Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

1 Thessalonians

3

1Mwishowe hatukuweza kuvumilia zaidi. Basi, tuliamua kubaki kule Athene peke yetu,
1Wherefore no longer forbearing, we thought good to be left in Athens alone,
2na kumtuma kwenu ndugu yetu Timotheo, ambaye ni mfanyakazi mwenzetu kwa ajili ya Mungu katika kuhubiri Habari Njema ya Kristo. Tulimtuma ili awaimarisheni na kuwafarijini,
2and did send Timotheus — our brother, and a ministrant of God, and our fellow-workman in the good news of the Christ — to establish you, and to comfort you concerning your faith,
3kusudi imani ya mtu yeyote miongoni mwenu isije ikafifia kwa sababu ya taabu hizo. Ninyi mnajua kwamba tunapaswa kupata mateso.
3that no one be moved in these tribulations, for yourselves have known that for this we are set,
4Maana, tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwaambieni kwamba tutateswa; na kama mjuavyo ndivyo ilivyotukia.
4for even when we were with you, we said to you beforehand, that we are about to suffer tribulation, as also it did come to pass, and ye have known [it];
5Ndio maana nilimtuma Timotheo kwenu. Sikuweza kungoja zaidi, na hivyo nilimtuma nipate habari za imani yenu. Isije ikawa labda Mshawishi aliwajaribuni na kazi yote tuliyofanya miongoni mwenu imepotea bure!
5because of this also, I, no longer forbearing, did send to know your faith, lest he who is tempting did tempt you, and in vain might be our labour.
6Sasa Timotheo amekwisha rudi, naye ametupa habari za kufurahisha kuhusu imani na upendo wenu. Ametuarifu kwamba mnatukumbuka daima, na kwamba mna hamu ya kutuona sisi kama nasi tulivyo na hamu ya kuwaoneni.
6And now Timotheus having come unto us from you, and having declared good news to us of your faith and love, and that ye have a good remembrance of us always, desiring much to see us, as we also [to see] you,
7Basi, habari za imani yenu zimetutia moyo katika taabu na mateso yetu yote,
7because of this we were comforted, brethren, over you, in all our tribulation and necessity, through your faith,
8kwani sasa tunaishi kweli ikiwa ninyi mnasimama imara katika kuungana na Bwana.
8because now we live, if ye may stand fast in the Lord;
9Sasa twaweza kumshukuru Mungu wetu kwa ajili yenu. Tunamshukuru kwa furaha tuliyo nayo mbele yake kwa sababu yenu.
9for what thanks are we able to recompense to God for you, for all the joy with which we do joy because of you in the presence of our God?
10Tunazidi kumwomba Mungu usiku na mchana kwa moyo wetu wote ili atupatie fursa ya kuwaoneni uso kwa uso ili tuweze kurekebisha chochote kilichopungua katika imani yenu.
10night and day exceedingly beseeching, that we might see your face, and perfect the things lacking in your faith.
11Tunamwomba Mungu, Baba yetu mwenyewe, na Bwana wetu Yesu atutayarishie njia ya kuja kwenu.
11And our God and Father Himself, and our Lord Jesus Christ, direct our way unto you,
12Bwana awawezeshe ninyi kupendana na kuwapenda watu wote zaidi na zaidi, kama vile sisi tunavyowapenda ninyi.
12and you the Lord cause to increase and to abound in the love to one another, and to all, even as we also to you,
13Hivyo ataiimarisha mioyo yenu, nanyi mtakuwa wakamilifu na watakatifu mbele ya Mungu na Baba yetu wakati Bwana wetu Yesu atakapokuja pamoja na wote walio wake.
13to the establishing your hearts blameless in sanctification before our God and Father, in the presence of our Lord Jesus Christ with all His saints.