Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Matthew

19

1Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, alitoka Galilaya, akaenda katika mkoa wa Yudea, ng'ambo ya mto Yordani.
1And it came to pass, when Jesus finished these words, he removed from Galilee, and did come to the borders of Judea, beyond the Jordan,
2Watu wengi walimfuata huko, naye akawaponya.
2and great multitudes followed him, and he healed them there.
3Mafarisayo kadhaa walimjia, wakamwuliza kwa kumtega, "Je, ni halali mume kumpa talaka mkewe kwa kisa chochote?"
3And the Pharisees came near to him, tempting him, and saying to him, `Is it lawful for a man to put away his wife for every cause?`
4Yesu akawajibu, "Je, hamkusoma katika Maandiko Matakatifu kwamba Mungu aliyemuumba mtu tangu mwanzo alimfanya mwanamume na mwanamke,
4And he answering said to them, `Did ye not read, that He who made [them], from the beginning a male and a female made them,
5na akasema: Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ataungana na mke wake, nao wawili watakuwa mwili mmoja?
5and said, For this cause shall a man leave father and mother, and cleave to his wife, and they shall be — the two — for one flesh?
6Kwa hiyo wao si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asikitenganishe."
6so that they are no more two, but one flesh; what therefore God did join together, let no man put asunder.`
7Lakini wao wakamwuliza, "Kwa nini basi, Mose alituagiza mwanamke apewe hati ya talaka na kuachwa?"
7They say to him, `Why then did Moses command to give a roll of divorce, and to put her away?`
8Yesu akawajibu, "Mose aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
8He saith to them — `Moses for your stiffness of heart did suffer you to put away your wives, but from the beginning it hath not been so.
9Lakini haikuwa hivyo tangu mwanzo. Basi nawaambieni, yeyote atakayemwacha mke wake isipokuwa kwa sababu ya uzinzi, akaoa mke mwingine, anazini."
9`And I say to you, that, whoever may put away his wife, if not for whoredom, and may marry another, doth commit adultery; and he who did marry her that hath been put away, doth commit adultery.`
10Wanafunzi wake wakamwambia, "Ikiwa mambo ya mume na mkewe ni hivyo, ni afadhali kutooa kabisa."
10His disciples say to him, `If the case of the man with the woman is so, it is not good to marry.`
11Yesu akawaambia, "Si wote wanaoweza kulipokea fundisho hili, isipokuwa tu wale waliojaliwa na Mungu.
11And he said to them, `All do not receive this word, but those to whom it hath been given;
12Maana kuna sababu kadhaa za kutoweza kuoa: wengine ni kwa sababu wamezaliwa hivyo, wengine kwa sababu wamefanywa hivyo na watu, na wengine wameamua kutooa kwa ajili ya Ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea fundisho hili na alipokee."
12for there are eunuchs who from the mother`s womb were so born; and there are eunuchs who were made eunuchs by men; and there are eunuchs who kept themselves eunuchs because of the reign of the heavens: he who is able to receive [it] — let him receive.`
13Kisha watu wakamletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono na kuwaombea. Lakini wanafunzi wakawakemea.
13Then were brought near to him children that he might put hands on them and pray, and the disciples rebuked them.
14Yesu akasema, "Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie; maana Ufalme wa mbinguni ni wa watu walio kama watoto hawa."
14But Jesus said, `Suffer the children, and forbid them not, to come unto me, for of such is the reign of the heavens;`
15Basi, akawawekea mikono, kisha akaondoka mahali hapo.
15and having laid on them [his] hands, he departed thence.
16Mtu mmoja alimjia Yesu, akamwuliza, "Mwalimu, nifanye kitu gani chema ili niupate uzima wa milele?"
16And lo, one having come near, said to him, `Good teacher, what good thing shall I do, that I may have life age-during?`
17Yesu akamwambia, "Mbona unaniuliza kuhusu jambo jema? Kuna mmoja tu aliye mwema. Ukitaka kuingia katika uzima, shika amri."
17And he said to him, `Why me dost thou call good? no one [is] good except One — God; but if thou dost will to enter into the life, keep the commands.`
18Yule mtu akamwuliza, "Amri zipi?" Yesu akasema, "Usiue, usizini, usiibe, usitoe ushahidi wa uongo,
18He saith to him, `What kind?` And Jesus said, `Thou shalt not kill, thou shalt not commit adultery, thou shalt not steal, thou shalt not bear false witness,
19waheshimu baba yako na mama yako; na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe."
19honour thy father and mother, and, thou shalt love thy neighbor as thyself.`
20Huyo kijana akamwambia, "Hayo yote nimeyazingatia tangu utoto wangu; sasa nifanye nini zaidi?"
20The young man saith to him, `All these did I keep from my youth; what yet do I lack?`
21Yesu akamwambia, "Kama unapenda kuwa mkamilifu, nenda ukauze mali yako uwape maskini hiyo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni, kisha njoo unifuate."
21Jesus said to him, `If thou dost will to be perfect, go away, sell what thou hast, and give to the poor, and thou shalt have treasure in heaven, and come, follow me.`
22Huyo kijana aliposikia hayo, alienda zake akiwa mwenye huzuni, maana alikuwa na mali nyingi.
22And the young man, having heard the word, went away sorrowful, for he had many possessions;
23Hapo Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kweli nawaambieni, itakuwa vigumu sana kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni.
23and Jesus said to his disciples, `Verily I say to you, that hardly shall a rich man enter into the reign of the heavens;
24Tena nawaambieni, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni."
24and again I say to you, it is easier for a camel through the eye of a needle to go, than for a rich man to enter into the reign of God.`
25Wale wanafunzi waliposikia hivyo walishangaa, wakamwuliza, "Ni nani basi, awezaye kuokoka?"
25And his disciples having heard, were amazed exceedingly, saying, `Who, then, is able to be saved?`
26Yesu akawatazama, akasema, "Kwa binadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu mambo yote huwezekana."
26And Jesus having earnestly beheld, said to them, `With men this is impossible, but with God all things are possible.`
27Kisha Petro akasema, "Na sisi je? Tumeacha yote tukakufuata; tutapata nini basi?"
27Then Peter answering said to him, `Lo, we did leave all, and follow thee, what then shall we have?`
28Yesu akawaambia, "Nawaambieni kweli, Mwana wa Mtu atakapoketi katika kiti cha enzi cha utukufu wake katika ulimwengu mpya, ninyi mlionifuata mtaketi katika viti kumi na viwili mkiyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
28And Jesus said to them, `Verily I say to you, that ye who did follow me, in the regeneration, when the Son of Man may sit upon a throne of his glory, shall sit — ye also — upon twelve thrones, judging the twelve tribes of Israel;
29Na kila aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi, na kupata uzima wa milele.
29and every one who left houses, or brothers, or sisters, or father, or mother, or wife, or children, or fields, for my name`s sake, an hundredfold shall receive, and life age-during shall inherit;
30Lakini walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.
30and many first shall be last, and last first.