1Yahusu sasa vyakula vilivyotambikiwa sanamu: Tunajua kwamba sisi sote tuna ujuzi, lakini ujuzi huo huwafanya watu wawe na majivuno; lakini mapendo hujenga.
1And concerning the things sacrificed to idols, we have known that we all have knowledge: knowledge puffeth up, but love buildeth up;
2Anayefikiri kwamba anajua kitu, kwa kweli hajui chochote kama inavyompasa.
2and if any one doth think to know anything, he hath not yet known anything according as it behoveth [him] to know;
3Lakini anayempenda Mungu huyo anajulikana naye.
3and if any one doth love God, this one hath been known by Him.
4Kwa hiyo, kuhusu vyakula vilivyotambikiwa sanamu, twajua kwamba sanamu si kitu duniani; twajua kwamba Mungu ni mmoja tu.
4Concerning the eating then of the things sacrificed to idols, we have known that an idol [is] nothing in the world, and that there is no other God except one;
5Hata kama viko vitu viitwavyo miungu duniani au mbinguni, na hata kama wako miungu na mabwana wengi,
5for even if there are those called gods, whether in heaven, whether upon earth — as there are gods many and lords many —
6hata hivyo, kwetu sisi yuko Mungu mmoja tu: Baba, Muumba wa vyote, ambaye kwa ajili yake sisi tuko. Pia yuko Bwana mmoja tu, Yesu Kristo, ambaye kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, na sisi twaishi kwa njia yake.
6yet to us [is] one God, the Father, of whom [are] the all things, and we to Him; and one Lord, Jesus Christ, through whom [are] the all things, and we through Him;
7Lakini, si kila mtu anao ujuzi huu. Maana wako watu wengine waliokwisha zoea sanamu, watu ambao mpaka hivi sasa wanapokula vyakula huviona bado kama vyakula vilivyotambikiwa sanamu. Na kwa vile dhamiri zao ni dhaifu, hutiwa unajisi.
7but not in all men [is] the knowledge, and certain with conscience of the idol, till now, as a thing sacrificed to an idol do eat [it], and their conscience, being weak, is defiled.
8Lakini chakula hakiwezi kutupeleka karibu zaidi na Mungu. Tukiacha kukila hatupungukiwi kitu, tukikila hatuongezewi kitu.
8But victuals do not commend us to God, for neither if we may eat are we in advance; nor if we may not eat, are we behind;
9Lakini, jihadharini: huu uhuru wenu usiwafanye walio na imani dhaifu waanguke katika dhambi.
9but see, lest this privilege of yours may become a stumbling-block to the infirm,
10Maana, mtu ambaye dhamiri yake ni dhaifu, akikuona wewe mwenye ujuzi unakula vyakula hivyo ndani ya hekalu la sanamu, je, hatatiwa moyo wa kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu?
10for if any one may see thee that hast knowledge in an idol`s temple reclining at meat — shall not his conscience — he being infirm — be emboldened to eat the things sacrificed to idols,
11Hivyo, huyo ndugu yako dhaifu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake, atapotea kwa sababu ya ujuzi wako.
11and the brother who is infirm shall perish by thy knowledge, because of whom Christ died?
12Kama mkiwakosesha ndugu zenu jinsi hiyo na kuzijeruhi dhamiri zao dhaifu, mtakuwa mmemkosea Kristo.
12and thus sinning in regard to the brethren, and smiting their weak conscience — in regard to Christ ye sin;
13Kwa hiyo, ikiwa chakula husababisha kuanguka kwa ndugu yangu, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi.
13wherefore, if victuals cause my brother to stumble, I may eat no flesh — to the age — that my brother I may not cause to stumble.