Swahili: New Testament

American Standard Version

1 Corinthians

10

1Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
1For I would not, brethren, have you ignorant, that our fathers were all under the cloud, and all passed through the sea;
2Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
2and were all baptized unto Moses in the cloud and in the sea;
3Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
3and did all eat the same spiritual food;
4wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
4and did all drink the same spiritual drink: for they drank of a spiritual rock that followed them: and the rock was Christ.
5Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
5Howbeit with most of them God was not well pleased: for they were overthrown in the wilderness.
6Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
6Now these things were our examples, to the intent we should not lust after evil things, as they also lusted.
7Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: "Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza."
7Neither be ye idolaters, as were some of them; as it is written, The people sat down to eat and drink, and rose up to play.
8Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
8Neither let us commit fornication, as some of them committed, and fell in one day three and twenty thousand.
9Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
9Neither let us make trial of the Lord, as some of them made trial, and perished by the serpents.
10Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
10Neither murmur ye, as some of them murmured, and perished by the destroyer.
11Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili.
11Now these things happened unto them by way of example; and they were written for our admonition, upon whom the ends of the ages are come.
12Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
12Wherefore let him that thinketh he standeth take heed lest he fall.
13Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
13There hath no temptation taken you but such as man can bear: but God is faithful, who will not suffer you to be tempted above that ye are able; but will with the temptation make also the way of escape, that ye may be able to endure it.
14Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
14Wherefore, my beloved, flee from idolatry.
15Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
15I speak as to wise men; judge ye what I say.
16Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
16The cup of blessing which we bless, is it not a communion of the blood of Christ? The bread which we break, is it not a communion of the body of Christ?
17Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
17seeing that we, who are many, are one bread, one body: for we are all partake of the one bread.
18Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
18Behold Israel after the flesh: have not they that eat the sacrifices communion with the altar?
19Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
19What say I then? that a thing sacrificed to idols is anything, or that an idol is anything?
20Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
20But [I say], that the things which the Gentiles sacrifice, they sacrifice to demons, and not to God: and I would not that ye should have communion with demons.
21Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
21Ye cannot drink the cup of the Lord, and the cup of demons: ye cannot partake of the table of the Lord, and of the table of demons.
22Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
22Or do we provoke the Lord to jealousy? are we stronger than he?
23Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
23All things are lawful; but not all things are expedient. All things are lawful; but not all things edify.
24Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
24Let no man seek his own, but [each] his neighbor's [good].
25Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
25Whatsoever is sold in the shambles, eat, asking no question for conscience' sake,
26maana Maandiko yasema: "Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana."
26for the earth is the Lord's, and the fulness thereof.
27Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
27If one of them that believe not biddeth you [to a feast], and ye are disposed to go; whatsoever is set before you, eat, asking no question for conscience' sake.
28Lakini mtu akiwaambieni: "Chakula hiki kimetambikiwa sanamu," basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
28But if any man say unto you, This hath been offered in sacrifice, eat not, for his sake that showed it, and for conscience sake:
29Nasema, "kwa ajili ya dhamiri," si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: "Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
29conscience, I say, not thine own, but the other's; for why is my liberty judged by another conscience?
30Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?"
30If I partake with thankfulness, why am I evil spoken of for that for which I give thanks?
31Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
31Whether therefore ye eat, or drink, or whatsoever ye do, do all to the glory of God.
32Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
32Give no occasions of stumbling, either to Jews, or to Greeks, or to the church of God:
33Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.
33even as I also please all men in all things, not seeking mine own profit, but the [profit] of the many, that they may be saved.