Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Romans

10

1Ndugu zangu, ninataka na kutazamia kwa moyo wangu wote hao wananchi wenzangu wakombolewe. Tena nawaombea kwa Mungu daima.
1Brethren, the pleasure indeed of my heart, and my supplication that [is] to God for Israel, is — for salvation;
2Maana naweza kuthibitisha kwa niaba yao kwamba wanayo bidii ya kumtafuta Mungu; lakini bidii hiyo haikujengwa juu ya ujuzi wa kweli.
2for I bear them testimony that they have a zeal of God, but not according to knowledge,
3Maana hawakufahamu jinsi Mungu anavyowafanya watu wawe waadilifu, na wamejaribu kuanzisha mtindo wao wenyewe, na hivyo hawakuikubali njia hiyo ya Mungu ya kuwafanya wawe waadilifu.
3for not knowing the righteousness of God, and their own righteousness seeking to establish, to the righteousness of God they did not submit.
4Maana kwa kuja kwake Kristo, Sheria imefikia kikomo chake, ili kila mtu anayeamini akubaliwe kuwa mwadilifu.
4For Christ is an end of law for righteousness to every one who is believing,
5Kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, Mose aliandika hivi: "Mtu yeyote anayetimiza matakwa ya Sheria ataishi."
5for Moses doth describe the righteousness that [is] of the law, that, `The man who did them shall live in them,`
6Lakini, kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya imani, yasemwa hivi: "Usiseme moyoni mwako: Nani atapanda mpaka mbinguni? (yaani, kumleta Kristo chini);
6and the righteousness of faith doth thus speak: `Thou mayest not say in thine heart, Who shall go up to the heaven,` that is, Christ to bring down?
7wala usiseme: Nani atashuka mpaka Kuzimu (yaani, kumleta Kristo kutoka kwa wafu)."
7or, `Who shall go down to the abyss,` that is, Christ out of the dead to bring up.
8Maandiko Matakatifu yesema hivi, "Ujumbe huo wa Mungu uko karibu nawe, uko kinywani mwako na moyoni mwako" nao ndio ile imani tunayoihubiri.
8But what doth it say? `Nigh thee is the saying — in thy mouth, and in thy heart:` that is, the saying of the faith, that we preach;
9Kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka wafu, utaokoka.
9that if thou mayest confess with thy mouth the Lord Jesus, and mayest believe in thy heart that God did raise him out of the dead, thou shalt be saved,
10Maana tunaamini kwa moyo na kukubaliwa kuwa waadilifu; na tunakiri kwa midomo yetu na kuokolewa.
10for with the heart doth [one] believe to righteousness, and with the mouth is confession made to salvation;
11Maandiko Matakatifu yasema: "Kila amwaminiye hatakuwa na sababu ya kuaibika."
11for the Writing saith, `Every one who is believing on him shall not be ashamed,`
12Jambo hili ni kwa wote, kwani hakuna tofauti kati ya Wayahudi na wasio Wayahudi; Bwana wa wote ni mmoja, naye ni mkarimu sana kwao wote wamwombao.
12for there is no difference between Jew and Greek, for the same Lord of all [is] rich to all those calling upon Him,
13Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kila mtu atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa."
13for every one — whoever shall call upon the name of the Lord, he shall be saved.`
14Basi, watamwombaje yeye ambaye hawamwamini? Tena, watamwaminije kama hawajapata kusikia habari zake? Na watasikiaje habari zake kama hakuna mhubiri?
14How then shall they call upon [him] in whom they did not believe? and how shall they believe [on him] of whom they did not hear? and how shall they hear apart from one preaching?
15Na watu watahubirije kama hawakutumwa? Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Ni jambo la kupendeza mno kuja kwa wale wanaohubiri Habari Njema!"
15and how shall they preach, if they may not be sent? according as it hath been written, `How beautiful the feet of those proclaiming good tidings of peace, of those proclaiming good tidings of the good things!`
16Lakini wote hawakuipokea hiyo Habari Njema. Maana Isaya alisema: "Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?"
16But they were not all obedient to the good tidings, for Isaiah saith, `Lord, who did give credence to our report?`
17Hivyo basi, imani inatokana na kuusikiliza ujumbe, na huo ujumbe unatokana na neno la Kristo.
17so then the faith [is] by a report, and the report through a saying of God,
18Lakini nauliza: je, hawakuusikia huo ujumbe? Naam, waliusikia; kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Sauti yao imeenea duniani kote; maneno yao yamefika mpaka kingo za ulimwengu."
18but I say, Did they not hear? yes, indeed — `to all the earth their voice went forth, and to the ends of the habitable world their sayings.`
19Tena nauliza: je, yawezekana kwamba watu wa Israeli hawakufahamu? Mose mwenyewe ni kwa kwanza kujibu: "Nitawafanyeni mwaonee wivu watu ambao si taifa; nitawafanyeni muwe na hasira juu ya taifa la watu wapumbavu."
19But I say, Did not Israel know? first Moses saith, `I will provoke you to jealousy by [that which is] not a nation; by an unintelligent nation I will anger you,`
20Tena Isaya anathubutu hata kusema: "Wale ambao hawakunitafuta wamenipata; nimejionyesha kwao wasiouliza habari zangu."
20and Isaiah is very bold, and saith, `I was found by those not seeking Me; I became manifest to those not inquiring after Me;`
21Lakini kuhusu Israeli anasema: "Mchana kutwa niliwanyoshea mikono yangu watu waasi na wasiotii."
21and unto Israel He saith, `All the day I did stretch out My hands unto a people unbelieving and gainsaying.`