Swahili: New Testament

الكتاب المقدس (Van Dyke)

Luke

1

1Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
1اذ كان كثيرون قد اخذوا بتاليف قصة في الامور المتيقنة عندنا
2Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
2كما سلمها الينا الذين كانوا منذ البدء معاينين وخداما للكلمة
3Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
3رأيت انا ايضا اذ قد تتبعت كل شيء من الاول بتدقيق ان اكتب على التوالي اليك ايها العزيز ثاوفيلس
4ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
4لتعرف صحة الكلام الذي علّمت به
5Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
5كان في ايام هيرودس ملك اليهودية كاهن اسمه زكريا من فرقة ابيا وامرأته من بنات هرون واسمها اليصابات.
6Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
6وكانا كلاهما بارين امام الله سالكين في جميع وصايا الرب واحكامه بلا لوم.
7Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
7ولم يكن لهما ولد اذ كانت اليصابات عاقرا وكانا كلاهما متقدمين في أيامهما
8Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
8فبينما هو يكهن في نوبة فرقته امام الله
9Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
9حسب عادة الكهنوت اصابته القرعة ان يدخل الى هيكل الرب ويبخر.
10Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
10وكان كل جمهور الشعب يصلّون خارجا وقت البخور.
11Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
11فظهر له ملاك الرب واقفا عن يمين مذبح البخور.
12Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
12فلما رآه زكريا اضطرب ووقع عليه خوف.
13Lakini malaika akamwambia, "Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
13فقال له الملاك لا تخف يا زكريا لان طلبتك قد سمعت وامرأتك اليصابات ستلد لك ابنا وتسميه يوحنا.
14Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
14ويكون لك فرح وابتهاج وكثيرون سيفرحون بولادته.
15Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
15لانه يكون عظيما امام الرب وخمرا ومسكرا لا يشرب. ومن بطن امه يمتلئ من الروح القدس.
16Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
16ويرد كثيرين من بني اسرائيل الى الرب الههم.
17Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake."
17ويتقدم امامه بروح ايليا وقوته ليرد قلوب الآباء الى الابناء والعصاة الى فكر الابرار لكي يهيئ للرب شعبا مستعدا.
18Zakariya akamwambia huyo malaika, "Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu."
18فقال زكريا للملاك كيف اعلم هذا لاني انا شيخ وامرأتي متقدمة في ايامها.
19Malaika akamjibu, "Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
19فاجاب الملاك وقال له انا جبرائيل الواقف قدام الله وأرسلت لاكلمك وابشرك بهذا.
20Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia."
20وها انت تكون صامتا ولا تقدر ان تتكلم الى اليوم الذي يكون فيه هذا لانك لم تصدق كلامي الذي سيتم في وقته.
21Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
21وكان الشعب منتظرين زكريا ومتعجبين من ابطائه في الهيكل.
22Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
22فلما خرج لم يستطع ان يكلمهم ففهموا انه قد رأى رؤيا في الهيكل. فكان يومئ اليهم وبقي صامتا
23Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
23ولما كملت ايام خدمته مضى الى بيته.
24Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
24وبعد تلك الايام حبلت اليصابات امرأته واخفت نفسها خمسة اشهر قائلة
25"Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu."
25هكذا قد فعل بي الرب في الايام التي فيها نظر اليّ لينزع عاري بين الناس
26Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
26وفي الشهر السادس أرسل جبرائيل الملاك من الله الى مدينة من الجليل اسمها ناصرة
27kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
27الى عذراء مخطوبة لرجل من بيت داود اسمه يوسف. واسم العذراء مريم.
28Malaika akamwendea, akamwambia, "Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe."
28فدخل اليها الملاك وقال سلام لك ايتها المنعم عليها. الرب معك مباركة انت في النساء.
29Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
29فلما رأته اضطربت من كلامه وفكرت ما عسى ان تكون هذه التحية.
30Malaika akamwambia, "Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
30فقال لها الملاك لا تخافي يا مريم لانك قد وجدت نعمة عند الله.
31Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
31وها انت ستحبلين وتلدين ابنا وتسمينه يسوع.
32Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
32هذا يكون عظيما وابن العلي يدعى ويعطيه الرب الاله كرسي داود ابيه.
33Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho."
33ويملك على بيت يعقوب الى الابد ولا يكون لملكه نهاية
34Maria akamjibu, "Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?"
34فقالت مريم للملاك كيف يكون هذا وانا لست اعرف رجلا.
35Malaika akamjibu, "Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
35فاجاب الملاك وقال لها. الروح القدس يحل عليك وقوة العلي تظللك فلذلك ايضا القدوس المولود منك يدعى ابن الله.
36Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
36وهوذا اليصابات نسيبتك هي ايضا حبلى بابن في شيخوختها وهذا هو الشهر السادس لتلك المدعوة عاقرا.
37Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu."
37لانه ليس شيء غير ممكن لدى الله.
