Swahili: New Testament

الكتاب المقدس (Van Dyke)

Luke

24

1Jumapili, alfajiri na mapema, wale wanawake walikwenda kaburini wakichukua yale manukato waliyotayarisha.
1ثم في اول الاسبوع اول الفجر أتين الى القبر حاملات الحنوط الذي أعددنه ومعهنّ اناس.
2Walikuta lile jiwe limeviringishwa mbali na kaburi.
2فوجدن الحجر مدحرجا عن القبر.
3Walipoingia ndani, hawakuona mwili wa Bwana Yesu.
3فدخلن ولم يجدن جسد الرب يسوع.
4Walipokuwa bado wanashangaa juu ya jambo hilo, mara watu wawili waliovaa mavazi yenye kung'aa sana, wakasimama karibu nao.
4وفيما هنّ محتارات في ذلك اذا رجلان وقفا بهنّ بثياب براقة.
5Hao wanawake wakaingiwa na hofu, wakainama chini. Ndipo wale watu wakawaambia, "Kwa nini mnamtafuta aliye hai kati ya wafu?
5واذ كنّ خائفات ومنكسات وجوههنّ الى الارض قالا لهنّ. لماذا تطلبن الحي بين الاموات.
6Hayuko hapa; amefufuka. Kumbukeni aliyowaambieni alipokuwa kule Galilaya:
6ليس هو ههنا لكنه قام. اذكرن كيف كلمكنّ وهو بعد في الجليل
7Ni lazima Mwana wa Mtu atolewe kwa watu waovu, nao watamsulubisha, na siku ya tatu atafufuka."
7قائلا انه ينبغي ان يسلّم ابن الانسان في ايدي اناس خطاة ويصلب وفي اليوم الثالث يقوم.
8Hapo wanawake wakayakumbuka maneno yake,
8فتذكرن كلامه.
9wakarudi kutoka kaburini, wakawapa mitume wale kumi na mmoja na wengine habari za mambo hayo yote.
9ورجعن من القبر واخبرن الاحد عشر وجميع الباقين بهذا كله.
10Hao waliotoa habari hizo kwa mitume ni: Maria Magdalene, Yoana na Maria mama wa Yakobo, pamoja na wanawake wengine walioandamana nao.
10وكانت مريم المجدلية ويونّا ومريم ام يعقوب والباقيات معهنّ اللواتي قلن هذا للرسل.
11Mitume waliyachukua maneno hayo kama yasiyo na msingi, hivyo hawakuamini.
11فتراءى كلامهنّ لهم كالهذيان ولم يصدقوهنّ.
12Lakini Petro alitoka, akaenda mbio hadi kaburini. Alipoinama kuchungulia ndani, akaiona tu ile sanda. Akarudi nyumbani huku akiwa anashangaa juu ya hayo yaliyotokea.
12فقام بطرس وركض الى القبر فانحنى ونظر الاكفان موضوعة وحدها فمضى متعجبا في نفسه مما كان
13Siku hiyohiyo, wawili kati ya wafuasi wake Yesu wakawa wanakwenda katika kijiji kimoja kiitwacho Emau, umbali wa kilomita kumi na moja kutoka Yerusalemu.
13واذا اثنان منهم كانا منطلقين في ذلك اليوم الى قرية بعيدة عن اورشليم ستين غلوة اسمها عمواس.
14Wakawa wanazungumza juu ya hayo yote yaliyotukia.
14وكانا يتكلمان بعضهما مع بعض عن جميع هذه الحوادث.
15Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akatokea, akatembea pamoja nao.
15وفيما هما يتكلمان ويتحاوران اقترب اليهما يسوع نفسه وكان يمشي معهما.
16Walimwona kwa macho, lakini hawakumtambua.
16ولكن أمسكت اعينهما عن معرفته.
17Akawauliza, "Mnazungumza nini huku mnatembea?" Nao wakasimama kimya, nyuso zao wamezikunja kwa huzuni.
17فقال لهما ما هذا الكلام الذي تتطارحان به وانتما ماشيان عابسين.
