Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Acts

10

1Kulikuwa na mtu mmoja huko Kaisarea aitwaye Kornelio, Jemadari wa kikosi kimoja kiitwacho "Kikosi cha Italia."
1And there was a certain man in Cesarea, by name Cornelius, a centurion from a band called Italian,
2Alikuwa mtu mwema; naye pamoja na jamaa yake yote walimcha Mungu; alikuwa anafanya mengi kusaidia maskini wa Kiyahudi na alikuwa anasali daima.
2pious, and fearing God with all his house, doing also many kind acts to the people, and beseeching God always,
3Yapata saa tisa mchana, aliona dhahiri katika maono malaika wa Mungu akiingia ndani na kumwambia, "Kornelio!"
3he saw in a vision manifestly, as it were the ninth hour of the day, a messenger of God coming in unto him, and saying to him, `Cornelius;`
4Kornelio alimkodolea macho huyo malaika kwa hofu, akamwambia, "Kuna nini Mheshimiwa?" Huyo malaika akamwambia, "Mungu amezipokea sala na sadaka zako kwa maskini.
4and he having looked earnestly on him, and becoming afraid, said, `What is it, Lord?` And he said to him, `Thy prayers and thy kind acts came up for a memorial before God,
5Sasa, watume watu Yopa wakamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
5and now send men to Joppa, and send for a certain one Simon, who is surnamed Peter,
6Yeye yumo nyumbani kwa Simoni mtengenezaji wa ngozi ambaye nyumba yake iko karibu na bahari."
6this one doth lodge with a certain Simon a tanner, whose house is by the sea; this one shall speak to thee what it behoveth thee to do.`
7Huyo malaika aliyesema hayo alipokwisha kwenda zake, Kornelio aliwaita watumishi wawili wa nyumbani na mmoja wa askari zake ambaye alikuwa mcha Mungu,
7And when the messenger who is speaking to Cornelius went away, having called two of his domestics, and a pious soldier of those waiting on him continually,
8akawaeleza yote yaliyotukia, akawatuma Yopa.
8and having declared to them all things, he sent them to Joppa.
9Kesho yake, hao watu watatu wakiwa bado safarini, lakini karibu kufika Yopa, Petro alipanda juu ya paa la nyumba yapata saa sita mchana ili kusali.
9And on the morrow, as these are proceeding on the way, and are drawing nigh to the city, Peter went up upon the house-top to pray, about the sixth hour,
10Aliona njaa, akatamani kupata chakula. Chakula kilipokuwa kinatayarishwa, alipatwa na usingizi mzito akaona maono.
10and he became very hungry, and wished to eat; and they making ready, there fell upon him a trance,
11Aliona mbingu zimefunguliwa na kitu kama shuka kubwa inateremshwa chini ikiwa imeshikwa pembe zake nne.
11and he doth behold the heaven opened, and descending unto him a certain vessel, as a great sheet, bound at the four corners, and let down upon the earth,
12Ndani ya shuka hiyo kulikuwa na kila aina ya wanyama: wanyama wenye miguu minne, wanyama watambaao na ndege wa angani.
12in which were all the four-footed beasts of the earth, and the wild beasts, and the creeping things, and the fowls of the heaven,
13Akasikia sauti ikimwambia: "Petro, amka uchinje, ule!"
13and there came a voice unto him: `Having risen, Peter, slay and eat.`
14Petro akajibu, "La, Bwana; mimi sijaonja kamwe chochote ambacho ni najisi au kichafu."
14And Peter said, `Not so, Lord; because at no time did I eat anything common or unclean;`
15Ile sauti ikasikika tena ikimwambia: "Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa!"
15and [there is] a voice again a second time unto him: `What God did cleanse, thou, declare not thou common;`
16Jambo hili lilifanyika mara tatu, kisha ile shuka ikarudishwa juu mbinguni.
16and this was done thrice, and again was the vessel received up to the heaven.
17Petro alipokuwa bado anashangaa juu ya maana ya hilo maono alilokuwa ameliona, wale watu waliotumwa na Kornelio, baada ya kuigundua nyumba ya Simoni, walifika mlangoni,
17And as Peter was perplexed in himself what the vision that he saw might be, then, lo, the men who have been sent from Cornelius, having made inquiry for the house of Simon, stood at the gate,
18Wakaita kwa sauti: "Je, kuna mgeni humu aitwaye Simoni Petro?"