38Maria akasema, "Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema." Kisha yule malaika akaenda zake.
38فقالت مريم هوذا انا أمة الرب. ليكن لي كقولك. فمضى من عندها الملاك
39Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
39فقامت مريم في تلك الايام وذهبت بسرعة الى الجبال الى مدينة يهوذا.
40Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
40ودخلت بيت زكريا وسلمت على اليصابات.
41Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
41فلما سمعت اليصابات سلام مريم ارتكض الجنين في بطنها. وامتلأت اليصابات من الروح القدس.
42akasema kwa sauti kubwa, "Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
42وصرخت بصوت عظيم وقالت مباركة انت في النساء ومباركة هي ثمرة بطنك.
43Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
43فمن اين لي هذا ان تأتي ام ربي اليّ.
44Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
44فهوذا حين صار صوت سلامك في اذنيّ ارتكض الجنين بابتهاج في بطني.
45Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia."
45فطوبى للتي آمنت ان يتم ما قيل لها من قبل الرب
46Naye Maria akasema,
46فقالت مريم تعظم نفسي الرب
47"Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
47وتبتهج روحي بالله مخلّصي.
48Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
48لانه نظر الى اتضاع امته. فهوذا منذ الآن جميع الاجيال تطوبني.
49Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
49لان القدير صنع بي عظائم واسمه قدوس.
50Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
50ورحمته الى جيل الاجيال للذين يتقونه.
51Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
51صنع قوة بذراعه. شتّت المستكبرين بفكر قلوبهم.
52amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
52أنزل الاعزاء عن الكراسي ورفع المتضعين.
53Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
53اشبع الجياع خيرات وصرف الاغنياء فارغين.
54Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
54عضد اسرائيل فتاه ليذكر رحمة.
55Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele."
55كما كلم آباءنا. لابراهيم ونسله الى الابد.
56Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
56فمكثت مريم عندها نحو ثلاثة اشهر ثم رجعت الى بيتها
57Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
57واما اليصابات فتم زمانها لتلد فولدت ابنا.
58Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
58وسمع جيرانها واقرباؤها ان الرب عظّم رحمته لها ففرحوا معها.
59Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
59وفي اليوم الثامن جاءوا ليختنوا الصبي وسموه باسم ابيه زكريا.
60Lakini mama yake akasema, "La, sivyo, bali ataitwa Yohane."
60فاجابت امه وقالت لا بل يسمى يوحنا.
61Wakamwambia, "Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?"
61فقالوا لها ليس احد في عشيرتك تسمى بهذا الاسم.
62Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
62ثم اومأوا الى ابيه ماذا يريد ان يسمى.
63Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: "Yohane ndilo jina lake." Wote wakastaajabu.
63فطلب لوحا وكتب قائلا اسمه يوحنا. فتعجب الجميع.
64Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
64وفي الحال انفتح فمه ولسانه وتكلم وبارك الله.
65Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
65فوقع خوف على كل جيرانهم. وتحدّث بهذه الأمور جميعها في كل جبال اليهودية.
66Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: "Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?" Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
66فاودعها جميع السامعين في قلوبهم قائلين اترى ماذا يكون هذا الصبي. وكانت يد الرب معه
67Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
67وامتلأ زكريا ابوه من الروح القدس وتنبأ قائلا
68"Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
68مبارك الرب اله اسرائيل لانه افتقد وصنع فداء لشعبه.
69Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
69واقام لنا قرن خلاص في بيت داود فتاه.
70Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu,
70كما تكلم بفم انبيائه القديسين الذين هم منذ الدهر.
71kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
71خلاص من اعدائنا ومن ايدي جميع مبغضينا.
72Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
72ليصنع رحمة مع آبائنا ويذكر عهده المقدس.
73Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
73القسم الذي حلف لابراهيم ابينا
74tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
74ان يعطينا اننا بلا خوف منقذين من ايدي اعدائنا نعبده
75kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
75بقداسة وبر قدامه جميع ايام حياتنا.
76Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
76وانت ايها الصبي نبي العلي تدعى لانك تتقدم امام وجه الرب لتعدّ طرقه.
77kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
77لتعطي شعبه معرفة الخلاص بمغفرة خطاياهم
78Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
78باحشاء رحمة الهنا التي بها افتقدنا المشرق من العلاء.
79na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani."
79ليضيء على الجالسين في الظلمة وظلال الموت لكي يهدي اقدامنا في طريق السلام.
80Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.
80اما الصبي فكان ينمو ويتقوى بالروح وكان في البراري الى يوم ظهوره لاسرائيل