1Anathubutuje mmoja wenu kumshtaki ndugu muumini mbele ya mahakama ya watu wasiomjua Mungu badala ya kumshtaki mbele ya watu wa Mungu?
1Dare any one of you, having a matter with the other, go to be judged before the unrighteous, and not before the saints?
2Je, hamjui kwamba watu wa Mungu watauhukumu ulimwengu? Ikiwa basi, ulimwengu utahukumiwa nanyi, kwa nini hamstahili kuhukumu hata katika mambo madogo?
2have ye not known that the saints shall judge the world? and if by you the world is judged, are ye unworthy of the smaller judgments?
3Je, hamjui kwamba, licha ya kuhukumu mambo ya kawaida ya kila siku, tutawahukumu hata malaika?
3have ye not known that we shall judge messengers? why not then the things of life?
4Mnapokuwa na mizozo juu ya mambo ya kawaida, je, mnawaita wawe mahakimu watu ambao hata hawalijali kanisa?
4of the things of life, indeed, then, if ye may have judgment, those despised in the assembly — these cause ye to sit;
5Aibu kwenu! Ndiyo kusema hakuna hata mmoja miongoni mwenu mwenye hekima kiasi cha kuweza kutatua tatizo kati ya ndugu waumini?
5unto your shame I speak: so there is not among you one wise man, not even one, who shall be able to discern in the midst of his brethren!
6Badala yake, kweli imekuwa mtindo ndugu kumpeleka ndugu yake mahakamani, tena mbele ya mahakimu wasioamini.
6but brother with brother doth go to be judged, and this before unbelievers!
7Kwa kweli huko kushtakiana tu wenyewe kwa wenyewe kwabainisha kwamba mmeshindwa kabisa! Je, haingekuwa jambo bora zaidi kwenu kudhulumiwa! Haingekuwa bora zaidi kwenu kunyang'anywa mali yenu?
7Already, indeed, then, there is altogether a fault among you, that ye have judgments with one another; wherefore do ye not rather suffer injustice? wherefore be ye not rather defrauded?
8Lakini, badala yake, ninyi ndio mnaodhulumu na kunyang'anya; tena, hayo mnawafanyia ndugu zenu!
8but ye — ye do injustice, and ye defraud, and these — brethren!
9Au je, hamjui kwamba watu wabaya hawataurithi Utawala wa Mungu? Msijidanganye! Watu wanaoishi maisha ya uasherati, wanaoabudu sanamu, wazinzi, au walawiti,
9have ye not known that the unrighteous the reign of God shall not inherit? be not led astray; neither whoremongers, nor idolaters, nor adulterers, nor effeminate, nor sodomites,
10wevi, wachoyo, walevi, wasengenyaji, wanyang'anyi, hao wote hawatashiriki Utawala wa Mungu.
10nor thieves, nor covetous, nor drunkards, nor revilers, nor extortioners, the reign of God shall inherit.
11Baadhi yenu mlikuwa hivyo; lakini sasa mmeoshwa, mkafanywa watakatifu, na kupatanishwa na Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.
11And certain of you were these! but ye were washed, but ye were sanctified, but ye were declared righteous, in the name of the Lord Jesus, and in the Spirit of our God.
12Mtu anaweza kusema: "Kwangu mimi kila kitu ni halali." Sawa; lakini si kila kitu kinafaa. Nakubali kwamba kila kitu ni halali kwangu lakini sitaki kutawaliwa na kitu chochote.
12All things are lawful to me, but all things are not profitable; all things are lawful to me, but I — I will not be under authority by any;
13Unaweza kusema: "Chakula ni kwa ajili ya tumbo, na tumbo ni kwa ajili ya chakula." Sawa; lakini Mungu ataviharibu vyote viwili. Mwili wa mtu si kwa ajili ya uzinzi bali ni kwa ajili ya kumtumikia Bwana, naye Bwana ni kwa ajili ya mwili.
13the meats [are] for the belly, and the belly for the meats. And God both this and these shall make useless; and the body [is] not for whoredom, but for the Lord, and the Lord for the body;
14Basi, Mungu aliyemfufua Bwana kutoka wafu atatufufua nasi pia kwa nguvu yake.
14and God both the Lord did raise, and us will raise up through His power.
15Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo vya mwili wa Kristo? Je, mnadhani naweza kuchukua sehemu ya mwili wa Kristo na kuifanya kuwa sehemu ya mwili wa kahaba? Hata kidogo!
15Have ye not known that your bodies are members of Christ? having taken, then, the members of the Christ, shall I make [them] members of an harlot? let it be not!
16Maana, kama mjuavyo, anayeungana na kahaba huwa mwili mmoja naye--kama ilivyoandikwa: "Nao wawili watakuwa mwili mmoja."
16have ye not known that he who is joined to the harlot is one body? `for they shall be — saith He — the two for one flesh.`
17Lakini aliyejiunga na Bwana huwa roho moja naye.
17And he who is joined to the Lord is one spirit;
18Jiepusheni kabisa na uzinzi. Dhambi nyingine zote hutendwa nje ya mwili lakini mzinzi hutenda dhambi dhidi ya mwili wake mwenyewe.
18flee the whoredom; every sin — whatever a man may commit — is without the body, and he who is committing whoredom, against his own body doth sin.
19Je, hamjui kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, ambaye mlimpokea kutoka kwa Mungu? Ninyi basi, si mali yenu wenyewe.
19Have ye not known that your body is a sanctuary of the Holy Spirit in you, which ye have from God? and ye are not your own,
20Mlinunuliwa kwa bei kubwa. Kwa hiyo, itumieni miili yenu kwa ajili ya kumtukuza Mungu.
20for ye were bought with a price; glorify, then, God in your body and in your spirit, which are God`s.