1Sasa, kwa vile tumekubaliwa kuwa wadilifu kwa imani, basi, tunayo amani na Mungu kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo.
1Having been declared righteous, then, by faith, we have peace toward God through our Lord Jesus Christ,
2Kwa imani yetu, yeye ametuleta katika hali hii ya neema ya Mungu ambamo sasa tunaishi. Basi, tunajivunia tumaini tulilo nalo la kushiriki utukufu wa Mungu.
2through whom also we have the access by the faith into this grace in which we have stood, and we boast on the hope of the glory of God.
3Naam, si hayo tu, bali tunafurahi pia katika taabu tukijua kwamba taabu huleta saburi,
3And not only [so], but we also boast in the tribulations, knowing that the tribulation doth work endurance;
4nayo saburi huleta uthabiti, na uthabiti huleta tumaini.
4and the endurance, experience; and the experience, hope;
5Tumaini hilo haliwezi kutuhadaa, maana Mungu amekwisha miminia mioyoni mwetu upendo wake kwa njia ya Roho Mtakatifu aliyetujalia.
5and the hope doth not make ashamed, because the love of God hath been poured forth in our hearts through the Holy Spirit that hath been given to us.
6Tulipokuwa bado wanyonge, Kristo, wakati ulipotimia, alikufa kwa ajili yetu sisi waovu.
6For in our being still ailing, Christ in due time did die for the impious;
7Si rahisi mtu kufa kwa ajili ya mtu mwadilifu; labda mtu anaweza kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.
7for scarcely for a righteous man will any one die, for for the good man perhaps some one also doth dare to die;
8Lakini Mungu amethibitisha kwamba anatupenda, maana wakati tulipokuwa bado wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.
8and God doth commend His own love to us, that, in our being still sinners, Christ did die for us;
9Kwa kuwa sasa tumekubaliwa kuwa waadilifu kwa damu ya Kristo, ni dhahiri zaidi kwamba atatuokoa katika ghadhabu ya Mungu.
9much more, then, having been declared righteous now in his blood, we shall be saved through him from the wrath;
10Maana, tulipokuwa bado adui zake, Mungu alitupatanisha naye kwa kifo cha Mwanae. Na kwa vile sasa tumepatanishwa naye, ni dhahiri zaidi kwamba tutaokolewa kwa uzima wa Kristo.
10for if, being enemies, we have been reconciled to God through the death of His Son, much more, having been reconciled, we shall be saved in his life.
11Wala si hayo tu, ila tunafurahi pia katika Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ametupatanisha na Mungu.
11And not only [so], but we are also boasting in God, through our Lord Jesus Christ, through whom now we did receive the reconciliation;
12Kwa njia ya mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, nayo ikasababisha kifo. Hivyo kifo kimeenea katika jumuiya yote ya binadamu, kwa maana wote wametenda dhambi.
12because of this, even as through one man the sin did enter into the world, and through the sin the death; and thus to all men the death did pass through, for that all did sin;
13Kabla ya Sheria kuwako, dhambi ilikuwako ulimwenguni; lakini dhambi haiwekwi katika kumbukumbu bila sheria.
13for till law sin was in the world: and sin is not reckoned when there is not law;
14Lakini tangu wakati wa Adamu mpaka wakati wa Mose, kifo kiliwatawala hata wale ambao hawakutenda dhambi kama ile ya Adamu, ya kumwasi Mungu. Adamu alikuwa kielelezo cha yule ambaye atakuja baadaye.
14but the death did reign from Adam till Moses, even upon those not having sinned in the likeness of Adam`s transgression, who is a type of him who is coming.
15Lakini ipo tofauti: neema ya Mungu si kama dhambi ya Adamu. Maana, ingawa dhambi ya mtu mmoja ilisababisha kifo kwa wote, kwa fadhili ya mtu mmoja, yaani Yesu Kristo, Mungu amewazidishia wote neema na zawadi zake.
15But, not as the offence so also [is] the free gift; for if by the offence of the one the many did die, much more did the grace of God, and the free gift in grace of the one man Jesus Christ, abound to the many;
16Kuna tofauti baina ya zawadi ya Mungu, na dhambi ya mtu yule mmoja. Maana, baada ya kosa la mtu mmoja, Mungu alitoa hukumu; lakini baada ya makosa ya watu wengi, Mungu aliwapa zawadi yake kwa kuwasamehe.
16and not as through one who did sin [is] the free gift, for the judgment indeed [is] of one to condemnation, but the gift [is] of many offences to a declaration of `Righteous,`
17Kweli, kwa dhambi ya mtu mmoja kifo kilianza kutawala kwa sababu ya huyo mtu mmoja; lakini, ni dhahiri zaidi kwamba alichokifanya yule mtu mmoja, yaani Yesu Kristo, ni bora zaidi. Wote wanaopokea neema na zawadi hiyo ya kukubaliwa kuwa waadilifu, watatawala katika uzima kwa njia ya huyo mmoja, yaani Yesu Kristo.
17for if by the offence of the one the death did reign through the one, much more those, who the abundance of the grace and of the free gift of the righteousness are receiving, in life shall reign through the one — Jesus Christ.
18Basi, kama vile kosa la mtu mmoja lilivyoleta hukumu kwa binadamu wote, kadhalika kitendo kimoja kiadilifu kinawapa uhuru na uzima.
18So, then, as through one offence to all men [it is] to condemnation, so also through one declaration of `Righteous` [it is] to all men to justification of life;
19Na kama kwa kutotii kwa mtu mmoja watu wengi walifanywa wenye dhambi, kadhalika kutii kwa mtu mmoja kutawafanya wengi wakubaliwe kuwa waadilifu.
19for as through the disobedience of the one man, the many were constituted sinners: so also through the obedience of the one, shall the many be constituted righteous.
20Sheria ilitokea, ikasababisha kuongezeka kwa uhalifu; lakini pale dhambi ilipoongezeka, neema iliongezeka zaidi.
20And law came in, that the offence might abound, and where the sin did abound, the grace did overabound,
21Kama vile dhambi ilivyotawala kwa kifo, kadhalika neema inatawala kwa njia ya uadilifu, na kuleta uzima wa milele kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu.
21that even as the sin did reign in the death, so also the grace may reign, through righteousness, to life age-during, through Jesus Christ our Lord.