Swahili: New Testament

King James Version

Ephesians

5

1Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
1Be ye therefore followers of God, as dear children;
2Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
2And walk in love, as Christ also hath loved us, and hath given himself for us an offering and a sacrifice to God for a sweetsmelling savour.
3Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
3But fornication, and all uncleanness, or covetousness, let it not be once named among you, as becometh saints;
4Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
4Neither filthiness, nor foolish talking, nor jesting, which are not convenient: but rather giving of thanks.
5Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
5For this ye know, that no whoremonger, nor unclean person, nor covetous man, who is an idolater, hath any inheritance in the kingdom of Christ and of God.
6Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
6Let no man deceive you with vain words: for because of these things cometh the wrath of God upon the children of disobedience.
7Basi, msishirikiane nao.
7Be not ye therefore partakers with them.
8Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
8For ye were sometimes darkness, but now are ye light in the Lord: walk as children of light:
9maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
9(For the fruit of the Spirit is in all goodness and righteousness and truth;)
10Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
10Proving what is acceptable unto the Lord.
11Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
11And have no fellowship with the unfruitful works of darkness, but rather reprove them.
12Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
12For it is a shame even to speak of those things which are done of them in secret.
13Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
13But all things that are reproved are made manifest by the light: for whatsoever doth make manifest is light.
14na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: "Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza."
14Wherefore he saith, Awake thou that sleepest, and arise from the dead, and Christ shall give thee light.
15Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
15See then that ye walk circumspectly, not as fools, but as wise,
16Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
16Redeeming the time, because the days are evil.
17Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
17Wherefore be ye not unwise, but understanding what the will of the Lord is.
18Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
18And be not drunk with wine, wherein is excess; but be filled with the Spirit;
19Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
19Speaking to yourselves in psalms and hymns and spiritual songs, singing and making melody in your heart to the Lord;
20Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
20Giving thanks always for all things unto God and the Father in the name of our Lord Jesus Christ;
21Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
21Submitting yourselves one to another in the fear of God.
22Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
22Wives, submit yourselves unto your own husbands, as unto the Lord.
23Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
23For the husband is the head of the wife, even as Christ is the head of the church: and he is the saviour of the body.
24Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
24Therefore as the church is subject unto Christ, so let the wives be to their own husbands in every thing.
25Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
25Husbands, love your wives, even as Christ also loved the church, and gave himself for it;
26Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
26That he might sanctify and cleanse it with the washing of water by the word,
27kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
27That he might present it to himself a glorious church, not having spot, or wrinkle, or any such thing; but that it should be holy and without blemish.
28Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
28So ought men to love their wives as their own bodies. He that loveth his wife loveth himself.
29(Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
29For no man ever yet hated his own flesh; but nourisheth and cherisheth it, even as the Lord the church:
30maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
30For we are members of his body, of his flesh, and of his bones.
31Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja."
31For this cause shall a man leave his father and mother, and shall be joined unto his wife, and they two shall be one flesh.
32Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
32This is a great mystery: but I speak concerning Christ and the church.
33Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.
33Nevertheless let every one of you in particular so love his wife even as himself; and the wife see that she reverence her husband.