Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

John

16

1"Nimewaambieni hayo kusudi msiiache imani yenu.
1`These things I have spoken to you, that ye may not be stumbled,
2Watu watawatenga ninyi na masunagogi yao. Tena, wakati unakuja ambapo kila atakayewaua ninyi atadhani anamhudumia Mungu.
2out of the synagogues they will put you; but an hour doth come, that every one who hath killed you, may think to offer service unto God;
3Watawatendeeni mambo hayo kwa sababu hawamjui Baba, wala hawanijui mimi.
3and these things they will do to you, because they did not know the Father, nor me.
4Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni. "Sikuwaambieni mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
4`But these things I have spoken to you, that when the hour may come, ye may remember them, that I said [them] to you, and these things to you from the beginning I did not say, because I was with you;
5Lakini sasa namwendea yule aliyenituma; na hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza: Unakwenda wapi?
5and now I go away to Him who sent me, and none of you doth ask me, Whither dost thou go?
6Kwa kuwa nimewaambieni mambo hayo mmejaa huzuni mioyoni mwenu.
6but because these things I have said to you, the sorrow hath filled your heart.
7Lakini, nawaambieni ukweli: afadhali kwenu mimi niende zangu, maana nisipokwenda Msaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, basi, nitamtuma kwenu.
7`But I tell you the truth; it is better for you that I go away, for if I may not go away, the Comforter will not come unto you, and if I go on, I will send Him unto you;
8Naye atakapokuja atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, uadilifu na hukumu ya Mungu.
8and having come, He will convict the world concerning sin, and concerning righteousness, and concerning judgment;
9Wamekosea kuhusu dhambi kwa sababu hawaniamini;
9concerning sin indeed, because they do not believe in me;
10kuhusu uadilifu, kwa sababu naenda zangu kwa Baba, nanyi hamtaniona tena;
10and concerning righteousness, because unto my Father I go away, and no more do ye behold me;
11kuhusu hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amekwisha hukumiwa.
11and concerning judgment, because the ruler of this world hath been judged.
12"Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili.
12`I have yet many things to say to you, but ye are not able to bear [them] now;
13Lakini atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza kwenye ukweli wote; maana hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, bali atawaambieni yote atakayosikia, na atasema mambo yatakayokuwa yanakuja.
13and when He may come — the Spirit of truth — He will guide you to all the truth, for He will not speak from Himself, but as many things as He will hear He will speak, and the coming things He will tell you;
14Yeye atanitukuza mimi kwa kuwa atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
14He will glorify me, because of mine He will take, and will tell to you.
15Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu; ndiyo maana nimesema kwamba huyo Roho Mtakatifu atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
15`All things, as many as the Father hath, are mine; because of this I said, That of mine He will take, and will tell to you;
16"Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona!"
16a little while, and ye do not behold me, and again a little while, and ye shall see me, because I go away unto the Father.`
17Hapo baadhi ya wanafunzi wake wakaulizana, "Ana maana gani anapotwambia: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona? Tena anasema: Kwa kuwa ninakwenda kwa Baba!"
17Therefore said [some] of his disciples one to another, `What is this that he saith to us, A little while, and ye do not behold me, and again a little while, and ye shall see me, and, Because I go away unto the Father?`
18Basi, wakawa wanaulizana, "Ana maana gani anaposema: Bado kitambo kidogo? Hatuelewi anaongelea nini."
18they said then, `What is this he saith — the little while? we have not known what he saith.`
19Yesu alijua kwamba walitaka kumwuliza, basi akawaambia, "Je, mnaulizana juu ya yale niliyosema: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona?
19Jesus, therefore, knew that they were wishing to ask him, and he said to them, `Concerning this do ye seek one with another, because I said, A little while, and you do not behold me, and again a little while, and ye shall see me?
20Nawaambieni kweli, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi: mtaona huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
20verily, verily, I say to you, that ye shall weep and lament, and the world will rejoice; and ye shall be sorrowful, but your sorrow joy will become.
21Wakati mama anapojifungua huona huzuni kwa sababu saa ya maumivu imefika; lakini akisha jifungua hayakumbuki tena maumivu hayo kwa sababu ya furaha kwamba mtu amezaliwa duniani.
21`The woman, when she may bear, hath sorrow, because her hour did come, and when she may bear the child, no more doth she remember the anguish, because of the joy that a man was born to the world.
22Ninyi pia mna huzuni sasa; lakini nitawajieni tena, nanyi mtajaa furaha mioyoni mwenu, na furaha hiyo hakuna mtu atakayeiondoa kwenu.
22`And ye, therefore, now, indeed, have sorrow; and again I will see you, and your heart shall rejoice, and your joy no one doth take from you,
23Siku hiyo hamtaniomba chochote. Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu, atawapeni.
23and in that day ye will question me nothing; verily, verily, I say to you, as many things as ye may ask of the Father in my name, He will give you;
24Mpaka sasa hamjaomba chochote kwa jina langu. Ombeni nanyi mtapata ili furaha yenu ikamilike.
24till now ye did ask nothing in my name; ask, and ye shall receive, that your joy may be full.
25"Nimewaambieni mambo hayo kwa mafumbo. Lakini wakati utakuja ambapo sitasema tena nanyi kwa mafumbo, bali nitawaambieni waziwazi juu ya Baba.
25`These things in similitudes I have spoken to you, but there cometh an hour when no more in similitudes will I speak to you, but freely of the Father, will tell you.
26Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitamwomba Baba kwa niaba yenu;
26`In that day, in my name ye will make request, and I do not say to you that I will ask the Father for you,
27maana yeye mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu ninyi mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
27for the Father himself doth love you, because me ye have loved, and ye have believed that I from God came forth;
28Mimi nilitoka kwa Baba, nikaja ulimwenguni; na sasa nauacha ulimwengu na kurudi kwa Baba."
28I came forth from the Father, and have come to the world; again I leave the world, and go on unto the Father.`
29Basi, wanafunzi wake wakamwambia, "Ahaa! Sasa unasema waziwazi kabisa bila kutumia mafumbo.
29His disciples say to him, `Lo, now freely thou dost speak, and no similitude speakest thou;
30Sasa tunajua kwamba wewe unajua kila kitu, na huna haja ya kuulizwa maswali na mtu yeyote; kwa hiyo tunaamini kwamba umetoka kwa Mungu."
30now we have known that thou hast known all things, and hast no need that any one do question thee; in this we believe that from God thou didst come forth.`
31Yesu akawajibu, "Je, mnaamini sasa?
31Jesus answered them, `Now do ye believe? lo, there doth come an hour,
32Wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo ninyi nyote mtatawanyika kila mtu kwake, nami nitaachwa peke yangu. Kumbe, lakini mimi siko peke yangu, maana Baba yu pamoja nami.
32and now it hath come, that ye may be scattered, each to his own things, and me ye may leave alone, and I am not alone, because the Father is with me;
33Nimewaambieni mambo haya ili mpate kuwa na amani katika kuungana nami. Ulimwenguni mtapata masumbuko; lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu!"
33these things I have spoken to you, that in me ye may have peace, in the world ye shall have tribulation, but take courage — I have overcome the world.`