Swahili: New Testament

الكتاب المقدس (Van Dyke)

Matthew

22

1Yesu alisema nao tena kwa kutumia mifano:
1وجعل يسوع يكلمهم ايضا بامثال قائلا.
2"Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme aliyemwandalia mwanawe karamu ya arusi.
2يشبه ملكوت السموات انسانا ملكا صنع عرسا لابنه.
3Basi, akawatuma watumishi kuwaita walioalikwa waje arusini, lakini walioalikwa hawakutaka kufika.
3وارسل عبيده ليدعوا المدعوين الى العرس فلم يريدوا ان يأتوا.
4Akawatuma tena watumishi wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa: karamu yangu iko tayari sasa; fahali wangu na ng'ombe wanono wamekwisha chinjwa; kila kitu ni tayari, njoni arusini.
4فارسل ايضا عبيدا آخرين قائلا قولوا للمدعوين هوذا غذائي اعددته. ثيراني ومسمناتي قد ذبحت وكل شيء معد. تعالوا الى العرس.
5Lakini wao hawakujali, wakaenda zao; mmoja shambani kwake, mwingine kwenye shughuli zake,
5ولكنهم تهاونوا ومضوا واحد الى حقله وآخر الى تجارته.
6na wengine wakawakamata wale watumishi wakawatukana, wakawaua.
6والباقون امسكوا عبيده وشتموهم وقتلوهم.
7Yule mfalme akakasirika, akawatuma askari wake wakawaangamize wauaji hao na kuuteketeza mji wao.
7فلما سمع الملك غضب وارسل جنوده واهلك أولئك القاتلين واحرق مدينتهم.
8Kisha akawaambia watumishi wake: Karamu ya arusi iko tayari kweli, lakini walioalikwa hawakustahili.
8ثم قال لعبيده اما العرس فمستعد واما المدعوون فلم يكونوا مستحقين.
9Basi, nendeni kwenye barabara na wowote wale mtakaowakuta waiteni waje arusini.
9فاذهبوا الى مفارق الطرق وكل من وجدتموه فادعوه الى العرس.
10Wale watumishi wakatoka, wakaenda njiani, wakawaleta watu wote, wabaya na wema. Nyumba ya arusi ikajaa wageni.
10فخرج أولئك العبيد الى الطرق وجمعوا كل الذين وجدوهم اشرارا وصالحين. فامتلأ العرس من المتكئين.
11"Mfalme alipoingia kuwaona wageni, akamwona mtu mmoja ambaye hakuvaa mavazi ya arusi.
11فلما دخل الملك لينظر المتكئين رأى هناك انسانا لم يكن لابسا لباس العرس.
12Mfalme akamwuliza, Rafiki, umeingiaje hapa bila vazi la arusi? Lakini yeye akakaa kimya.
12فقال له يا صاحب كيف دخلت الى هنا وليس عليك لباس العرس. فسكت.
13Hapo mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni miguu na mikono mkamtupe nje gizani; huko atalia na kusaga meno."
13حينئذ قال الملك للخدام اربطوا رجليه ويديه وخذوه واطرحوه في الظلمة الخارجية. هناك يكون البكاء وصرير الاسنان.
14Yesu akamaliza kwa kusema, "Wengi wamealikwa, lakini wachache wameteuliwa."
14لان كثيرين يدعون وقليلين ينتخبون
15Kisha, Mafarisayo wakaenda zao, wakashauriana jinsi ya kumnasa Yesu kwa maneno yake.
15حينئذ ذهب الفريسيون وتشاوروا لكي يصطادوه بكلمة.
16Basi, wakawatuma wafuasi wao pamoja na wafuasi wa kikundi cha Herode. Wakamwuliza, "Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwaminifu, na kwamba wafundisha njia ya Mungu kwa uaminifu; humwogopi mtu yeyote, maana cheo cha mtu si kitu kwako.
16فارسلوا اليه تلاميذهم مع الهيرودسيين قائلين يا معلّم نعلم انك صادق وتعلّم طريق الله بالحق ولا تبالي باحد لانك لا تنظر الى وجوه الناس.
17Haya, twambie maoni yako. Je, ni halali au la, kulipa Kaisari?"
17فقل لنا ماذا تظن. أيجوز ان تعطى جزية لقيصر ام لا.
18Lakini Yesu alitambua uovu wao, akawaambia, "Enyi
18فعلم يسوع خبثهم وقال لماذا تجربونني يا مراؤون.
19Nionyesheni fedha ya kulipia kodi." Nao wakamtolea sarafu ya fedha. sarafu ya fedha.
19أروني معاملة الجزية. فقدموا له دينارا.
20Basi, Yesu akawauliza, "Sura na chapa hii ni ya nani?"
20فقال لهم لمن هذه الصورة والكتابة.
21Wakamjibu, "Ni vya Kaisari." Hapo Yesu akawaambia, "Basi, mpeni Kaisari yaliyo yake Kaisari, na Mungu yaliyo yake Mungu."
21قالوا له لقيصر. فقال لهم اعطوا اذا ما لقيصر لقيصر وما للّه للّه.
