Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

1 Corinthians

15

1Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
1And I make known to you, brethren, the good news that I proclaimed to you, which also ye did receive, in which also ye have stood,
2Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
2through which also ye are being saved, in what words I proclaimed good news to you, if ye hold fast, except ye did believe in vain,
3Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
3for I delivered to you first, what also I did receive, that Christ died for our sins, according to the Writings,
4kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
4and that he was buried, and that he hath risen on the third day, according to the Writings,
5kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
5and that he appeared to Cephas, then to the twelve,
6Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
6afterwards he appeared to above five hundred brethren at once, of whom the greater part remain till now, and certain also did fall asleep;
7Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
7afterwards he appeared to James, then to all the apostles.
8Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
8And last of all — as to the untimely birth — he appeared also to me,
9Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
9for I am the least of the apostles, who am not worthy to be called an apostle, because I did persecute the assembly of God,
10Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
10and by the grace of God I am what I am, and His grace that [is] towards me came not in vain, but more abundantly than they all did I labour, yet not I, but the grace of God that [is] with me;
11Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
11whether, then, I or they, so we preach, and so ye did believe.
12Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
12And if Christ is preached, that out of the dead he hath risen, how say certain among you, that there is no rising again of dead persons?
13Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
13and if there be no rising again of dead persons, neither hath Christ risen;
14na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
14and if Christ hath not risen, then void [is] our preaching, and void also your faith,
15Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua--kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
15and we also are found false witnesses of God, because we did testify of God that He raised up the Christ, whom He did not raise if then dead persons do not rise;
16Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
16for if dead persons do not rise, neither hath Christ risen,
17Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
17and if Christ hath not risen, vain is your faith, ye are yet in your sins;
18Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
18then, also, those having fallen asleep in Christ did perish;
19Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
19if in this life we have hope in Christ only, of all men we are most to be pitied.
20Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
20And now, Christ hath risen out of the dead — the first-fruits of those sleeping he became,
21Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
21for since through man [is] the death, also through man [is] a rising again of the dead,
22Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
22for even as in Adam all die, so also in the Christ all shall be made alive,
23Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
23and each in his proper order, a first-fruit Christ, afterwards those who are the Christ`s, in his presence,
24Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
24then — the end, when he may deliver up the reign to God, even the Father, when he may have made useless all rule, and all authority and power —
25Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
25for it behoveth him to reign till he may have put all the enemies under his feet —
26Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
26the last enemy is done away — death;
27Maana, Maandiko yasema: "Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake." Lakini, Maandiko yanaposema: "Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale" ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
27for all things He did put under his feet, and, when one may say that all things have been subjected, [it is] evident that He is excepted who did subject the all things to him,
28Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
28and when the all things may be subjected to him, then the Son also himself shall be subject to Him, who did subject to him the all things, that God may be the all in all.
29Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
29Seeing what shall they do who are baptized for the dead, if the dead do not rise at all? why also are they baptized for the dead?
30Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
30why also do we stand in peril every hour?
31Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
31Every day do I die, by the glorying of you that I have in Christ Jesus our Lord:
32Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, "Tule na tunywe, maana kesho tutakufa."
32if after the manner of a man with wild beasts I fought in Ephesus, what the advantage to me if the dead do not rise? let us eat and drink, for to-morrow we die!
33Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
33Be not led astray; evil communications corrupt good manners;
34Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
34awake up, as is right, and sin not; for certain have an ignorance of God; for shame to you I say [it].
35Lakini mtu anaweza kuuliza: "Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?"
35But some one will say, `How do the dead rise?
36Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
36unwise! thou — what thou dost sow is not quickened except it may die;
37Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
37and that which thou dost sow, not the body that shall be dost thou sow, but bare grain, it may be of wheat, or of some one of the others,
38Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
38and God doth give to it a body according as He willed, and to each of the seeds its proper body.
39Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
39All flesh [is] not the same flesh, but there is one flesh of men, and another flesh of beasts, and another of fishes, and another of birds;
40Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
40and [there are] heavenly bodies, and earthly bodies; but one [is] the glory of the heavenly, and another that of the earthly;
41Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
41one glory of sun, and another glory of moon, and another glory of stars, for star from star doth differ in glory.
42Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
42So also [is] the rising again of the dead: it is sown in corruption, it is raised in incorruption;
43Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
43it is sown in dishonour, it is raised in glory; it is sown in weakness, it is raised in power;
44Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
44it is sown a natural body, it is raised a spiritual body; there is a natural body, and there is a spiritual body;
45Maana Maandiko yasema: "Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;" lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
45so also it hath been written, `The first man Adam became a living creature,` the last Adam [is] for a life-giving spirit,
46Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
46but that which is spiritual [is] not first, but that which [was] natural, afterwards that which [is] spiritual.
47Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
47The first man [is] out of the earth, earthy; the second man [is] the Lord out of heaven;
48Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
48as [is] the earthy, such [are] also the earthy; and as [is] the heavenly, such [are] also the heavenly;
49Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
49and, according as we did bear the image of the earthy, we shall bear also the image of the heavenly.
50Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
50And this I say, brethren, that flesh and blood the reign of God is not able to inherit, nor doth the corruption inherit the incorruption;
51Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
51lo, I tell you a secret; we indeed shall not all sleep, and we all shall be changed;
52wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
52in a moment, in the twinkling of an eye, in the last trumpet, for it shall sound, and the dead shall be raised incorruptible, and we — we shall be changed:
53Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
53for it behoveth this corruptible to put on incorruption, and this mortal to put on immortality;
54Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: "Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!"
54and when this corruptible may have put on incorruption, and this mortal may have put on immortality, then shall be brought to pass the word that hath been written, `The Death was swallowed up — to victory;
55"Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?"
55where, O Death, thy sting? where, O Hades, thy victory?`
56Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
56and the sting of the death [is] the sin, and the power of the sin the law;
57Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
57and to God — thanks, to Him who is giving us the victory through our Lord Jesus Christ;
58Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.
58so that, my brethren beloved, become ye stedfast, unmovable, abounding in the work of the Lord at all times, knowing that your labour is not vain in the Lord.