18Mmoja, aitwaye Kleopa, akamjibu, "Je, wewe ni mgeni peke yako Yerusalemu ambaye hujui yaliyotukia huko siku hizi?"
18فاجاب احدهما الذي اسمه كليوباس وقال له هل انت متغرب وحدك في اورشليم ولم تعلم الامور التي حدثت فيها في هذه الايام.
19Naye akawajibu, "Mambo gani?" Wao wakamjibu, "Mambo yaliyompata Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii mwenye uwezo wa kutenda na kufundisha mbele ya Mungu na mbele ya watu wote.
19فقال لهما وما هي. فقالا المختصة بيسوع الناصري الذي كان انسانا نبيا مقتدرا في الفعل والقول امام الله وجميع الشعب.
20Makuhani na watawala wetu walimtoa ahukumiwe kufa, wakamsulubisha.
20كيف اسلمه رؤساء الكهنة وحكامنا لقضاء الموت وصلبوه.
21Lakini sisi tulitumaini kwamba yeye ndiye angeikomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu mambo hayo yalipotendeka.
21ونحن كنا نرجو انه هو المزمع ان يفدي اسرائيل. ولكن مع هذا كله اليوم له ثلاثة ايام منذ حدث ذلك.
22Tena, wanawake wengine wa kwetu wametushtua. Walikwenda kaburini mapema asubuhi,
22بل بعض النساء منا حيرننا اذ كنّ باكرا عند القبر.
23wasiukute mwili wake. Wakarudi wakasema kwamba walitokewa na malaika waliowaambia kwamba alikuwa hai.
23ولما لم يجدن جسده أتين قائلات انهنّ رأين منظر ملائكة قالوا انه حيّ.
24Wengine wetu walikwenda kaburini wakashuhudia yale waliyosema hao wanawake; ila yeye hawakumwona."
24ومضى قوم من الذين معنا الى القبر فوجدوا هكذا كما قالت ايضا النساء واما هو فلم يروه.
25Kisha Yesu akawaambia, "Mbona mu wapumbavu kiasi hicho na mioyo yenu ni mizito hivyo kusadiki yote yaliyonenwa na manabii?
25فقال لهما ايها الغبيان والبطيئا القلوب في الايمان بجميع ما تكلم به الانبياء.
26Je, haikumpasa Kristo kuteswa, na hivyo aingie katika utukufu wake?"
26أما كان ينبغي ان المسيح يتألم بهذا ويدخل الى مجده.
27Akawafafanulia mambo yote yaliyomhusu yeye katika Maandiko Matakatifu kuanzia Mose hadi manabii wote.
27ثم ابتدأ من موسى ومن جميع الانبياء يفسر لهما الأمور المختصة به في جميع الكتب
28Walipokikaribia kile kijiji walikokuwa wanakwenda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea na safari;
28ثم اقتربوا الى القرية التي كانا منطلقين اليها وهو تظاهر كانه منطلق الى مكان ابعد.
29lakini wao wakamsihi wakisema, "Kaa pamoja nasi, maana kunakuchwa, na usiku unakaribia." Basi, akaingia kijijini, akakaa pamoja nao.
29فالزماه قائلين امكث معنا لانه نحو المساء وقد مال النهار. فدخل ليمكث معهما.
30Alipoketi kula chakula pamoja nao, akachukua mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.
30فلما اتكأ معهما اخذ خبزا وبارك وكسّر وناولهما.
31Mara macho yao yakafumbuliwa, wakamtambua; lakini yeye akatoweka kati yao.
31فانفتحت اعينهما وعرفاه ثم اختفى عنهما.
32Basi, wakaambiana, "Je, mioyo yetu haikuwa inawaka ndani yetu wakati alipokuwa anatufafanulia Maandiko Matakatifu kule njiani?"
32فقال بعضهما لبعض ألم يكن قلبنا ملتهبا فينا اذ كان يكلمنا في الطريق ويوضح لنا الكتب.
33Wakaondoka saa ileile, wakarudi Yerusalemu: wakawakuta wale mitume kumi na mmoja na wale wengine waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika
33فقاما في تلك الساعة ورجعا الى اورشليم ووجدا الاحد عشر مجتمعين هم والذين معهم
34wakisema, "Hakika Bwana amefufuka, amemtokea Simoni."
