1Kutokana na hayo, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, namwomba Mungu.
1For this cause, I Paul, the prisoner of Christ Jesus for you the nations,
2Bila shaka mmekwisha sikia kwamba Mungu, kwa neema yake, alinikabidhi kazi hii niifanye kwa faida yenu.
2if, indeed, ye did hear of the dispensation of the grace of God that was given to me in regard to you,
3Mimi nilijulishwa kwa njia ya ufunuo mpango wake uliofichika. (Nimeandika kwa ufupi juu ya jambo hili,
3that by revelation He made known to me the secret, according as I wrote before in few [words] —
4nanyi mkiyasoma maneno yangu mtaweza kujua jinsi ninavyoielewa siri hiyo ya Kristo.)
4in regard to which ye are able, reading [it], to understand my knowledge in the secret of the Christ,
5Zamani watu hawakujulishwa siri hiyo; lakini sasa Mungu amewajulisha mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho.
5which in other generations was not made known to the sons of men, as it was now revealed to His holy apostles and prophets in the Spirit —
6Siri yenyewe ni hii: kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapata sehemu yao pamoja na Wayahudi katika zile baraka za Mungu; wao ni viungo vya mwili uleule, na wanashiriki ahadi ileile aliyofanya Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
6that the nations be fellow-heirs, and of the same body, and partakers of His promise in the Christ, through the good news,
7Mimi nimefanywa kuwa mtumishi wa Habari Njema kwa neema ya pekee aliyonijalia Mungu kwa uwezo wake mkuu.
7of which I became a ministrant, according to the gift of the grace of God that was given to me, according to the working of His power;
8Mimi ni mdogo kuliko watu wote wa Mungu; lakini amenijalia neema yake, ili niwahubirie watu wa mataifa utajiri wake Kristo usiopimika,
8to me — the less than the least of all the saints — was given this grace, among the nations to proclaim good news — the untraceable riches of the Christ,
9tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele,
9and to cause all to see what [is] the fellowship of the secret that hath been hid from the ages in God, who the all things did create by Jesus Christ,
10kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi.
10that there might be made known now to the principalities and the authorities in the heavenly [places], through the assembly, the manifold wisdom of God,
11Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
11according to a purpose of the ages, which He made in Christ Jesus our Lord,
12Basi, katika kuungana na Kristo, na kwa njia ya imani katika Kristo, sisi tunathubutu kumkaribia Mungu kwa uhodari.
12in whom we have the freedom and the access in confidence through the faith of him,
13Kwa hiyo, nawaombeni msife moyo kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, maana hayo ni kwa ajili ya utukufu wenu.
13wherefore, I ask [you] not to faint in my tribulations for you, which is your glory.
14Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,
14For this cause I bow my knees unto the Father of our Lord Jesus Christ,
15aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni.
15of whom the whole family in the heavens and on earth is named,
16Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu,
16that He may give to you, according to the riches of His glory, with might to be strengthened through His Spirit, in regard to the inner man,
17naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo
17that the Christ may dwell through the faith in your hearts, in love having been rooted and founded,
18kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina.
18that ye may be in strength to comprehend, with all the saints, what [is] the breadth, and length, and depth, and height,
19Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
19to know also the love of the Christ that is exceeding the knowledge, that ye may be filled — to all the fulness of God;
20Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu, aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;
20and to Him who is able above all things to do exceeding abundantly what we ask or think, according to the power that is working in us,
21kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina.
21to Him [is] the glory in the assembly in Christ Jesus, to all the generations of the age of the ages. Amen.