1Basi, Myahudi ana nini zaidi kuliko watu wengine? Au kutahiriwa kuna faida gani?
1What, then, [is] the superiority of the Jew? or what the profit of the circumcision?
2Naam, iko faida kwa kila upande. Kwanza, Mungu aliwakabidhi Wayahudi ujumbe wake.
2much in every way; for first, indeed, that they were intrusted with the oracles of God;
3Lakini itakuwaje iwapo baadhi yao hawakuwa waaminifu? Je, jambo hilo litaondoa uaminifu wa Mungu?
3for what, if certain were faithless? shall their faithlessness the faithfulness of god make useless?
4Hata kidogo! Mungu hubaki mwaminifu daima, ingawaje kila binadamu ni mwongo. Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Kila usemapo, maneno yako ni ya haki; na katika hukumu, wewe hushinda."
4let it not be! and let God become true, and every man false, according as it hath been written, `That Thou mayest be declared righteous in Thy words, and mayest overcome in Thy being judged.`
5Lakini, ikiwa uovu wetu unathibitisha kwamba Mungu anatenda kwa haki, tutasema nini? Je, tutasema kwamba anakosa haki akituadhibu? (Hapa naongea kibinadamu).
5And, if our unrighteousness God`s righteousness doth establish, what shall we say? is God unrighteous who is inflicting the wrath? (after the manner of a man I speak)
6Hata kidogo! Ingekuwa hivyo, Mungu angewezaje kuuhukumu ulimwengu?
6let it not be! since how shall God judge the world?
7Labda utasema: "Ikiwa ukosefu wa uaminifu kwa upande wangu unamdhihirisha Mungu kuwa mwaminifu zaidi na hivyo kumpatia utukufu, basi singepaswa kuhukumiwa kuwa mwenye dhambi!"
7for if the truth of God in my falsehood did more abound to His glory, why yet am I also as a sinner judged?
8Ni sawa na kusema: tufanye maovu ili tupate mema! Ndivyo wengine walivyotukashifu kwa kutushtaki kwamba tumefundisha hivyo. Watahukumiwa wanavyostahili!
8and not, as we are evil spoken of, and as certain affirm us to say — `We may do the evil things, that the good ones may come?` whose judgment is righteous.
9Tuseme nini, basi? Je, sisi Wayahudi ni bora zaidi kuliko wengine? Hata kidogo! Kwa maana nimekwisha bainisha hapo mwanzoni kwamba Wayahudi na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa dhambi.
9What, then? are we better? not at all! for we did before charge both Jews and Greeks with being all under sin,
10Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!
10according as it hath been written — `There is none righteous, not even one;
11Hakuna mtu anayeelewa, wala anayemtafuta Mungu.
11There is none who is understanding, there is none who is seeking after God.
12Wote wamepotoka wote wamekosa; hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja.
12All did go out of the way, together they became unprofitable, there is none doing good, there is not even one.
13Makoo yao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu, midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.
13A sepulchre opened [is] their throat; with their tongues they used deceit; poison of asps [is] under their lips.
14Vinywa vyao vimejaa laana chungu.
14Whose mouth is full of cursing and bitterness.
15Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,
15Swift [are] their feet to shed blood.
16popote waendapo husababisha maafa na mateso;
16Ruin and misery [are] in their ways.
17njia ya amani hawaijui.
17And a way of peace they did not know.
18Hawajali kabisa kumcha Mungu."
18There is no fear of God before their eyes.`
19Tunajua kwamba Sheria huwahusu walio chini ya Sheria hiyo, hata hawawezi kuwa na kisingizio chochote, na ulimwengu wote uko chini ya hukumu ya Mungu.
19And we have known that as many things as the law saith, to those in the law it doth speak, that every mouth may be stopped, and all the world may come under judgment to God;
20Maana hakuna binadamu yeyote anayekubaliwa kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuishika Sheria; kazi ya Sheria ni kumwonyesha tu mtu kwamba ametenda dhambi.
20wherefore by works of law shall no flesh be declared righteous before Him, for through law is a knowledge of sin.
21Lakini sasa, njia ya Mungu ya kuwakubali watu kuwa waadilifu imekwisha dhihirishwa, tena bila kutegemea Sheria. Sheria na manabii hushuhudia jambo hili.
21And now apart from law hath the righteousness of God been manifested, testified to by the law and the prophets,
22Mungu huwakubali watu kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao kwa Yesu Kristo; Mungu hufanya hivyo kwa wote wanaoamini; hakuna ubaguzi wowote.
22and the righteousness of God [is] through the faith of Jesus Christ to all, and upon all those believing, — for there is no difference,
23Watu wote wametenda dhambi na wametindikiwa utukufu wa Mungu.
23for all did sin, and are come short of the glory of God —
24Lakini kwa zawadi ya neema ya Mungu, watu wote hukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Yesu Kristo anayewakomboa.
24being declared righteous freely by His grace through the redemption that [is] in Christ Jesus,
25Mungu alimtoa Yesu kusudi, kwa damu yake, awe njia ya kuwaondolea watu dhambi zao kwa imani yao kwake. Alifanya hivyo ili apate kuonyesha kwamba yeye ni mwadilifu. Hapo zamani Mungu alikuwa mvumilivu bila kuzijali dhambi za watu;
25whom God did set forth a mercy seat, through the faith in his blood, for the shewing forth of His righteousness, because of the passing over of the bygone sins in the forbearance of God —
26lakini sasa, wakati huu, anazikabili dhambi za watu apate kuonyesha uadilifu wake. Kwa namna hiyo Mungu mwenyewe huonyesha kwamba yeye ni mwadilifu na kwamba humkubali kuwa mwadilifu mtu yeyote anayemwamini Yesu.
26for the shewing forth of His righteousness in the present time, for His being righteous, and declaring him righteous who [is] of the faith of Jesus.
27Basi, tunaweza kujivunia nini? Hakuna! Kwa nini? Je, kwa sababu ya kutimiza Sheria? La! Bali kwa sababu tunaamini.
27Where then [is] the boasting? it was excluded; by what law? of works? no, but by a law of faith:
28Maana mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya Sheria.
28therefore do we reckon a man to be declared righteous by faith, apart from works of law.
29Au je, Mungu nu Mungu wa Wayahudi tu, ama pia wa watu wa mataifa mengine? Naam, wa mataifa mengine pia.
29The God of Jews only [is He], and not also of nations?
30Mungu ni mmoja, naye atawakubali Wayahudi kuwa waadilifu kwa imani yao, na watu wa mataifa mengine pia kwa imani yao.
30yes, also of nations; since one [is] God who shall declare righteous the circumcision by faith, and the uncircumcision through the faith.
31Je, tunaitumia imani kuibatilisha Sheria? Hata kidogo; bali tunaipa Sheria thamani yake kamili.
31Law then do we make useless through the faith? let it not be! yea, we do establish law.