1Mimi Paulo mtume,
1Paul, an apostle — not from men, nor through man, but through Jesus Christ, and God the Father, who did raise him out of the dead —
2na ndugu wote walio pamoja nami, tunayaandikia makanisa yaliyoko Galatia. Mimi nimepata kuwa mtume si kutokana na mamlaka ya binadamu, wala si kwa nguvu ya mtu, bali kwa uwezo wa Yesu Kristo na wa Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka wafu.
2and all the brethren with me, to the assemblies of Galatia:
3Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
3Grace to you, and peace from God the Father, and our Lord Jesus Christ,
4Kristo alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba, ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu mbaya wa sasa.
4who did give himself for our sins, that he might deliver us out of the present evil age, according to the will of God even our Father,
5Kwake yeye uwe utukufu milele! Amina.
5to whom [is] the glory to the ages of the ages. Amen.
6Nashangaa kwamba muda mfupi tu umepita, nanyi mnamwasi yule aliyewaita kwa neema ya Kristo, mkafuata Habari Njema ya namna nyingine.
6I wonder that ye are so quickly removed from Him who did call you in the grace of Christ to another good news;
7Lakini hakuna "Habari Njema" nyingine. Ukweli ni kwamba wako watu wanaowavurugeni, watu wanaotaka kuipotosha Habari Njema ya Kristo.
7that is not another, except there be certain who are troubling you, and wishing to pervert the good news of the Christ;
8Lakini, hata kama mmoja wetu au malaika kutoka mbinguni, atawahubirieni Habari Njema tofauti na ile tuliyowahubirieni sisi, basi huyo na alaaniwe!
8but even if we or a messenger out of heaven may proclaim good news to you different from what we did proclaim to you — anathema let him be!
9Tulikwisha sema, na sasa nasema tena: kama mtu yeyote anawahubirieni Habari Njema ya aina nyingine, tofauti na ile mliyokwisha pokea, huyo na alaaniwe!
9as we have said before, and now say again, If any one to you may proclaim good news different from what ye did receive — anathema let him be!
10Sasa nataka kibali cha nani: cha binadamu, ama cha Mungu? Au je, nataka kuwapendeza watu? Kama ningefanya hivyo, mimi singekuwa kamwe mtumishi wa Kristo.
10for now men do I persuade, or God? or do I seek to please men? for if yet men I did please — Christ`s servant I should not be.
11Ndugu, napenda mfahamu kwamba ile Habari Njema niliyoihubiri si ujumbe wa kibinadamu.
11And I make known to you, brethren, the good news that were proclaimed by me, that it is not according to man,
12Wala mimi sikuipokea kutoka kwa binadamu, wala sikufundishwa na mtu. Yesu Kristo mwenyewe ndiye aliyenifunulia.
12for neither did I from man receive it, nor was I taught [it], but through a revelation of Jesus Christ,
13Bila shaka mlikwisha sikia jinsi nilivyokuwa ninaishi zamani kwa kuzingatia dini ya Kiyahudi, na jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kupita kiasi na kutaka kuliharibu kabisa.
13for ye did hear of my behaviour once in Judaism, that exceedingly I was persecuting the assembly of God, and wasting it,
14Naam, mimi niliwashinda wengi wa wananchi wenzangu wa rika langu katika kuizingatia dini ya Kiyahudi, nikajitahidi sana kuyashika mapokeo ya wazee wetu.
14and I was advancing in Judaism above many equals in age in mine own race, being more abundantly zealous of my fathers` deliverances,
15Lakini Mungu, kwa neema yake, alikuwa ameniteua hata kabla sijazaliwa, akaniita nimtumikie.
15and when God was well pleased — having separated me from the womb of my mother, and having called [me] through His grace —
16Mara tu alipoamua kunifunulia Mwanae kusudi niihubiri Habari Njema yake kwa watu wa mataifa mengine, bila kutafuta maoni ya binadamu,
16to reveal His Son in me, that I might proclaim him good news among the nations, immediately I conferred not with flesh and blood,
17na bila kwenda kwanza Yerusalemu kwa wale waliopata kuwa mitume kabla yangu, nilikwenda kwanza Arabia, kisha nikarudi tena Damasko.
17nor did I go up to Jerusalem unto those who were apostles before me, but I went away to Arabia, and again returned to Damascus,
18Ilikuwa tu baada ya miaka mitatu, ndipo nilipokwenda Yerusalemu kuonana na Kefa; nilikaa kwake siku kumi na tano.
18then, after three years I went up to Jerusalem to enquire about Peter, and remained with him fifteen days,
19Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
19and other of the apostles I did not see, except James, the brother of the Lord.
20Haya ninayowaandikieni, Mungu anajua; sisemi uongo.
20And the things that I write to you, lo, before God — I lie not;
21Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.
21then I came to the regions of Syria and of Cilicia,
22Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.
22and was unknown by face to the assemblies of Judea, that [are] in Christ,
23Walichokuwa wanajua ni kile tu walichosikia: "Mtu yule aliyekuwa akitutesa hapo awali, sasa anaihubiri imani ileile aliyokuwa anajaribu kuiangamiza."
23and only they were hearing, that `he who is persecuting us then, doth now proclaim good news — the faith that then he was wasting;`
24Basi, wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
24and they were glorifying God in me.