1Baada ya kusema yale aliyotaka watu wasikie, Yesu alikwenda Kafarnaumu.
1And when he completed all his sayings in the ears of the people, he went into Capernaum;
2Huko kulikuwa na jemadari mmoja Mroma ambaye alikuwa na mtumishi wake aliyempenda sana. Huyu mtumishi alikuwa mgonjwa karibu kufa.
2and a certain centurion`s servant being ill, was about to die, who was much valued by him,
3Yule jemadari aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee fulani Wayahudi waende kumwomba aje amponye mtumishi wake.
3and having heard about Jesus, he sent unto him elders of the Jews, beseeching him, that having come he might thoroughly save his servant.
4Walipofika kwa Yesu, walimsihi sana, wakasema: "Huyu anastahili afanyiwe jambo hilo,
4And they, having come near unto Jesus, were calling upon him earnestly, saying — `He is worthy to whom thou shalt do this,
5maana analipenda taifa letu, na ndiye aliyetujengea lile sunagogi."
5for he doth love our nation, and the synagogue he did build to us.`
6Basi, Yesu akaenda pamoja nao. Alipokuwa karibu kufika nyumbani kwa yule jemadari Mroma, yule jemadari aliwatuma marafiki zake wamwambie Yesu: "Bwana, usijisumbue zaidi, maana mimi sistahili uingie nyumbani mwangu.
6And Jesus was going on with them, and now when he is not far distant from the house the centurion sent unto him friends, saying to him, `Sir, be not troubled, for I am not worthy that under my roof thou mayest enter;
7Ndio maana sikujiona nastahili hata kuja kwako; amuru tu, na mtumishi wangu atapona.
7wherefore not even myself thought I worthy to come unto thee, but say in a word, and my lad shall be healed;
8Mimi pia ni mtu niliye chini ya mamlaka, na ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda!, naye huenda; namwambia mwingine, Njoo! naye huja; na nikimwambia mtumishi wangu, Fanya hiki!, hufanya."
8for I also am a man placed under authority, having under myself soldiers, and I say to this [one], Go, and he goeth; and to another, Be coming, and he cometh; and to my servant, Do this, and he doth [it].`
9Yesu aliposikia hayo, alishangaa; halafu akauelekea ule umati wa watu uliokuwa unamfuata, akasema, "Sijaona imani kubwa namna hii hata katika Israeli."
9And having heard these things Jesus wondered at him, and having turned to the multitude following him, he said, `I say to you, not even in Israel so much faith did I find;`
10Wale watu walipowasili nyumbani walimkuta yule mtumishi hajambo kabisa.
10and those sent, having turned back to the house, found the ailing servant in health.
11Baadaye kidogo Yesu alikwenda katika mji mmoja uitwao Naini, na wafuasi wake pamoja na kundi kubwa la watu waliandamana naye.
11And it came to pass, on the morrow, he was going on to a city called Nain, and there were going with him many of his disciples, and a great multitude,
12Basi, alipokuwa anakaribia lango la mji, walitokea watu wamebeba maiti ya kijana mmoja, mtoto wa pekee wa mama mjane. Watu wengi wa mji ule walikuwa pamoja na huyo mama.
12and as he came nigh to the gate of the city, then, lo, one dead was being carried forth, an only son of his mother, and she a widow, and a great multitude of the city was with her.
13Bwana alipomwona mama huyo, alimwonea huruma, akamwambia, "Usilie."
13And the Lord having seen her, was moved with compassion towards her, and said to her, `Be not weeping;`
14Kisha akaenda, akaligusa lile jeneza, na wale waliokuwa wanalichukua wakasimama. Halafu akasema, "Kijana! Nakuamuru, amka!"
14and having come near, he touched the bier, and those bearing [it] stood still, and he said, `Young man, to thee I say, Arise;`
15Yule aliyekufa akaketi, akaanza kuongea. Na Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
15and the dead sat up, and began to speak, and he gave him to his mother;
16Watu wote walishikwa na hofu, wakawa wanamtukuza Mungu wakisema: "Nabii mkuu ametokea kati yetu. Mungu amekuja kuwakomboa watu wake."
16and fear took hold of all, and they were glorifying God, saying — `A great prophet hath risen among us,` and — `God did look upon His people.`
17Habari hizo zikaenea kote katika Uyahudi na katika nchi za jirani.
17And the account of this went forth in all Judea about him, and in all the region around.
18Wanafunzi wa Yohane walimpa habari Yohane juu ya mambo hayo yote. Naye Yohane, baada ya kuwaita wawili kati ya wanafunzi wake,
18And the disciples of John told him about all these things,
19aliwatuma kwa Bwana wamwulize: "Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?"
