Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Acts

27

1Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho "Kikosi cha Augusto."
1And when our sailing to Italy was determined, they were delivering up both Paul and certain others, prisoners, to a centurion, by name Julius, of the band of Sebastus,
2Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonika, alikuwa pamoja nasi.
2and having embarked in a ship of Adramyttium, we, being about to sail by the coasts of Asia, did set sail, there being with us Aristarchus, a Macedonian of Thessalonica,
3Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
3on the next [day] also we touched at Sidon, and Julius, courteously treating Paul, did permit [him], having gone on unto friends, to receive [their] care.
4Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi.
4And thence, having set sail, we sailed under Cyprus, because of the winds being contrary,
5Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
5and having sailed over the sea over-against Cilicia and Pamphylia, we came to Myria of Lycia,
6Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani.
6and there the centurion having found a ship of Alexandria, sailing to Italy, did put us into it,
7Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
7and having sailed slowly many days, and with difficulty coming over-against Cnidus, the wind not suffering us, we sailed under Crete, over-against Salmone,
8Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo "Bandari Nzuri", karibu na mji wa Lasea.
8and hardly passing it, we came to a certain place called `Fair Havens,` nigh to which was the city [of] Lasaea.
9Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo:
9And much time being spent, and the sailing being now dangerous — because of the fast also being already past — Paul was admonishing,
10"Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu."
10saying to them, `Men, I perceive that with hurt, and much damage, not only of the lading and of the ship, but also of our lives — the voyage is about to be;`
11Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
11but the centurion to the pilot and to the shipowner gave credence more than to the things spoken by Paul;
12Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
12and the haven being incommodious to winter in, the more part gave counsel to sail thence also, if by any means they might be able, having attained to Phenice, [there] to winter, [which is] a haven of Crete, looking to the south-west and north-west,
13Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakang'oa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete.
13and a south wind blowing softly, having thought they had obtained [their] purpose, having lifted anchor, they sailed close by Crete,
14Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao "Upepo wa Kaskazi" ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
14and not long after there arose against it a tempestuous wind, that is called Euroclydon,
15Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo.
15and the ship being caught, and not being able to bear up against the wind, having given [her] up, we were borne on,
16Kisiwa kimoja kiitwacho Kanda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
16and having run under a certain little isle, called Clauda, we were hardly able to become masters of the boat,
17Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libya. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
17which having taken up, they were using helps, undergirding the ship, and fearing lest they may fall on the quicksand, having let down the mast — so were borne on.
18Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli.
18And we, being exceedingly tempest-tossed, the succeeding [day] they were making a clearing,
19Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
19and on the third [day] with our own hands the tackling of the ship we cast out,
20Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
20and neither sun nor stars appearing for more days, and not a little tempest lying upon us, thenceforth all hope was taken away of our being saved.
21Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, "Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
21And there having been long fasting, then Paul having stood in the midst of them, said, `It behoved [you], indeed, O men — having hearkened to me — not to set sail from Crete, and to save this hurt and damage;
22Lakini sasa ninawaombeni muwe na moyo; hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake; meli tu ndiyo itakayopotea.
22and now I exhort you to be of good cheer, for there shall be no loss of life among you — but of the ship;
23Kwa maana jana usiku malaika wa yule Mungu ambaye mimi ni wake na ambaye mimi ninamwabudu alinitokea,
23for there stood by me this night a messenger of God — whose I am, and whom I serve —
24akaniambia: Paulo usiogope! Ni lazima utasimama mbele ya Kaisari; naye Mungu, kwa wema wake, amekufadhili kwa kuwaokoa wote wanaosafiri nawe wasiangamie.
24saying, Be not afraid Paul; before Caesar it behoveth thee to stand; and, lo, God hath granted to thee all those sailing with thee;
25Hivyo, waheshimiwa, jipeni moyo! Maana ninamwamini Mungu kwamba itakuwa sawa kama nilivyoambiwa.
25wherefore be of good cheer, men! for I believe God, that so it shall be, even as it hath been spoken to me,
26Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani."
26and on a certain island it behoveth us to be cast.`
27Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huku katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
27And when the fourteenth night came — we being borne up and down in the Adria — toward the middle of the night the sailors were supposing that some country drew nigh to them;
28Hivyo walitafuta kina cha bahari kwa kuteremsha kamba iliyokuwa imefungiwa kitu kizito, wakapata kina cha mita arobaini. Baadaye wakapima tena wakapata mita thelathini.
