Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Mark

11

1Walipokuwa wanakaribia Yerusalemu walifika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni. Hapo aliwatuma wawili wa wanafunzi wake,
1And when they come nigh to Jerusalem, to Bethphage, and Bethany, unto the mount of the Olives, he sendeth forth two of his disciples,
2akawaambia, "Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia humo, mtakuta mwana punda amefungwa ambaye bado hajatumiwa na mtu. Mfungueni mkamlete.
2and saith to them, `Go away to the village that is over-against you, and immediately, entering into it, ye shall find a colt tied, on which no one of men hath sat, having loosed it, bring [it]:
3Kama mtu akiwauliza, Mbona mnafanya hivyo? Mwambieni, Bwana anamhitaji na atamrudisha hapa mara."
3and if any one may say to you, Why do ye this? say ye that the lord hath need of it, and immediately he will send it hither.`
4Basi, wakaenda, wakamkuta mwana punda barabarani amefungwa mlangoni. Walipokuwa wakimfungua,
4And they went away, and found the colt tied at the door without, by the two ways, and they loose it,
5baadhi ya watu waliokuwa wamesimama hapo wakawauliza "Kwa nini mnamfungua huyo mwana punda?"
5and certain of those standing there said to them, `What do ye — loosing the colt?`
6Wanafunzi wakajibu kama Yesu alivyokuwa amewaambia; nao wakawaacha waende zao.
6and they said to them as Jesus commanded, and they suffered them.
7Wakampelekea Yesu huyo mwana punda. Wakatandika mavazi yao juu ya huyo mwana punda, na Yesu akaketi juu yake.
7And they brought the colt unto Jesus, and did cast upon it their garments, and he sat upon it,
8Watu wengi wakatandaza mavazi yao barabarani; wengine wakatandaza matawi ya miti waliyoyakata mashambani.
8and many did spread their garments in the way, and others were cutting down branches from the trees, and were strewing in the way.
9Watu wote waliotangulia na wale waliofuata wakapaaza sauti zao wakisema, "Hosana! Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana!
9And those going before and those following were crying out, saying, `Hosanna! blessed [is] he who is coming in the name of the Lord;
10Ubarikiwe Ufalme ujao wa baba yetu Daudi. Hosana juu mbinguni!"
10blessed is the coming reign, in the name of the Lord, of our father David; Hosanna in the highest.`
11Yesu aliingia mjini Yerusalemu akaenda moja kwa moja mpaka Hekaluni, akatazama kila kitu kwa makini. Lakini kwa vile ilikwisha kuwa jioni, akaenda Bethania pamoja na wale kumi na wawili.
11And Jesus entered into Jerusalem, and into the temple, and having looked round on all things, it being now evening, he went forth to Bethany with the twelve.
12Kesho yake, walipokuwa wanatoka Bethania, Yesu aliona njaa.
12And on the morrow, they having come forth from Bethany, he hungered,
13Basi, akaona kwa mbali mtini wenye majani mengi. Akauendea ili aone kama ulikuwa na tunda lolote. Alipoufikia, aliukuta bila tunda lolote ila majani matupu, kwa vile hayakuwa majira ya mtini kuzaa matunda.
13and having seen a fig-tree afar off having leaves, he came, if perhaps he shall find anything in it, and having come to it, he found nothing except leaves, for it was not a time of figs,
14Hapo akauambia mtini, "Tangu leo hata milele mtu yeyote asile matunda kwako." Nao wanafunzi wake walisikia maneno hayo.
14and Jesus answering said to it, `No more from thee — to the age — may any eat fruit;` and his disciples were hearing.
15Basi, wakafika Yerusalemu. Yesu akaingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza nje watu waliokuwa wanauza na kununua vitu humo ndani. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilishana fedha na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.
15And they come to Jerusalem, and Jesus having gone into the temple, began to cast forth those selling and buying in the temple, and the tables of the money-changers and the seats of those selling the doves, he overthrew,
16Hakumruhusu mtu yeyote kupitia Hekaluni akichukua kitu.
