Swahili: New Testament

King James Version

Hebrews

3

1Ndugu zangu watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu ambaye Mungu alimtuma awe Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama.
1Wherefore, holy brethren, partakers of the heavenly calling, consider the Apostle and High Priest of our profession, Christ Jesus;
2Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
2Who was faithful to him that appointed him, as also Moses was faithful in all his house.
3Mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Hali kadhalika naye Yesu anastahili heshima kubwa zaidi kuliko Mose.
3For this man was counted worthy of more glory than Moses, inasmuch as he who hath builded the house hath more honour than the house.
4Kila nyumba hujengwa na mjenzi fulani--na Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
4For every house is builded by some man; but he that built all things is God.
5Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye.
5And Moses verily was faithful in all his house, as a servant, for a testimony of those things which were to be spoken after;
6Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tukizingatia uhodari wetu na uthabiti wetu katika kile tunachotumainia.
6But Christ as a son over his own house; whose house are we, if we hold fast the confidence and the rejoicing of the hope firm unto the end.
7Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo,
7Wherefore (as the Holy Ghost saith, To day if ye will hear his voice,
8msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu; kama walivyokuwa siku ile kule jangwani,
8Harden not your hearts, as in the provocation, in the day of temptation in the wilderness:
9Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, asema Bwana, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu kwa miaka arobaini.
9When your fathers tempted me, proved me, and saw my works forty years.
10Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu.
10Wherefore I was grieved with that generation, and said, They do alway err in their heart; and they have not known my ways.
11Basi, nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko."
11So I sware in my wrath, They shall not enter into my rest.)
12Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai.
12Take heed, brethren, lest there be in any of you an evil heart of unbelief, in departing from the living God.
13Maadamu hiyo "Leo" inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi.
13But exhort one another daily, while it is called To day; lest any of you be hardened through the deceitfulness of sin.
14Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
14For we are made partakers of Christ, if we hold the beginning of our confidence stedfast unto the end;
15Maandiko yasema hivi: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu."
15While it is said, To day if ye will hear his voice, harden not your hearts, as in the provocation.
16Ni akina nani basi, waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri.
16For some, when they had heard, did provoke: howbeit not all that came out of Egypt by Moses.
17Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arobaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani.
17But with whom was he grieved forty years? was it not with them that had sinned, whose carcases fell in the wilderness?
18Mungu alipoapa: "Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko," alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi.
18And to whom sware he that they should not enter into his rest, but to them that believed not?
19Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.
19So we see that they could not enter in because of unbelief.