Swahili: New Testament

الكتاب المقدس (Van Dyke)

Mark

3

1Yesu aliingia tena katika sunagogi na mle ndani mlikuwa na mtu aliyekuwa na mkono uliopooza.
1ثم دخل ايضا الى المجمع. وكان هناك رجل يده يابسة.
2Humo baadhi ya watu walimngojea amponye mtu huyo siku ya sabato ili wapate kumshtaki.
2فصاروا يراقبونه هل يشفيه في السبت. لكي يشتكوا عليه.
3Yesu akamwambia huyo mtu aliyekuwa na mkono uliopooza, "Njoo hapa katikati."
3فقال للرجل الذي له اليد اليابسة قم في الوسط.
4Kisha, akawauliza, "Je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuua?" Lakini wao hawakusema neno.
4ثم قال لهم هل يحل في السبت فعل الخير او فعل الشر. تخليص نفس او قتل. فسكتوا.
5Hapo akawatazama wote kwa hasira, akaona huzuni kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao. Kisha akamwambia huyo mtu, "Nyosha mkono wako!" Naye akaunyosha mkono wake, ukawa mzima tena.
5فنظر حوله اليهم بغضب حزينا على غلاظة قلوبهم وقال للرجل مدّ يدك. فمدها فعادت يده صحيحة كالاخرى.
6Mara Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri pamoja na watu wa kikundi cha Herode jinsi ya kumwangamiza Yesu.
6فخرج الفريسيون للوقت مع الهيرودسيين وتشاوروا عليه لكي يهلكوه
7Yesu aliondoka hapo pamoja na wanafunzi wake, akaenda kando ya ziwa, na umati wa watu ukamfuata. Watu hao walikuwa wametoka Yerusalemu, Yudea,
7فانصرف يسوع مع تلاميذه الى البحر وتبعه جمع كثير من الجليل ومن اليهودية
8Idumea, ng'ambo ya mto Yordani, Tiro na Sidoni. Watu hao wengi walimwendea Yesu kwa sababu ya kusikia mambo mengi aliyokuwa ameyatenda.
8ومن اورشليم ومن ادومية ومن عبر الاردن. والذين حول صور وصيدا جمع كثير اذ سمعوا كم صنع أتوا اليه.
9Yesu akawaambia wanafunzi wake wamtayarishie mashua moja, ili umati wa watu usije ukamsonga.
9فقال لتلاميذه ان تلازمه سفينة صغيرة لسبب الجمع كي لا يزحموه.
10Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.
10لانه كان قد شفى كثيرين حتى وقع عليه ليلمسه كل من فيه داء.
11Na watu waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu walipomwona, walijitupa chini mbele yake na kupaaza sauti, "Wewe ni Mwana wa Mungu!"
11والارواح النجسة حينما نظرته خرّت له وصرخت قائلة انك انت ابن الله.
12Lakini Yesu akawaamuru kwa ukali wasimjulishe kwa watu.
12واوصاهم كثيرا ان لا يظهروه
13Yesu alipanda kilimani, akawaita wale aliowataka. Basi, wakamwendea,
13ثم صعد الى الجبل ودعا الذين ارادهم فذهبوا اليه.
14naye akawateua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume, wakae naye, awatume kuhubiri
14واقام اثني عشر ليكونوا معه وليرسلهم ليكرزوا.
15na wawe na mamlaka ya kuwafukuza pepo.
15ويكون لهم سلطان على شفاء الامراض واخراج الشياطين.
16Basi, hao kumi na wawili walioteuliwa ndio hawa: Simoni (ambaye Yesu alimpa jina, Petro),
16وجعل لسمعان اسم بطرس.
17Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo (Yesu aliwapa hawa ndugu wawili jina Boanerge, maana yake "wanangurumo"),
17ويعقوب بن زبدي ويوحنا اخا يعقوب وجعل لهما اسم بوانرجس اي ابني الرعد.
18Andrea na Filipo, Batholomayo, Mathayo, Thoma, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkanani na
