Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Romans

12

1Kwa hiyo, ndugu zangu, maadam Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: jitoleeni nafsi zenu kwa Mungu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.
1I call upon you, therefore, brethren, through the compassions of God, to present your bodies a sacrifice — living, sanctified, acceptable to God — your intelligent service;
2Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu.
2and be not conformed to this age, but be transformed by the renewing of your mind, for your proving what [is] the will of God — the good, and acceptable, and perfect.
3Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni ninyi nyote: msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kufuatana na kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.
3For I say, through the grace that was given to me, to every one who is among you, not to think above what it behoveth to think; but to think so as to think wisely, as to each God did deal a measure of faith,
4Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake.
4for as in one body we have many members, and all the members have not the same office,
5Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
5so we, the many, one body are in Christ, and members each one of one another.
6Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake.
6And having gifts, different according to the grace that was given to us; whether prophecy — `According to the proportion of faith!`
7Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe.
7or ministration — `In the ministration!` or he who is teaching — `In the teaching!`
8Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.
8or he who is exhorting — `In the exhortation!` he who is sharing — `In simplicity!` he who is leading — `In diligence?` he who is doing kindness — `In cheerfulness.`
9Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
9The love unfeigned: abhorring the evil; cleaving to the good;
10Pendaneni kidugu; kila mmoja amfikirie mwenzake kwanza kwa heshima.
10in the love of brethren, to one another kindly affectioned: in the honour going before one another;
11Msilegee katika bidii, muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.
11in the diligence not slothful; in the spirit fervent; the Lord serving;
12Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida na kusali daima.
12in the hope rejoicing; in the tribulation enduring; in the prayer persevering;
13Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.
13to the necessities of the saints communicating; the hospitality pursuing.
14Watakieni baraka wote wanaowadhulumu ninyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani.
14Bless those persecuting you; bless, and curse not;
15Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
15to rejoice with the rejoicing, and to weep with the weeping,
16Muwe na wema uleule kwa kila mtu. Msijitakie makuu, bali jishugulisheni na watu wadogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.
16of the same mind one toward another, not minding the high things, but with the lowly going along; become not wise in your own conceit;
17Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.
17giving back to no one evil for evil; providing right things before all men.
18Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.
18If possible — so far as in you — with all men being in peace;
19Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza asema Bwana."
19not avenging yourselves, beloved, but give place to the wrath, for it hath been written, `Vengeance [is] Mine,
20Tena, Maandiko yasema: "Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake."
20I will recompense again, saith the Lord;` if, then, thine enemy doth hunger, feed him; if he doth thirst, give him drink; for this doing, coals of fire thou shalt heap upon his head;
21Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
21Be not overcome by the evil, but overcome, in the good, the evil.