1Yesu alisema "Kweli nawaambieni, yeyote yule asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia mlangoni, bali hupenya na kuingia kwa njia nyingine, huyo ni mwizi na mnyang'anyi.
1الحق الحق اقول لكم ان الذي لا يدخل من الباب الى حظيرة الخراف بل يطلع من موضع آخر فذاك سارق ولص.
2Lakini anayeingia kwa kupitia mlangoni, huyo ndiye mchungaji wa kondoo.
2واما الذي يدخل من الباب فهو راعي الخراف.
3Mngoja mlango wa zizi humfungulia, na kondoo husikia sauti yake, naye huwaita kondoo wake kila mmoja kwa jina lake na kuwaongoza nje.
3لهذا يفتح البواب والخراف تسمع صوته فيدعو خرافه الخاصة باسماء ويخرجها.
4Akisha watoa nje huwatangulia mbele nao kondoo humfuata, kwani wanaijua sauti yake.
4ومتى اخرج خرافه الخاصة يذهب امامها والخراف تتبعه لانها تعرف صوته.
5Kondoo hao hawawezi kumfuata mgeni, bali watamkimbia kwa sababu hawaijui sauti yake."
5واما الغريب فلا تتبعه بل تهرب منه لانها لا تعرف صوت الغرباء.
6Yesu aliwaambia mfano huo, lakini wao hawakuelewa alichotaka kuwaambia.
6هذا المثل قاله لهم يسوع. واما هم فلم يفهموا ما هو الذي كان يكلمهم به
7Basi, akasema tena, "Kweli nawaambieni, mimi ni mlango wa kondoo.
7فقال لهم يسوع ايضا الحق الحق اقول لكم اني انا باب الخراف.
8Wale wengine wote waliokuja kabla yangu ni wezi na wanyang'anyi, nao kondoo hawakuwasikiliza.
8جميع الذين أتوا قبلي هم سراق ولصوص. ولكن الخراف لم تسمع لهم.
9Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na kupata malisho.
9انا هو الباب. ان دخل بي احد فيخلص ويدخل ويخرج ويجد مرعى.
10Mwizi huja kwa shabaha ya kuiba, kuua na kuharibu. Mimi nimekuja mpate kuwa na uzima--uzima kamili.
10السارق لا يأتي الا ليسرق ويذبح ويهلك. واما انا فقد أتيت لتكون لهم حياة وليكون لهم افضل.
11"Mimi ni mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo wake.
11انا هو الراعي الصالح. والراعي الصالح يبذل نفسه عن الخراف.
12Mtu wa kuajiriwa ambaye si mchungaji, na wala kondoo si mali yake, anapoona mbwa mwitu anakuja, huwaacha kondoo na kukimbia. Kisha mbwa mwitu huwakamata na kuwatawanya.
12واما الذي هو اجير وليس راعيا الذي ليست الخراف له فيرى الذئب مقبلا ويترك الخراف ويهرب. فيخطف الذئب الخراف ويبددها.
13Yeye hajali kitu juu ya kondoo kwa sababu yeye ni mtu wa mshahara tu.
13والاجير يهرب لانه اجير ولا يبالي بالخراف.
14Mimi ni mchungaji mwema. Nawajua walio wangu, nao walio wangu wananijua mimi,
14اما انا فاني الراعي الصالح واعرف خاصتي وخاصتي تعرفني
15kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Mimi nayatoa maisha yangu kwa ajili yao.
15كما ان الآب يعرفني وانا اعرف الآب. وانا اضع نفسي عن الخراف.
16Tena ninao kondoo wengine ambao hawamo zizini humu. Inanibidi kuwaleta hao pia, nao wataisikia sauti yangu, na kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.
16ولي خراف أخر ليست من هذه الحظيرة ينبغي ان آتي بتلك ايضا فتسمع صوتي وتكون رعية واحدة وراع واحد.
17"Baba ananipenda kwani nautoa uhai wangu ili nipate kuupokea tena.
17لهذا يحبني الآب لاني اضع نفسي لآخذها ايضا.
18Hakuna mtu anayeninyang'anya uhai wangu; mimi na nautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa na uwezo wa kuuchukua tena. Hivi ndivyo Baba alivyoniamuru nifanye."
18ليس احد يأخذها مني بل اضعها انا من ذاتي. لي سلطان ان اضعها ولي سلطان ان آخذها ايضا. هذه الوصية قبلتها من ابي.
19Kukawa tena na mafarakano kati ya Wayahudi kwa sababu ya maneno haya.
19فحدث ايضا انشقاق بين اليهود بسبب هذا الكلام.
20Wengi wao wakasema, "Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?"
20فقال كثيرون منهم به شيطان وهو يهذي. لماذا تستمعون له.
21Wengine wakasema, "Haya si maneno ya mwenye pepo. Je, pepo anaweza kuyafumbua macho ya vipofu?"