18واندراوس وفيلبس وبرثولماوس ومتى وتوما ويعقوب بن حلفى وتداوس وسمعان القانوي.
19Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
19ويهوذا الاسخريوطي الذي اسلمه. ثم أتوا الى بيت.
20Kisha Yesu alikwenda nyumbani. Umati wa watu ukakusanyika tena, hata Yesu na wafuasi wake wasiweze kupata nafasi ya kula chakula.
20فاجتمع ايضا جمع حتى لم يقدروا ولا على اكل خبز.
21Basi, watu wa jamaa yake walipopata habari hiyo wakatoka kwenda kumchukua maana walikuwa wanasema kwamba amepatwa na wazimu.
21ولما سمع اقرباؤه خرجوا ليمسكوه لانهم قالوا انه مختل.
22Nao walimu wa Sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu, wakasema, "Ana Beelzebuli! Tena, anawafukuza pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo."
22واما الكتبة الذين نزلوا من اورشليم فقالوا ان معه بعلزبول. وانه برئيس الشياطين يخرج الشياطين.
23Hapo Yesu akawaita, akawaambia kwa mifano, "Shetani anawezaje kumfukuza Shetani?
23فدعاهم وقال لهم بامثال كيف يقدر شيطان ان يخرج شيطانا.
24Ikiwa utawala mmoja umegawanyika makundimakundi yanayopigana, utawala huo hauwezi kudumu.
24وان انقسمت مملكة على ذاتها لا تقدر تلك المملكة ان تثبت.
25Tena, ikiwa jamaa moja imegawanyika makundimakundi yanayopingana, jamaa hiyo itaangamia.
25وان انقسم بيت على ذاته لا يقدر ذلك البيت ان يثبت.
26Ikiwa basi, utawala wa Shetani umegawanyika vikundivikundi hauwezi kudumu, bali utaangamia kabisa.
26وان قام الشيطان على ذاته وانقسم لا يقدر ان يثبت بل يكون له انقضاء.
27"Hakuna mtu awezaye kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, isipokuwa kwanza amemfunga huyo mtu mwenye nguvu; hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
27لا يستطيع احد ان يدخل بيت قوي وينهب امتعته ان لم يربط القوي اولا وحينئذ ينهب بيته.
28"Kweli nawaambieni, watu watasamehewa dhambi zao zote na kufuru zao zote;
28الحق اقول لكم ان جميع الخطايا تغفر لبني البشر والتجاديف التي يجدفونها.
29lakini anayesema mabaya dhidi ya Roho Mtakatifu, hatasamehewa kamwe; ana hatia ya dhambi ya milele."
29ولكن من جدّف على الروح القدس فليس له مغفرة الى الابد بل هو مستوجب دينونة ابدية.
30(Yesu alisema hivyo kwa sababu walikuwa wanasema, "Ana pepo mchafu.")
30لانهم قالوا ان معه روحا نجسا
31Mama yake Yesu na ndugu zake walifika hapo, wakasimama nje, wakampelekea ujumbe kutaka kumwona.
31فجاءت حينئذ اخوته وامه ووقفوا خارجا وارسلوا اليه يدعونه.
32Umati wa watu ulikuwa umekaa hapo kumzunguka. Basi, wakamwambia, "Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kukuona."
32وكان الجمع جالسا حوله فقالوا له هوذا امك واخوتك خارجا يطلبونك.
33Yesu akawaambia, "Mama yangu na ndugu zangu ni kina nani?"
33فاجابهم قائلا من امي واخوتي.
34Hapo akawatazama watu waliokuwa wamemzunguka, akasema, "Tazameni! Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
34ثم نظر حوله الى الجالسين وقال ها امي واخوتي.
35Mtu yeyote anayefanya anayotaka Mungu, huyo ndiye kaka yangu, dada yangu na mama yangu."
35لان من يصنع مشيئة الله هو اخي واختي وامي