16and he did not suffer that any might bear a vessel through the temple,
17Kisha akawafundisha, "Imeandikwa: Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote! Lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi!"
17and he was teaching, saying to them, `Hath it not been written — My house a house of prayer shall be called for all the nations, and ye did make it a den of robbers?`
18Makuhani wakuu na walimu wa Sheria waliposikia hayo, walianza kutafuta njia ya kumwangamiza. Lakini walimwogopa kwa sababu umati wa watu ulishangazwa na mafundisho yake.
18And the scribes and the chief priests heard, and they were seeking how they shall destroy him, for they were afraid of him, because all the multitude was astonished at his teaching;
19Ilipokuwa jioni, Yesu na wanafunzi wake waliondoka mjini.
19and when evening came, he was going forth without the city.
20Asubuhi na mapema, walipokuwa wanapita, waliuona ule mtini umenyauka wote, hata mizizi.
20And in the morning, passing by, they saw the fig-tree having been dried up from the roots,
21Petro aliukumbuka, akamwambia Yesu, "Mwalimu, tazama! Ule mtini ulioulaani, umenyauka!"
21and Peter having remembered saith to him, `Rabbi, lo, the fig-tree that thou didst curse is dried up.`
22Yesu akawaambia, "Mwaminini Mungu.
22And Jesus answering saith to them, `Have faith of God;
23Nawaambieni kweli, mtu akiuambia mlima huu: Ng'oka ukajitose baharini bila kuona shaka moyoni mwake, ila akaamini kwamba mambo yote anayosema yanafanyika, atafanyiwa jambo hilo.
23for verily I say to you, that whoever may say to this mount, Be taken up, and be cast into the sea, and may not doubt in his heart, but may believe that the things that he saith do come to pass, it shall be to him whatever he may say.
24Kwa hiyo nawaambieni, mnaposali na kuomba kitu, aminini kwamba mmekipokea, nanyi mtapewa.
24Because of this I say to you, all whatever — praying — ye do ask, believe that ye receive, and it shall be to you.
25Mnaposimama kusali, sameheni kila mtu aliyewakosea chochote, ili Baba yenu aliye mbinguni awasamehe ninyi makosa yenu.
25`And whenever ye may stand praying, forgive, if ye have anything against any one, that your Father also who is in the heavens may forgive you your trespasses;
26Lakini msipowasamehe wengine, hata Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu."
26and, if ye do not forgive, neither will your Father who is in the heavens forgive your trespasses.`
27Basi, wakafika tena Yerusalemu. Yesu alipokuwa akitembea Hekaluni, makuhani wakuu, walimu wa Sheria na wazee walimwendea,
27And they come again to Jerusalem, and in the temple, as he is walking, there come unto him the chief priests, and the scribes, and the elders,
28wakamwuliza, "Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Nani aliyekupa mamlaka ya kufanya mambo haya?"
28and they say to him, `By what authority dost thou these things? and who gave thee this authority that these things thou mayest do?`
29Lakini Yesu akawaambia, "Nitawaulizeni swali moja; mkinijibu, na pia nitawaambieni ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
29And Jesus answering said to them, `I will question you — I also — one word; and answer me, and I will tell you by what authority I do these things;
30Je, mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka mbinguni ama kwa watu? Nijibuni."
30the baptism of John — from heaven was it? or from men? answer me.`
31Wakaanza kujadiliana, "Tukisema, Yalitoka mbinguni, atatuuliza, Basi, mbona hamkumsadiki?
31And they were reasoning with themselves, saying, `If we may say, From heaven, he will say, Wherefore, then, did ye not believe him?
32Na tukisema, Yalitoka kwa watu..." (Waliogopa umati wa watu maana wote waliamini kwamba Yohane alikuwa kweli nabii.)
32But if we may say, From men,` — they were fearing the people, for all were holding John that he was indeed a prophet;
33Basi, wakamjibu Yesu, "Sisi hatujui." Naye Yesu akawaambia, "Nami pia sitawaambieni ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani."
33and answering they say to Jesus, `We have not known;` and Jesus answering saith to them, `Neither do I tell you by what authority I do these things.`