1Kutokana na hayo, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, namwomba Mungu.
1For this cause I Paul, the prisoner of Jesus Christ for you Gentiles,
2Bila shaka mmekwisha sikia kwamba Mungu, kwa neema yake, alinikabidhi kazi hii niifanye kwa faida yenu.
2If ye have heard of the dispensation of the grace of God which is given me to you-ward:
3Mimi nilijulishwa kwa njia ya ufunuo mpango wake uliofichika. (Nimeandika kwa ufupi juu ya jambo hili,
3How that by revelation he made known unto me the mystery; (as I wrote afore in few words,
4nanyi mkiyasoma maneno yangu mtaweza kujua jinsi ninavyoielewa siri hiyo ya Kristo.)
4Whereby, when ye read, ye may understand my knowledge in the mystery of Christ)
5Zamani watu hawakujulishwa siri hiyo; lakini sasa Mungu amewajulisha mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho.
5Which in other ages was not made known unto the sons of men, as it is now revealed unto his holy apostles and prophets by the Spirit;
6Siri yenyewe ni hii: kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapata sehemu yao pamoja na Wayahudi katika zile baraka za Mungu; wao ni viungo vya mwili uleule, na wanashiriki ahadi ileile aliyofanya Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
6That the Gentiles should be fellowheirs, and of the same body, and partakers of his promise in Christ by the gospel:
7Mimi nimefanywa kuwa mtumishi wa Habari Njema kwa neema ya pekee aliyonijalia Mungu kwa uwezo wake mkuu.
7Whereof I was made a minister, according to the gift of the grace of God given unto me by the effectual working of his power.
8Mimi ni mdogo kuliko watu wote wa Mungu; lakini amenijalia neema yake, ili niwahubirie watu wa mataifa utajiri wake Kristo usiopimika,
8Unto me, who am less than the least of all saints, is this grace given, that I should preach among the Gentiles the unsearchable riches of Christ;
9tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele,
9And to make all men see what is the fellowship of the mystery, which from the beginning of the world hath been hid in God, who created all things by Jesus Christ:
10kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi.
10To the intent that now unto the principalities and powers in heavenly places might be known by the church the manifold wisdom of God,
11Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
11According to the eternal purpose which he purposed in Christ Jesus our Lord:
12Basi, katika kuungana na Kristo, na kwa njia ya imani katika Kristo, sisi tunathubutu kumkaribia Mungu kwa uhodari.
12In whom we have boldness and access with confidence by the faith of him.
13Kwa hiyo, nawaombeni msife moyo kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, maana hayo ni kwa ajili ya utukufu wenu.
13Wherefore I desire that ye faint not at my tribulations for you, which is your glory.
14Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,
14For this cause I bow my knees unto the Father of our Lord Jesus Christ,
15aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni.
15Of whom the whole family in heaven and earth is named,
16Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu,
16That he would grant you, according to the riches of his glory, to be strengthened with might by his Spirit in the inner man;
17naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo
17That Christ may dwell in your hearts by faith; that ye, being rooted and grounded in love,
18kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina.
18May be able to comprehend with all saints what is the breadth, and length, and depth, and height;
19Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
19And to know the love of Christ, which passeth knowledge, that ye might be filled with all the fulness of God.
20Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu, aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;
20Now unto him that is able to do exceeding abundantly above all that we ask or think, according to the power that worketh in us,
21kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina.
21Unto him be glory in the church by Christ Jesus throughout all ages, world without end. Amen.