21آخرون قالوا ليس هذا كلام من به شيطان. ألعل شيطانا يقدر ان يفتح اعين العميان
22Huko Yerusalemu kulikuwa na sikukuu ya Kutabaruku. Wakati huo ulikuwa wa baridi.
22وكان عيد التجديد في اورشليم وكان شتاء.
23Naye Yesu akawa anatembea Hekaluni katika ukumbi wa Solomoni.
23وكان يسوع يتمشى في الهيكل في رواق سليمان.
24Basi, Wayahudi wakamzunguka, wakamwuliza, "Utatuacha katika mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo, basi, tuambie wazi."
24فاحتاط به اليهود وقالوا له الى متى تعلّق انفسنا. ان كنت انت المسيح فقل لنا جهرا.
25Yesu akawajibu, "Nimewaambieni, lakini hamsadiki. Kazi ninazozifanya mimi kwa jina la Baba yangu zinanishuhudia.
25اجابهم يسوع اني قلت لكم ولستم تؤمنون. الاعمال التي انا اعملها باسم ابي هي تشهد لي.
26Lakini ninyi hamsadiki kwa sababu ninyi si kondoo wangu.
26ولكنكم لستم تؤمنون لانكم لستم من خرافي كما قلت لكم.
27Kondoo wangu huisikia sauti yangu; mimi nawajua, nao hunifuata.
27خرافي تسمع صوتي وانا اعرفها فتتبعني.
28Mimi nawapa uzima wa milele; nao hawatapotea milele, wala hakuna mtu atakayeweza kuwatoa mkononi mwangu.
28وانا اعطيها حياة ابدية ولن تهلك الى الابد ولا يخطفها احد من يدي.
29Baba yangu ambaye ndiye aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote, wale hakuna awezaye kuwatoa mikononi mwake Baba.
29ابي الذي اعطاني اياها هو اعظم من الكل ولا يقدر احد ان يخطف من يد ابي.
30Mimi na Baba, tu mmoja."
30انا والآب واحد
31Basi, Wayahudi wakachukua mawe ili wamtupie.
31فتناول اليهود ايضا حجارة ليرجموه.
32Yesu akawaambia, "Nimewaonyesheni kazi nyingi kutoka kwa Baba. Ni ipi kati ya hizo inayowafanya mnipige mawe?"
32اجابهم يسوع اعمالا كثيرة حسنة أريتكم من عند ابي. بسبب اي عمل منها ترجمونني.
33Wayahudi wakamjibu, "Hatukupigi mawe kwa ajili ya tendo jema, ila kwa sababu ya kukufuru! Maana wajifanya kuwa Mungu hali wewe ni binadamu tu."
33اجابه اليهود قائلين لسنا نرجمك لاجل عمل حسن بل لاجل تجديف. فانك وانت انسان تجعل نفسك الها.
34Yesu akawajibu, "Je, haikuandikwa katika Sheria yenu: Mimi nimesema, ninyi ni miungu?
34اجابهم يسوع أليس مكتوبا في ناموسكم انا قلت انكم آلهة.
35Mungu aliwaita miungu wale waliopewa neno lake; nasi twajua kwamba Maandiko Matakatifu yasema ukweli daima.
35ان قال آلهة لاولئك الذين صارت اليهم كلمة الله. ولا يمكن ان ينقض المكتوب.
36Je, yeye ambaye Baba alimweka wakfu na kumtuma ulimwenguni, mnamwambia: Unakufuru, eti kwa sababu nilisema: Mimi ni Mwana wa Mungu?
36فالذي قدسه الآب وارسله الى العالم أتقولون له انك تجدف لاني قلت اني ابن الله.
37Kama sifanyi kazi za Baba yangu msiniamini.
37ان كنت لست اعمل اعمال ابي فلا تؤمنوا بي.
38Lakini ikiwa ninazifanya, hata kama hamniamini, walau ziaminini hizo kazi mpate kujua na kutambua kwamba Baba yuko ndani yangu, nami niko ndani yake."
38ولكن ان كنت اعمل فان لم تؤمنوا بي فآمنوا بالاعمال لكي تعرفوا وتؤمنوا ان الآب فيّ وانا فيه
39Wakajaribu tena kumkamata lakini akachopoka mikononi mwao.
39فطلبوا ايضا ان يمسكوه فخرج من ايديهم.
40Yesu akaenda tena ng'ambo ya mto Yordani, mahali Yohane alipokuwa akibatiza, akakaa huko.
40ومضى ايضا الى عبر الاردن الى المكان الذي كان يوحنا يعمد فيه اولا ومكث هناك.
41Watu wengi walimwendea wakasema, "Yohane hakufanya ishara yoyote. Lakini yale yote Yohane aliyosema juu ya mtu huyu ni kweli kabisa."
41فأتى اليه كثيرون وقالوا ان يوحنا لم يفعل آية واحدة. ولكن كل ما قاله يوحنا عن هذا كان حقا.
42Watu wengi mahali hapo wakamwamini.
42فآمن كثيرون به هناك