Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Acts

20

1Ile ghasia ya Efeso ilipokwisha tulia Paulo aliwaita pamoja wale waumini, akawatia moyo. Kisha akawaaga, akasafiri kwenda Makedonia.
1And after the ceasing of the tumult, Paul having called near the disciples, and having embraced [them], went forth to go on to Macedonia;
2Alipitia sehemu za nchi zile akiwatia watu moyo kwa maneno mengi. Halafu akafika Ugiriki.
2and having gone through those parts, and having exhorted them with many words, he came to Greece;
3ambako alikaa kwa miezi mitatu. Alipokuwa anajitayarisha kwenda Siria, aligundua kwamba Wayahudi walikuwa wanamfanyia mpango mbaya; hivyo aliamua kurudi kwa kupitia Makedonia.
3having made also three months` [stay] — a counsel of the Jews having been against him — being about to set forth to Syria, there came [to him] a resolution of returning through Macedonia.
4Sopatro, mwana wa Pirho kutoka Berea, aliandamana naye; pia Aristarko na Sekundo kutoka Thesalonika, Gayo kutoka Derbe, Timotheo, Tukiko na Trofimo wa mkoa wa Asia.
4And there were accompanying him unto Asia, Sopater of Berea, and of Thessalonians Aristarchus and Secundus, and Gaius of Derbe, and Timotheus, and of Asiatics Tychicus and Trophimus;
5Hao walitutangulia na kutungojea kule Troa.
5these, having gone before, did remain for us in Troas,
6Sisi, baada ya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, tulipanda meli kutoka Filipi na baada ya siku tatu tukawafikia kule Troa. Huko tulikaa kwa muda wa juma moja.
6and we sailed, after the days of the unleavened food, from Philippi, and came unto them to Troas in five days, where we abode seven days.
7Jumamosi jioni, tulikutana ili kumega mkate. Kwa vile Paulo alikuwa amekusudia kuondoka kesho yake, aliwahutubia watu na kuendelea kuongea nao hadi usiku wa manane.
7And on the first of the week, the disciples having been gathered together to break bread, Paul was discoursing to them, about to depart on the morrow, he was also continuing the discourse till midnight,
8Katika chumba tulimokuwa, ghorofani, kulikuwa na taa nyingi zinawaka.
8and there were many lamps in the upper chamber where they were gathered together,
9Kijana mmoja aitwaye Eutuko alikuwa ameketi dirishani wakati Paulo alipokuwa anaendelea kuhutubu. Eutuko alianza kusinzia kidogokidogo na hatimaye usingizi ukambana, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu. Wakamwokota amekwisha kufa.
9and there was sitting a certain youth, by name Eutychus, upon the window — being borne down by a deep sleep, Paul discoursing long — he having sunk down from the sleep, fell down from the third story, and was lifted up dead.
10Lakini Paulo alishuka chini, akainama, akamkumbatia na kusema, "Msiwe na wasiwasi maana kuna uhai bado ndani yake."
10And Paul, having gone down, fell upon him, and having embraced [him], said, `Make no tumult, for his life is in him;`
11Kisha akapanda tena ghorofani, akamega mkate, akala. Aliendelea kuhubiri kwa muda mrefu hadi alfajiri, halafu akaondoka.
11and having come up, and having broken bread, and having tasted, for a long time also having talked — till daylight, so he went forth,
12Wale watu walimchukua yule kijana nyumbani akiwa mzima kabisa, wakapata kitulizo kikubwa.
12and they brought up the lad alive, and were comforted in no ordinary measure.
13Sisi tulipanda meli tukatangulia kwenda Aso ambako tungemchukua Paulo. Ndivyo alivyopanga; maana alitaka kufika huko kwa kupitia nchi kavu.
13And we having gone before unto the ship, did sail to Assos, thence intending to take in Paul, for so he had arranged, intending himself to go on foot;
14Basi, alitukuta kule Aso, tukampandisha melini, tukaenda Mitulene.
14and when he met with us at Assos, having taken him up, we came to Mitylene,
15Kutoka huko tulisafiri tukafika Kio kesho yake. Siku ya pili, tulitia nanga Samo na kesho yake tukafika Mileto.
15and thence having sailed, on the morrow we came over-against Chios, and the next day we arrived at Samos, and having remained in Trogyllium, on the following day we came to Miletus,
16Paulo alikuwa amekusudia kuendelea na safari kwa meli bila kupitia Efeso ili asikawie zaidi huko Asia. Alikuwa na haraka ya kufika Yerusalemu kwa sikukuu ya Pentekoste kama ingewezekana.
16for Paul decided to sail past Ephesus, that there may not be to him a loss of time in Asia, for he hasted, if it were possible for him, on the day of the Pentecost to be at Jerusalem.
17Kutoka Mileto Paulo alituma ujumbe kwa wazee wa Efeso wakutane naye.
17And from Miletus, having sent to Ephesus, he called for the elders of the assembly,
18Walipofika kwake aliwaambia, "Mnajua jinsi nilivyotumia wakati wote pamoja nanyi tangu siku ile ya kwanza nilipofika Asia.
18and when they were come unto him, he said to them, `Ye — ye know from the first day in which I came to Asia, how, with you at all times I was;
19Mnajua jinsi nilivyomtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote, kwa machozi na matatizo yaliyonipata kutokana na mipango ya hila ya Wayahudi.