19and John having called near a certain two of his disciples, sent unto Jesus, saying, `Art thou he who is coming, or for another do we look?`
20Wale wanafunzi walipomfikia Yesu wakamwambia, "Yohane Mbatizaji ametutuma kwako tukuulize: Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?"
20And having come near to him, the men said, `John the Baptist sent us unto thee, saying, Art thou he who is coming, or for another do we look?`
21Wakati huohuo, Yesu alikuwa anawaponya watu wengi waliokuwa wanateseka kwa magonjwa na waliopagawa na pepo wabaya, akawawezesha vipofu wengi kuona tena.
21And in that hour he cured many from sicknesses, and plagues, and evil spirits, and to many blind he granted sight.
22Basi, Yesu akawajibu, "Nendeni mkamwambie Yohane yale mliyojionea na kuyasikia: vipofu wanaona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa Habari njema.
22And Jesus answering said to them, `Having gone on, report to John what ye saw and heard, that blind men do see again, lame do walk, lepers are cleansed, deaf do hear, dead are raised, poor have good news proclaimed;
23Heri mtu yule ambaye hana mashaka nami!"
23and happy is he whoever may not be stumbled in me.`
24Hapo wajumbe wa Yohane walipokwisha kwenda zao, Yesu alianza kuyaambia makundi ya watu juu ya Yohane: "Mlikwenda kule jangwani, hivi mlitaka kuona kitu gani? Mlitaka kuona unyasi unaotikiswa na upepo?
24And the messengers of John having gone away, he began to say unto the multitudes concerning John: `What have ye gone forth to the wilderness to look on? a reed by the wind shaken?
25Basi, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona mtu aliyevalia mavazi maridadi? La hasha! Wanaovaa mavazi maridadi na kuishi maisha ya anasa, hukaa katika majumba ya wafalme!
25but what have ye gone forth to see? a man in soft garments clothed? lo, they in splendid apparellings, and living in luxury, are in the houses of kings!
26Basi, niambieni, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, hakika ni zaidi ya nabii.
26`But what have ye gone forth to see? a prophet? Yes, I say to you, and much more than a prophet:
27Huyu Yohane ndiye anayesemwa katika Maandiko Matakatifu: Hapa ni mtumishi wangu, asema Bwana; ninamtuma akutangulie, akutayarishie njia."
27this is he concerning whom it hath been written, Lo, I send my messenger before thy face, who shall prepare thy way before thee;
28Yesu akamalizia kwa kusema, "Nawaambieni, kati ya binadamu wote hakuna aliye mkubwa zaidi kuliko Yohane Mbatizaji. Hata hivyo, yule aliye mdogo kabisa katika ufalme wa Mungu ni mkubwa zaidi kuliko yeye."
28for I say to you, a greater prophet, among those born of women, than John the Baptist there is not; but the least in the reign of God is greater than he.`
29Waliposikia hayo watu wote na watoza ushuru waliusifu wema wa Mungu; hao ndio wale waliokuwa wameupokea ubatizo wa Yohane.
29And all the people having heard, and the tax-gatherers, declared God righteous, having been baptized with the baptism of John,
30Lakini Mafarisayo na walimu wa Sheria walikataa mpango wa Mungu uliowahusu wakakataa kubatizwa na Yohane.
30but the Pharisees, and the lawyers, the counsel of God did put away for themselves, not having been baptized by him.
31Yesu akaendelea kusema, "Basi, nitawafananisha watu wa kizazi hiki na kitu gani? Ni watu wa namna gani?
31And the Lord said, `To what, then, shall I liken the men of this generation? and to what are they like?
32Ni kama vijana waliokuwa wamekaa sokoni na kuambiana, kikundi kimoja na kingine: Tumewapigieni ngoma, lakini hamkucheza! Tumeomboleza, lakini hamkulia!
32they are like to children, to those sitting in a market-place, and calling one to another, and saying, We piped to you, and ye did not dance, we mourned to you, and ye did not weep!
33Kwa maana Yohane alikuja, yeye alifunga na hakunywa divai, nanyi mkasema: Amepagawa na pepo!
33`For John the Baptist came neither eating bread nor drinking wine, and ye say, He hath a demon;
34Akaja Mwana wa Mtu; anakula na kunywa, mkasema: Mwangalieni mlafi huyu na mlevi; rafiki ya watoza ushuru na wenye dhambi!
34the Son of Man came eating and drinking, and ye say, Lo, a man, a glutton, and a wine drinker, a friend of tax-gatherers and sinners;
35Hata hivyo, hekima ya Mungu imethibitishwa kuwa njema na wote wale wanaoikubali."
