzawa wa Abrahamu. Hii ndiyo orodha ya ukoo wake:
2 Ibrahim na Isaka hay, Isaka mo na Yakuba hay, Yakuba na Yahuda nda nga nya-izey hay,
2Abrahamu alimzaa Isaka, Isaka alimzaa Yakobo, Yakobo alimzaa Yuda na ndugu zake,
3 Yahuda na Farisa nda Zera hay Tamar gaa, Farisa mo na Hezron hay, Hezron na Arama hay,
3Yuda alimzaa Faresi na Zera (mama yao alikuwa Tamari), Faresi alimzaa Hesroni, Hesroni alimzaa Rami,
4 Arama na Aminadab hay, Aminadab na Nason hay, Nason na Salmon hay,
4Rami alimzaa Aminadabu, Aminadabu alimzaa Nashoni, Nashoni alimzaa Salmoni,
5 Salmon na Buwaza hay Rahab gaa, Buwaza na Obida hay Ruta gaa, Obida na Yasse hay,
5Salmoni alimzaa Boazi (mama yake Boazi alikuwa Rahabu). Boazi na Ruthi walikuwa wazazi wa Obedi, Obedi alimzaa Yese,
6 Yasse mo na Bonkoono Dawda hay. Dawda mo na Suleymanu hay Uriya wande zeena gaa,
6naye Yese alimzaa Mfalme Daudi. Daudi alimzaa Solomoni (mama yake Solomoni alikuwa mke wa Uria).
7 Suleymanu mo na Rehobowam hay, Rehobowam na Abiya hay, Abiya na Asa hay,
7Solomoni alimzaa Rehoboamu, Rehoboamu alimzaa Abiya, Abiya alimzaa Asa,
8 Asa na Yehosafat hay, Yehosafat mo na Yoram hay, Yoram na Uzziya hay,
8Asa alimzaa Yehoshafati, Yehoshafati alimzaa Yoramu, Yoramu alimzaa Uzia,
9 Uzziya na Yotam hay, Yotam na Ahaz hay, Ahaz na Hezeciya hay,
9Uzia alimzaa Yothamu, Yothamu alimzaa Ahazi, Ahazi alimzaa Hezekia,
10 Hezeciya na Manasse hay, Manasse na Amon hay, Amon na Yosiya hay,
10Hezekia alimzaa Manase, Manase alimzaa Amoni, Amoni alimzaa Yosia,
11 Yosiya na Yekoniya nda nga nya-izey hay dira ka koy Babila* yaŋo alwaato ra.
11Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake. Huo ulikuwa wakati Wayahudi walipopelekwa uhamishoni Babuloni.
12 Dira ka koy Babila banda, Yekoniya na Salitila hay, Salitila na Zerubabel hay,
12Baada ya Wayahudi kupelekwa uhamishomi Babuloni: Yekonia alimzaa Shealtieli, Shealtieli alimzaa Zerobabeli,
13 Zerubabel na Abihud hay, Abihud na Eliyacim hay, Eliyacim na Azura hay,
13Zerobabeli alimzaa Abiudi, Abiudi alimzaa Eliakimu, Eliakimu alimzaa Azori,
14 Azura na Zadok hay, Zadok na Ahima hay, Ahima na Aliyuda hay,
14Azori alimzaa Zadoki, Zadoki alimzaa Akimu, Akimu alimzaa Eliudi,
15 Aliyuda na Eliyezar hay, Eliyezar na Mattana hay, Mattana na Yakuba hay,
15Eliudi alimzaa Eleazeri, Eleazeri alimzaa Mathani, Mathani alimzaa Yakobo,
16 Yakuba na Yusufu, Maryama kurnyo, hay, Maryama kaŋ gaa i na Yesu, kaŋ se i ga ne Almasihu, hay.
16Yakobo alimzaa Yosefu, aliyekuwa mume wake Maria, mama yake Yesu, aitwaye Kristo.
17 Kaayey kulu za Ibrahim gaa ka koy Dawda gaa, iway cindi taaci no. Dawda gaa ka koy Babila koyyaŋ diraw, nga mo iway cindi taaci no. Babila koyyaŋ diraw banda mo ka kaa Almasihu gaa, kaay way cindi taaci no.
17Basi, kulikuwa na vizazi kumi na vinne tangu Abrahamu mpaka Daudi, vizazi kumi na vinne tangu Daudi mpaka Wayahudi walipochukuliwa mateka Babuloni, na vizazi kumi na vinne tangu kuchukuliwa mateka mpaka wakati wa Kristo.
18 Mate kaŋ Yesu Almasihu hayyaŋo bara nd'a neeya: alwaato kaŋ i na hiijay alkawlo te a nyaŋo Maryama nda Yusufu game ra, za i mana care kubay jina, i na Maryama gar da gunde Biya* Hanna do.
18Basi, hivi ndivyo Yesu Kristo alivyozaliwa: Maria, mama yake, alikuwa ameposwa na Yosefu. Lakini kabla hawajakaa pamoja kama mume na mke, alionekana kuwa mja mzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
19 A kurnyo Yusufu binde, zama nga wo boro adili no, a si ba nga m'a daŋ batama, a miila nga m'a taŋ tuguyaŋ ra.
19Yosefu, mumewe, kwa vile alikuwa mwadilifu, hakutaka kumwaibisha hadharani; hivyo alikusudia kumwacha kwa siri.
20 Amma za a goono ga woodin fongu nga bina ra, kal Rabbi* malayka bangay a se hindiri ra ka ne a se: «Yusufu, Dawda izo, ma si humburu Maryama hiija, naŋ a ma ciya ni wande, zama izo kaŋ go a gunda ra din, Biya Hanno do wane no.
20Alipokuwa bado anawaza jambo hilo, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akamwambia, "Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria awe mke wako, maana amekuwa mja mzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
21 A ga ize aru hay, ni g'a maa daŋ Yesu mo, zama nga no ga nga borey faaba i zunubey gaa.»
21Atajifungua mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yesu, kwa kuwa yeye atawaokoa watu wake kutoka katika dhambi zao."
22 Woodin kulu mo, a ciya no zama i ma Rabbi sanno kaŋ a ci annabi* do din toonandi kaŋ ne:
22Basi, haya yote yalitukia ili litimie lile neno Bwana alilosema kwa njia ya nabii:
23 «Guna, wandiyo ga te gunde, a ga ize aru hay mo, i g'a maa daŋ Immanuwel,» (danga, Irikoy go iri game ra nooya.)
23"Bikira atachukua mimba, atamzaa mtoto wa kiume, naye ataitwa Emanueli" (maana yake, "Mungu yu pamoja nasi").
24 Yusufu tun nga jirbo gaa ka te sanda mate kaŋ cine Rabbi malayka na nga lordi* nd'a. A na nga wando sambu.
24Hivyo, Yosefu alipoamka usingizini alifanya kama malaika huyo alivyomwambia, akamchukua mke wake nyumbani.
25 Amma a man'a bay wayboro, kal a na izo hay. A n'a maa daŋ Yesu.
25Lakini hakumjua kamwe kimwili hata Maria alipojifungua mtoto wa kiume. Naye Yosefu akampa jina Yesu.