19serving the Lord with all humility, and many tears, and temptations, that befell me in the counsels of the Jews against [me];
20Mnajua kwamba sikusita hata kidogo kuwahubiria hadharani na nyumbani mwenu na kuwafundisha chochote ambacho kingewasaidieni.
20how nothing I did keep back of what things are profitable, not to declare to you, and to teach you publicly, and in every house,
21Niliwaonya wote--Wayahudi kadhalika na watu wa mataifa, wamgeukie Mungu na kumwamini Bwana wetu Yesu.
21testifying fully both to Jews and Greeks, toward God reformation, and faith toward our Lord Jesus Christ.
22Sasa, sikilizeni! Mimi, nikiwa ninamtii Roho, nakwenda Yerusalemu bila kufahamu yatakayonipata huko.
22`And now, lo, I — bound in the Spirit — go on to Jerusalem, the things that shall befall me in it not knowing,
23Ninachojua tu ni kwamba Roho Mtakatifu ananithibitishia katika kila mji kwamba vifungo na mateso ndivyo vinavyoningojea.
23save that the Holy Spirit in every city doth testify fully, saying, that for me bonds and tribulations remain;
24Lakini, siuthamini uhai wangu kuwa ni kitu sana kwangu. Nataka tu nikamilishe ule utume wangu na kumaliza ile kazi aliyonipa Bwana Yesu niifanye, yaani nitangaze Habari Njema ya neema ya Mungu.
24but I make account of none of these, neither do I count my life precious to myself, so that I finish my course with joy, and the ministration that I received from the Lord Jesus, to testify fully the good news of the grace of God.
25"Nimekuwa nikienda huko na huko kati yenu nikiuhubiri Ufalme wa Mungu. Sasa lakini, najua hakuna hata mmoja wenu atakayeniona tena.
25`And now, lo, I have known that no more shall ye see my face, — ye all among whom I did go preaching the reign of God;
26Hivyo, leo hii ninawathibitishieni rasmi kwamba ikijatokea akapotea mmoja wenu, mimi sina lawama yoyote.
26wherefore I take you to witness this day, that I [am] clear from the blood of all,
27Kwa maana sikusita hata kidogo kuwatangazieni azimio lote la Mungu.
27for I did not keep back from declaring to you all the counsel of God.
28Jihadharini wenyewe; lilindeni lile kundi ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi muwe walezi wake. Lichungeni kanisa la Mungu ambalo amejipatia kwa damu ya Mwanae.
28`Take heed, therefore, to yourselves, and to all the flock, among which the Holy Spirit made you overseers, to feed the assembly of God that He acquired through His own blood,
29Nafahamu vizuri sana kwamba baada ya kuondoka kwangu mbwa mwitu wakali watawavamieni, na hawatakuwa na huruma kwa kundi hilo.
29for I have known this, that there shall enter in, after my departing, grievous wolves unto you, not sparing the flock,
30Hata kutoka miongoni mwenu watatokea watu ambao watasema mambo ya uongo ili kuwapotosha watu na kuwafanya wawafuate wao tu.
30and of your own selves there shall arise men, speaking perverse things, to draw away the disciples after them.
31Kwa hiyo, muwe macho mkikumbuka kwamba kwa muda wa miaka mitatu, usiku na mchana, sikuchoka kumwonya kila mmoja wenu kwa machozi.
31`Therefore, watch, remembering that three years, night and day, I did not cease with tears warning each one;
32"Na sasa basi, ninawaweka ninyi chini ya ulinzi wa Mungu na ujumbe wa neema yake. Yeye anao uwezo wa kuwajenga ninyi na kuwawezesha mzipate zile baraka alizowawekea watu wake.
32and now, I commend you, brethren, to God, and to the word of His grace, that is able to build up, and to give you an inheritance among all those sanctified.
33Mimi sikutamani hata mara moja fedha, wala dhahabu, wala nguo za mtu yeyote.
33`The silver or gold or garments of no one did I covet;
34Mnajua ninyi wenyewe kwamba nimefanya kazi kwa mikono yangu mwenyewe, ili kujipatia mahitaji yangu na ya wenzangu.
34and ye yourselves know that to my necessities, and to those who were with me, minister did these hands;
35Nimekuwa nikiwapeni daima mfano kwamba kwa kufanya kazi mithili hiyo tunapaswa kuwasaidia walio dhaifu, tukikumbuka maneno ya Bwana Yesu mwenyewe: Heri zaidi kutoa kuliko kupokea."
35all things I did shew you, that, thus labouring, it behoveth [us] to partake with the ailing, to be mindful also of the words of the Lord Jesus, that he himself said, It is more blessed to give than to receive.`
36Baada ya kusema hayo, Paulo alipiga magoti pamoja nao wote, akasali.
36And these things having said, having bowed his knees, with them all, he did pray,
37Wote walikuwa wanalia; wakamwaga kwa kumkumbatia na kumbusu.
37and there came a great weeping to all, and having fallen upon the neck of Paul, they were kissing him,
38Jambo lililowahuzunisha zaidi lilikuwa neno alilosema kwamba hawangemwona tena. Basi, wakamsindikiza hadi melini.
38sorrowing most of all for the word that he had said — that they are about no more to see his face; and they were accompanying him to the ship.