35and the wisdom was justified from all her children.`
36Mfarisayo mmoja alimwalika Yesu kula chakula nyumbani kwake. Akaingia nyumbani mwa huyo Mfarisayo, akakaa kula chakula.
36And a certain one of the Pharisees was asking him that he might eat with him, and having gone into the house of the Pharisee he reclined (at meat),
37Basi, katika mji ule kulikuwa na mama mmoja aliyekuwa anaishi maisha mabaya. Alipopata habari kwamba Yesu yuko nyumbani kwa huyo Mfarisayo, alichukua chupa ya alabasta yenye marashi.
37and lo, a woman in the city, who was a sinner, having known that he reclineth (at meat) in the house of the Pharisee, having provided an alabaster box of ointment,
38Akaja, akasimama karibu na miguu yake Yesu, akilia, na machozi yake yakamdondokea Yesu miguuni. Huyo mwanamke akaipangusa miguu ya Yesu kwa nywele zake. Kisha akaibusu na kuipaka yale marashi.
38and having stood behind, beside his feet, weeping, she began to wet his feet with the tears, and with the hairs of her head she was wiping, and was kissing his feet, and was anointing with the ointment.
39Yule Mfarisayo aliyemwalika Yesu alipoona hayo, akawaza moyoni mwake, "Kama mtu huyu angekuwa kweli nabii angejua huyu mwanamke ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi."
39And the Pharisee who did call him, having seen, spake within himself, saying, `This one, if he were a prophet, would have known who and of what kind [is] the woman who doth touch him, that she is a sinner.`
40Yesu akamwambia huyo Mfarisayo, "Simoni, ninacho kitu cha kukwambia." Naye Simoni akamwambia, "Ndio Mwalimu, sema." Yesu akasema,
40And Jesus answering said unto him, `Simon, I have something to say to thee;` and he saith, `Teacher, say on.`
41"Watu wawili walikuwa wamemkopa mtu fedha: mmoja alikuwa amekopa dinari mia tano, na mwingine hamsini.
41`Two debtors were to a certain creditor; the one was owing five hundred denaries, and the other fifty;
42Waliposhindwa kulipa madeni yao, huyo mtu aliwasamehe wote wawili. Sasa ni yupi kati ya hao wawili atampenda zaidi huyo bwana?"
42and they not having [wherewith] to give back, he forgave both; which then of them, say thou, will love him more?`
43Simoni akamjibu, "Ni dhahiri kwamba yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi atampenda zaidi yule bwana." Yesu akamwambia, "Sawa."
43And Simon answering said, `I suppose that to whom he forgave the more;` and he said to him, `Rightly thou didst judge.`
44Halafu akamgeukia yule mwanamke na kumwambia Simoni, "Unamwona huyu mwanamke, sivyo? Basi, mimi nilipoingia hapa nyumbani kwako hukunipa maji ya kunawa miguu yangu; lakini mwanamke huyu ameniosha miguu yangu kwa machozi yake na kunipangusa kwa nywele zake.
44And having turned unto the woman, he said to Simon, `Seest thou this woman? I entered into thy house; water for my feet thou didst not give, but this woman with tears did wet my feet, and with the hairs of her head did wipe;
45Wewe hukunisalimu kwa kunibusu, lakini huyu mwanamke tangu nilipoingia hapa amekuwa akiibusu miguu yangu.
45a kiss to me thou didst not give, but this woman, from what [time] I came in, did not cease kissing my feet;
46Wewe hukunionyesha ukarimu wako kwa kunipaka mafuta kichwani, lakini huyu mwanamke amefanya hivyo kwa kunipaka mafuta miguu yangu.
46with oil my head thou didst not anoint, but this woman with ointment did anoint my feet;
47Kwa hiyo nakwambia amesamehewa dhambi zake nyingi kwa kuwa ameonyesha upendo mkubwa. Mwenye kusamehe kidogo, hupenda kidogo."
47therefore I say to thee, her many sins have been forgiven, because she did love much; but to whom little is forgiven, little he doth love.`
48Basi, Yesu akamwambia yule mwanamke, "Umesamehewa dhambi zako."
48And he said to her, `Thy sins have been forgiven;`
49Na hapo wale waliokuwa pamoja naye mezani wakaulizana, "Ni mtu wa namna gani huyu awezaye kusamehe dhambi?"
49and those reclining with him (at meat) began to say within themselves, `Who is this, who also doth forgive sins?`
50Naye Yesu akamwambia yule mwanamke, "Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani."
50and he said unto the woman, `Thy faith have saved thee, be going on to peace.`