1Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,
1I exhort, then, first of all, there be made supplications, prayers, intercessions, thanksgivings, for all men:
2kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.
2for kings, and all who are in authority, that a quiet and peaceable life we may lead in all piety and gravity,
3Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,
3for this [is] right and acceptable before God our Saviour,
4ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
4who doth will all men to be saved, and to come to the full knowledge of the truth;
5Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,
5for one [is] God, one also [is] mediator of God and of men, the man Christ Jesus,
6ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.
6who did give himself a ransom for all — the testimony in its own times —
7Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
7in regard to which I was set a preacher and apostle — truth I say in Christ, I do not lie — a teacher of nations, in faith and truth.
8Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.
8I wish, therefore, that men pray in every place, lifting up kind hands, apart from anger and reasoning;
9Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
9in like manner also the women, in becoming apparel, with modesty and sobriety to adorn themselves, not in braided hair, or gold, or pearls, or garments of great price,
10bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.
10but — which becometh women professing godly piety — through good works.
11Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
11Let a woman in quietness learn in all subjection,
12Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
12and a woman I do not suffer to teach, nor to rule a husband, but to be in quietness,
13Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
13for Adam was first formed, then Eve,
14Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
14and Adam was not deceived, but the woman, having been deceived, into transgression came,
15Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.
15and she shall be saved through the child-bearing, if they remain in faith, and love, and sanctification, with sobriety.