22Waliposikia hivyo wakashangaa; wakamwacha, wakaenda zao.
22فلما سمعوا تعجبوا وتركوه ومضوا
23Siku hiyo, baadhi ya Masadukayo walimwendea Yesu. Hao ndio wale wasemao kwamba wafu hawafufuki.
23في ذلك اليوم جاء اليه صدوقيون الذين يقولون ليس قيامة فسألوه
24Basi, wakamwambia, "Mwalimu, Mose alisema mtu aliyeoa akifa bila kuacha watoto, lazima ndugu yake amwoe huyo mama mjane, amzalie ndugu yake watoto.
24قائلين يا معلّم قال موسى ان مات احد وليس له اولاد يتزوج اخوه بامرأته ويقم نسلا لاخيه.
25Sasa, hapa petu palikuwa na ndugu saba. Wa kwanza alioa kisha akafa bila kujaliwa watoto, akamwachia ndugu yake huyo mke wake mjane.
25فكان عندنا سبعة اخوة وتزوج الاول ومات. واذ لم يكن له نسل ترك امرأته لاخيه.
26Ikawa vivyo hivyo kwa ndugu wa pili, na wa tatu, mpaka wa saba.
26وكذلك الثاني والثالث الى السبعة.
27Baada ya ndugu hao wote kufa, akafa pia yule mama.
27وآخر الكل ماتت المرأة ايضا.
28Je, siku wafu watakapofufuka mama huyo atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba? Maana Wote saba walimwoa."
28ففي القيامة لمن من السبعة تكون زوجة. فانها كانت للجميع.
29Yesu akawajibu, "Kweli mmekosea kwa sababu hamjui Maandiko Matakatifu wala nguvu ya Mungu!
29فاجاب يسوع وقال لهم تضلون اذ لا تعرفون الكتب ولا قوة الله.
30Maana wafu watakapofufuliwa hawataoa wala kuolewa, watakuwa kama malaika mbinguni.
30لانهم في القيامة لا يزوجون ولا يتزوجون بل يكونون كملائكة الله في السماء.
31Lakini kuhusu suala la wafu kufufuka, hamjasoma yale aliyowaambieni Mungu?
31واما من جهة قيامة الاموات أفما قرأتم ما قيل لكم من قبل الله القائل
32Aliwaambia, Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo! Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai."
32انا اله ابراهيم واله اسحق واله يعقوب. ليس الله اله اموات بل اله احياء.
33Ule umati wa watu uliposikia hivyo ukayastaajabia mafundisho yake.
33فلما سمع الجموع بهتوا من تعليمه
34Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, wakakutana pamoja.
34اما الفريسيون فلما سمعوا انه ابكم الصدوقيين اجتمعوا معا.
35Mmoja wao, mwanasheria, akamwuliza Yesu kwa kumjaribu,
35وسأله واحد منهم وهو ناموسي ليجربه قائلا
36"Mwalimu, ni amri ipi iliyo kuu katika Sheria ya Mose?"
36يا معلّم اية وصية هي العظمى في الناموس.
37Yesu akamjibu, "Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote na kwa akili yako yote.
37فقال له يسوع تحب الرب الهك من كل قلبك ومن كل نفسك ومن كل فكرك.
38Hii ndiyo amri kuu ya kwanza.
38هذه هي الوصية الاولى والعظمى.
39Ya pili inafanana na hiyo: Mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe.
39والثانية مثلها. تحب قريبك كنفسك.
40Sheria yote ya Mose na mafundisho ya manabii vinategemea amri hizi mbili."
40بهاتين الوصيتين يتعلق الناموس كله والانبياء
41Mafarisayo walipokusanyika pamoja, Yesu aliwauliza,
41وفيما كان الفريسيون مجتمعين سألهم يسوع
42"Ninyi mwaonaje juu ya Kristo? Je, ni mwana wa nani?" Wakamjibu, "Wa Daudi."
42قائلا ماذا تظنون في المسيح. ابن من هو. قالوا له ابن داود.
43Yesu akawaambia, "Basi, inawezekanaje kwamba kwa nguvu ya Roho Mtakatifu Daudi anamwita yeye Bwana? Maana alisema:
43قال لهم فكيف يدعوه داود بالروح ربا قائلا
44Bwana alimwambia Bwana wangu: keti upande wangu wa kulia, mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako.
44قال الرب لربي اجلس عن يميني حتى اضع اعداءك موطئا لقدميك.
45Basi, ikiwa Daudi anamwita Kristo Bwana, anawezaje kuwa mwanawe?"
45فان كان داود يدعوه ربا فكيف يكون ابنه.
46Hakuna mtu yeyote aliyeweza kumjibu neno. Na tangu siku hiyo hakuna aliyethubutu tena kumwuliza swali.
46فلم يستطع احد ان يجيبه بكلمة. ومن ذلك اليوم لم يجسر احد ان يسأله بتة