18and having called, they were asking if Simon, who is surnamed Peter, doth lodge here?
19Petro alikuwa bado anajaribu kuelewa lile maono, na hapo Roho akamwambia, "Sikiliza! kuna watu watatu hapa, wanakutafuta.
19And Peter thinking about the vision, the Spirit said to him, `Lo, three men do seek thee;
20Shuka upesi na wala usisite kwenda pamoja nao kwa maana ni mimi niliyewatuma."
20but having risen, go down and go on with them, nothing doubting, because I have sent them;`
21Basi, Petro akateremka chini, akawaambia hao watu, "Mimi ndiye mnayemtafuta. Kwa nini mmekuja?"
21and Peter having come down unto the men who have been sent from Cornelius unto him, said, `Lo, I am he whom ye seek, what [is] the cause for which ye are present?`
22Wao wakamjibu, "Jemadari Kornelio ambaye ni mtu mwema, mcha Mungu na mwenye kuheshimika mbele ya Wayahudi wote ametutuma. Aliambiwa na malaika mtakatifu akualike nyumbani kwake ili asikilize chochote ulicho nacho cha kusema."
22And they said, `Cornelius, a centurion, a man righteous and fearing God, well testified to, also, by all the nation of the Jews, was divinely warned by a holy messenger to send for thee, to his house, and to hear sayings from thee.`
23Petro akawaalika ndani, akawapa mahali pa kulala usiku ule. Kesho yake, Petro alianza safari pamoja nao, na baadhi ya ndugu wa huko Yopa walifuatana naye.
23Having called them in, therefore, he lodged them, and on the morrow Peter went forth with them, and certain of the brethren from Joppa went with him,
24Siku ya pili yake, walifika Kaisarea na huko Kornelio alikuwa anawangojea pamoja na jamaa na marafiki aliokuwa amewaalika.
24and on the morrow they did enter into Cesarea; and Cornelius was waiting for them, having called together his kindred and near friends,
25Petro alipokuwa anaingia, Kornelio alitoka nje kumlaki, akapiga magoti mbele yake na kuinama chini kabisa.
25and as it came that Peter entered in, Cornelius having met him, having fallen at [his] feet, did bow before [him];
26Lakini Petro alimwinua, akamwambia, "Simama, kwa maana mimi ni binadamu tu."
26and Peter raised him, saying, `Stand up; I also myself am a man;`
27Petro aliendelea kuongea na Kornelio wakiwa wanaingia nyumbani ambamo aliwakuta watu wengi wamekusanyika.
27and talking with him he went in, and doth find many having come together.
28Petro akawaambia, "Ninyi wenyewe mnajua kwamba Myahudi yeyote amekatazwa na Sheria yake ya dini kushirikiana na watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amenijulisha nisimfikirie mtu yeyote kuwa najisi au mchafu.
28And he said unto them, `Ye know how it is unlawful for a man, a Jew, to keep company with, or to come unto, one of another race, but to me God did shew to call no man common or unclean;
29Kwa sababu hiyo, mliponiita nimekuja bila kusita. Basi, nawaulizeni: kwa nini mmeniita?"
29therefore also without gainsaying I came, having been sent for; I ask, therefore, for what matter ye did send for me?`
30Kornelio akasema, "Siku tatu zilizopita saa kama hii, saa tisa alasiri, nilikuwa nikisali chumbani mwangu. Ghafla, mtu aliyekuwa amevaa mavazi yenye kun'gaa alisimama mbele yangu,
30And Cornelius said, `Four days ago till this hour, I was fasting, and [at] the ninth hour praying in my house, and, lo, a man stood before me in bright clothing,
31akasema: Kornelio! Sala yako na sadaka zako kwa maskini vimekubaliwa na Mungu.
31and he said, Cornelius, thy prayer was heard, and thy kind acts were remembered before God;
32Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petroi; yuko nyumbani kwa Simoni mtengenezaji wa ngozi karibu na bahari.
32send, therefore, to Joppa, and call for Simon, who is surnamed Peter; this one doth lodge in the house of Simon a tanner, by the sea, who having come, shall speak to thee;
33Kwa hiyo nilikutumia ujumbe bila kuchelewa, nawe umefanya vyema kuja. Sasa, sisi tuko mbele ya Mungu, kusikiliza chochote ambacho bwana amekuamuru kusema."
