Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

1 Thessalonians

5

1Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
1And concerning the times and the seasons, brethren, ye have no need of my writing to you,
2Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
2for yourselves have known thoroughly that the day of the Lord as a thief in the night doth so come,
3Watu watakapokuwa wanasema: "Kila kitu ni shwari na salama" ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
3for when they may say, Peace and surety, then sudden destruction doth stand by them, as the travail [doth] her who is with child, and they shall not escape;
4Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
4and ye, brethren, are not in darkness, that the day may catch you as a thief;
5Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
5all ye are sons of light, and sons of day; we are not of night, nor of darkness,
6Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
6so, then, we may not sleep as also the others, but watch and be sober,
7Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
7for those sleeping, by night do sleep, and those making themselves drunk, by night are drunken,
8Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
8and we, being of the day — let us be sober, putting on a breastplate of faith and love, and an helmet — a hope of salvation,
9Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
9because God did not appoint us to anger, but to the acquiring of salvation through our Lord Jesus Christ,
10ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
10who did die for us, that whether we wake — whether we sleep — together with him we may live;
11Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
11wherefore, comfort ye one another, and build ye up, one the one, as also ye do.
12Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
12And we ask you, brethren, to know those labouring among you, and leading you in the Lord, and admonishing you,
13Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
13and to esteem them very abundantly in love, because of their work; be at peace among yourselves;
14Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
14and we exhort you, brethren, admonish the disorderly, comfort the feeble-minded, support the infirm, be patient unto all;
15Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
15see no one evil for evil may render to any one, but always that which is good pursue ye, both to one another and to all;
16Furahini daima,
16always rejoice ye;
17salini kila wakati
17continually pray ye;
18na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
18in every thing give thanks, for this [is] the will of God in Christ Jesus in regard to you.
19Msimpinge Roho Mtakatifu;
19The Spirit quench not;
20msidharau unabii.
20prophesyings despise not;
21Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
21all things prove; that which is good hold fast;
22na epukeni kila aina ya uovu.
22from all appearance of evil abstain ye;
23Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu--roho, mioyo na miili yenu--mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
23and the God of the peace Himself sanctify you wholly, and may your whole spirit, and soul, and body, be preserved unblameably in the presence of our Lord Jesus Christ;
24Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
24stedfast is He who is calling you, who also will do [it].
25Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
25Brethren, pray for us;
26Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
26salute all the brethren in an holy kiss;
27Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
27I charge you [by] the Lord, that the letter be read to all the holy brethren;
28Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
28the grace of our Lord Jesus Christ [is] with you! Amen.