28and having sounded they found twenty fathoms, and having gone a little farther, and again having sounded, they found fifteen fathoms,
29Kwa sababu ya kuogopa kukwama kwenye miamba, waliteremsha nanga nne nyuma ya meli; wakaomba kuche upesi.
29and fearing lest on rough places we may fall, out of the stern having cast four anchors, they were wishing day to come.
30Wanamaji walitaka kutoroka, na walikwisha kuteremsha ule mtumbwi majini, wakijisingizia kwamba wanakwenda kuteremsha nanga upande wa mbele wa meli.
30And the sailors seeking to flee out of the ship, and having let down the boat to the sea, in pretence as [if] out of the foreship they are about to cast anchors,
31Lakini Paulo alimwambia yule ofisa wa jeshi na askari wake, "Kama wanamaji hawa hawabaki ndani ya meli, hamtaokoka."
31Paul said to the centurion and to the soldiers, `If these do not remain in the ship — ye are not able to be saved;`
32Hapo wale askari walizikata kamba zilizokuwa zimeshikilia ule mtumbwi, wakauacha uchukuliwe na maji.
32then the soldiers did cut off the ropes of the boat, and suffered it to fall off.
33Karibu na alfajiri, Paulo aliwahimiza wote wale chakula: "Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika mashaka na bila kula; hamjala kitu chochote.
33And till the day was about to be, Paul was calling upon all to partake of nourishment, saying, `Fourteen days to-day, waiting, ye continue fasting, having taken nothing,
34Basi, ninawasihi mle chakula kwa maana mnakihitaji ili mweze kuendelea kuishi. Maana hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea."
34wherefore I call upon you to take nourishment, for this is for your safety, for of not one of you shall a hair from the head fall;`
35Baada ya kusema hivyo, Paulo alichukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, akaanza kula.
35and having said these things, and having taken bread, he gave thanks to God before all, and having broken [it], he began to eat;
36Hapo wote wakapata moyo, nao pia wakala chakula.
36and all having become of good cheer, themselves also took food,
37Jumla tulikuwa watu mia mbili na sabini na sita katika meli.
37(and we were — all the souls in the ship — two hundred, seventy and six),
38Baada ya kila mmoja kula chakula cha kutosha, walipunguza uzito wa meli kwa kutupa nafaka baharini.
38and having eaten sufficient nourishment, they were lightening the ship, casting forth the wheat into the sea.
39Kulipokucha, wanamaji hawakuweza kuitambua nchi ile, ila waliona ghuba moja yenye ufuko; wakaamua kutia nanga huko kama ikiwezekana.
39And when the day came, they were not discerning the land, but a certain creek were perceiving having a beach, into which they took counsel, if possible, to thrust forward the ship,
40Hivyo walikata nanga na kuziacha baharini, na wakati huohuo wakazifungua kamba zilizokuwa zimeufunga usukani, kisha wakatweka tanga moja mbele kushika upepo, wakaelekea ufukoni.
40and the anchors having taken up, they were committing [it] to the sea, at the same time — having loosed the bands of the rudders, and having hoisted up the mainsail to the wind — they were making for the shore,
41Lakini walifika mahali ambapo mikondo miwili ya bahari hukutana, na meli ikakwama. Sehemu ya mbele ilikuwa imezama mchangani bila kutikisika. Sehemu ya nyuma ya meli ilianza kuvunjika vipandevipande kwa mapigo ya nguvu ya mawimbi.
41and having fallen into a place of two seas, they ran the ship aground, and the fore-part, indeed, having stuck fast, did remain immoveable, but the hinder-part was broken by the violence of the waves.
42Askari walitaka kuwaua wafungwa wote kwa kuogopa kwamba wangeogelea hadi pwani na kutoroka.
42And the soldiers` counsel was that they should kill the prisoners, lest any one having swam out should escape,
43Lakini kwa vile yule ofisajeshi alitaka kumwokoa Paulo, aliwazuia wasifanye hivyo. Aliamuru wale waliojua kuogelea waruke kutoka melini na kuogelea hadi pwani,
43but the centurion, wishing to save Paul, hindered them from the counsel, and did command those able to swim, having cast themselves out first — to get unto the land,
44na wengine wafuate wakijishikilia kwenye mbao au kwenye vipande vya meli iliyovunjika. Ndivyo sisi sote tulivyofika salama pwani.
44and the rest, some indeed upon boards, and some upon certain things of the ship; and thus it came to pass that all came safe unto the land.