33at once, therefore, I sent to thee; thou also didst do well, having come; now, therefore, are we all before God present to hear all things that have been commanded thee by God.`
34Hapo Petro akaanza kusema: "Sasa nimetambua kwamba hakika Mungu hana ubaguzi.
34And Peter having opened his mouth, said, `Of a truth, I perceive that God is no respecter of persons,
35Mtu wa taifa lolote anayemcha Mungu na kutenda haki anapokelewa naye.
35but in every nation he who is fearing Him, and is working righteousness, is acceptable to Him;
36Huu ndio ule ujumbe Mungu alioupeleka kwa watu wa Israeli, akitangaza Habari Njema iletayo amani kwa njia ya Yesu Kristo ambaye ni Bwana wa wote.
36the word that he sent to the sons of Israel, proclaiming good news — peace through Jesus Christ (this one is Lord of all,)
37Ninyi mnajua jambo lililotukia katika nchi yote ya Wayahudi kuanzia Galilaya baada ya ule ubatizo aliohubiri Yohane.
37ye — ye have known; — the word that came throughout all Judea, having begun from Galilee, after the baptism that John preached;
38Mnajua Yesu wa Nazareti na jinsi Mungu alivyomteua kwa kummiminia Roho Mtakatifu na nguvu. Mungu alikuwa pamoja naye; yeye alikwenda huko na huko akitenda mema na kuwaponya wote waliokuwa wamevamiwa na Ibilisi.
38Jesus who [is] from Nazareth — how God did anoint him with the Holy Spirit and power; who went through, doing good, and healing all those oppressed by the devil, because God was with him;
39Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyotenda katika nchi ya Wayahudi na katika Yerusalemu. Walimuua kwa kumtundika msalabani;
39and we — we are witnesses of all things that he did, both in the country of the Jews, and in Jerusalem, — whom they did slay, having hanged upon a tree.
40lakini Mungu alimfufua siku ya tatu, akamfanya aonekane
40`This one God did raise up the third day, and gave him to become manifest,
41si kwa watu wote ila kwa wale Mungu aliokwisha wachagua wawe mashahidi wake, yaani sisi tuliokula na kunywa pamoja naye baada ya kufufuka kwake kutoka wafu.
41not to all the people, but to witnesses, to those having been chosen before by God — to us who did eat with [him], and did drink with him, after his rising out of the dead;
42Alituamuru kuihubiri Habari Njema kwa watu wote na kushuhudia kwamba yeye ndiye aliyeteuliwa na Mungu awe Mwamuzi wa wazima na wafu.
42and he commanded us to preach to the people, and to testify fully that it is he who hath been ordained by God judge of living and dead —
43Manabii wote waliongea juu yake kwamba kila mtu atakayemwamini atasamehewa dhambi zake zote kwa jina lake."
43to this one do all the prophets testify, that through his name every one that is believing in him doth receive remission of sins.`
44Wakati Petro alipokuwa bado anasema maneno hayo, Roho Mtakatifu aliwashukia wote waliokuwa wanasikiliza ujumbe huo.
44While Peter is yet speaking these sayings, the Holy spirit fell upon all those hearing the word,
45Wale Wayahudi waumini waliokuja pamoja na Petro kutoka Yopa walishangaa kuona kuwa Mungu aliwamiminia zawadi ya Roho Mtakatifu watu wa mataifa mengine pia;
45and those of the circumcision believing were astonished — as many as came with Peter — because also upon the nations the gift of the Holy Spirit hath been poured out,
46maana waliwasikia wakiongea kwa lugha mbalimbali wakimtukuza Mungu. Hapo Petro akasema,
46for they were hearing them speaking with tongues and magnifying God.
47"Watu hawa wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi wenyewe tulivyompokea. Je, kuna yeyote atakayeweza kuwazuia wasibatizwe kwa maji?"
47Then answered Peter, `The water is any one able to forbid, that these may not be baptized, who the Holy Spirit did receive — even as also we?`
48Basi, akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Kisha wakamwomba akae nao kwa siku chache.
48he commanded them also to be baptized in the name of the Lord; then they besought him to remain certain days.