34وهم يقولون ان الرب قام بالحقيقة وظهر لسمعان.
35Basi, hao wafuasi wawili wakawajulisha yale yaliyowapata njiani, na jinsi walivyomtambua katika kumega mkate.
35واما هما فكانا يخبران بما حدث في الطريق وكيف عرفاه عند كسر الخبز
36Wanafunzi wote wawili walipokuwa wakiwaambia hayo, Yesu mwenyewe akasimama kati yao, akawaambia "Amani kwenu."
36وفيما هم يتكلمون بهذا وقف يسوع نفسه في وسطهم وقال لهم سلام لكم.
37Wakashtuka na kushikwa na hofu wakidhani wameona mzimu.
37فجزعوا وخافوا وظنوا انهم نظروا روحا.
38Lakini yeye akawaambia, "Kwa nini mnafadhaika? Mbona mnakuwa na mashaka mioyoni mwenu?
38فقال لهم ما بالكم مضطربين ولماذا تخطر افكار في قلوبكم.
39Angalieni mikono na miguu yangu, ya kwamba ni mimi mwenyewe. Nipapaseni mkanione, maana mzimu hauna mwili na mifupa kama mnionavyo."
39انظروا يديّ ورجليّ اني انا هو. جسوني وانظروا فان الروح ليس له لحم وعظام كما ترون لي.
40Baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono na miguu.
40وحين قال هذا أراهم يديه ورجليه.
41Wakiwa bado katika hali ya kutosadiki kwa sababu ya furaha yao, na wakiwa wanastaajabu, akawauliza, "Mnacho chakula chochote hapa?"
41وبينما هم غير مصدقين من الفرح ومتعجبون قال لهم أعندكم ههنا طعام.
42Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.
42فناولوه جزءا من سمك مشوي وشيئا من شهد عسل.
43Akakichukua, akala, wote wakimwona.
43فأخذ وأكل قدامهم
44Halafu akawaambia, "Hii ndiyo maana ya maneno niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi: kwamba ilikuwa lazima kukamilisha yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Mose na katika vitabu vya manabii na katika kitabu cha Zaburi."
44وقال لهم هذا هو الكلام الذي كلمتكم به وانا بعد معكم انه لا بد ان يتم جميع ما هو مكتوب عني في ناموس موسى والانبياء والمزامير.
45Kisha, akaziangazia akili zao ili wapate kuelewa Maandiko Matakatifu.
45حينئذ فتح ذهنهم ليفهموا الكتب.
46Akawaambia, "Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka wafu,
46وقال لهم هكذا هو مكتوب وهكذا كان ينبغي ان المسيح يتألم ويقوم من الاموات في اليوم الثالث.
47na kwamba ni lazima, kwa jina lake, mataifa yote kuanzia na Yerusalemu yahubiriwe juu ya kutubu na kusamehewa dhambi.
47وان يكرز باسمه بالتوبة ومغفرة الخطايا لجميع الامم مبتدأ من اورشليم.
48Ninyi ni mashahidi wa mambo hayo.
48وانتم شهود لذلك.
49Nami mwenyewe nitawapelekeeni yule ambaye Baba aliahidi kumtuma, lakini ngojeni huku mjini mpaka mtakapopewa ile nguvu itokayo juu."
49وها انا ارسل اليكم موعد ابي. فاقيموا في مدينة اورشليم الى ان تلبسوا قوة من الاعالي
50Kisha akawaongoza nje ya mji hadi Bethania, akainua mikono yake juu, akawabariki.
50واخرجهم خارجا الى بيت عنيا. ورفع يديه وباركهم.
51Alipokuwa anawabariki, akawaacha; akachukuliwa mbinguni.
51وفيما هو يباركهم انفرد عنهم وأصعد الى السماء.
52Wao wakamwabudu, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kubwa:
52فسجدوا له ورجعوا الى اورشليم بفرح عظيم.
53wakakaa muda wote Hekaluni wakimsifu Mungu.
53وكانوا كل حين في الهيكل يسبّحون ويباركون الله آمين